Jumakidogo
R I P
- Jul 16, 2009
- 1,851
- 417
CCM mko wapi kuja kujibu mapigo ya wapinzani hasa chama kikuu cha upinzani kwenu CDM. Naona mmebaki jeshi la mtu mmoja mmoja huku mkimwacha Nape peke yake acheze nafasi zote uwanjani, goli kipa yeye! Beki yeye, kiungo mkabaji yeye, kiungo mshambuliaji yeye, refari yeye, kualika mashabiki yeye! Yote katika mechi moja tu. Pumzika kaka, au chama ndiyo mwisho wake umewadia? Manake naona pambano lenu na CDM ni sawa na kumpambanisha Tyson na Maneno Osward.