CCM Kagera yawafukuza madiwani wake 8

Nadhani sasa tupo bize na mabaraza ya katiba+uchaguzi wa ndani wa chama... CCM malizaneni na madiwani wenu huko, hatuna mda wa chaguzi ndogo ndogo... Tutaonana 2015....
 
Mmh! Kazi ipo...siasa hizi zitatufikisha pasipo. Sio bure, kuna mengi na makubwa ndani yake. Let's wait and see

Sent from my BlackBerry 9900 using Jamii Forums.
 
Teh teh teh ati Magamba wameiga Chadema kila kifanywacho na Chadema Mijigamba nayo huiga, kule Arusha Chadema ilifukuza mafisadi na CCM Bukoba walifukuza wakataa Ufisadi patamu hapo, sasa hapa ni kwamba moja Kwa moja Chadema ina Madiwani 12 Kwa kuwa hata hatuhitaji uchaguzi au niseme tunasubiri kuwaapisha na Chadema inawachukua wote na kila mmoja anasimama kwenye kata yake kama mwanzo tu.Nasema wanafaa Kwa Chadema Kwa kuwa mbiu yao ni kuukataa ufisadi kama mbiu ya Chadema isemavyo na isitoshe waliungana na Madiwani wa Chadema kuanzia mwanzo Hadi mwisho sasa si mnaona Ukombozi unakuja.Hao Madiwani walianza na Mungu na watamaliza na Mungu nikiwa na maana ni saa ya ukombozi sasa.
 
Utaratibu huu ni angamizo la Demokrasia na ni Jeneza la CDM. Sipenda CDM kuruhusu tena Mateja kama Shibuda. Naamini CDM ina watu wengi wazuri wakuchukua nafasi hizo na Ukatumika utaratibu mzuri wa kuwapata wagombea wasio kuwa na tabia za PANYA, Baba mwizi, mama mwizi, mtoto mwizi, Panya wote wezi, achaneni na tabia hii mbovu ya kuokota MAKOMBO ya ccm. Sipendi kuona CDM ikichukuwa viongozi toka ccm. HAKUNA KIONGOZI ccm alie SALAMA wote wameathirika na VIRUSI vya UFISADI
wazo lako ni zuri, ila kwa upande mwingine ukirudi kwa hawa madiwani ni kwamba wao wanajiamini kuwa wana support kubwa ya wananchi na ndio maana wakakomaa mpaka wamefukuzwa uanachama.kuwaacha bila kuwapa a second chance iwe CDM au chama kingine itakuwa siyo kuwatendea haki. ni vizuri wakawaeleze wananchi ni nini walichokuwa wanapigania na waombe nafasi ya kuchaguliwa tena ili wakakamilishe kazi walioianza ya kupambana na ufisadi.
 
Binafsi nachukua nafasi hii kuwapongeza madiwan 8 wa ccm waliofukuzwa kwa kitendo cha kumpinga meya wa kifisadi wa ccm pia.nimeshangazwa sana kwa madiwani hao kuonesha ushujaa wao wa kumpinga meya anaetuhumiwa kwa ufisadi.

Popote walipo madiwani hawa,wanastahili pongez kubwa kwa kuonekana kuwatetea wanyonge.tumekuwa tukiisema ccm na serikali yake kuwa ni wezi na mafisadi ila ukisema tu unakamatwa au kutekwa kwa kuwa tu unataka kuibua ulaji wa wakubwa. Chadema wamekuwa wakisema waziwazi na wamekuwa wakipingwa hadharani hata ikabidi wapakaziwe kuwa ni magaidi,wadini,na ukabila,lengo ni kuhakikisha kuwa wanaizima chadema wasiseme serikali.

Madiwani hawa wameonesha mfano wa kuigwa na hata wanatupa alama kuwa serikali yote ya ccm ndiyo inayotumaliza watanzania kwa upotevu wa pesa. Swali kwa mh rais,hv ni kweli kuwa meya alikuwa na mzozo binafsi na mbunge kagasheki? Sasa imekuaje madiwani wafukuzwe na kagasheki akabaki? Au mgogoro wa wa2 hao umekwisha? Ni lini? Kuna uongo hapo..kauli hii inaonesha wazi kuwa ccm rushwa na wizi umetawala...docta slaa alisema 'itafika mahali nchi haitatawalika,.
Angalia ufisadi huu,: wajumbe waliokutana katka ukumbi wa hotel ya walij guard ni 55,wliosema ndiyo ni 50 huku 5 pekee wakisema hapana.gharama ya ukumbi huo ni tsh 150,000/= huku wajumbe wakilipwa posho 30,000/= kila mmoja, jumla kwa watu 55 ni sh 1,650,000/- bado chakula,vinywaj julisha gharama ya ukumbi...pesa zote hizo ccm iliyokopa kwa makampuni ya ujenzi wliopewa zabuni kwa vitisho kuwa meya akiondoka, hata wao hawtapata kitu.
Madiwani hawa nawashangaa pia kukataa mil 40 wlizoletewa wasitishe saini ya kutokuwa na imani na meya..kweli mmeokoka sijui lini..hongera..

Lakini pia meya anatuhumiwa kukopa bil 2.9 kutoka mfuko wa dhamana ya uwekezaji (UTT), mil 200 bila kibali cha baraza la madiwani,mradi wa kuosha magari kutumia mil 297,kushindwa kutoa mchanganuo wa mapato na matumizi ya miradi ya mil 134 ya ujenzi wa kituo cha mabasi...

Hongera tena madiwan mliofukuzwa na msijione kuwa hamfai hapana,kama tungekuwa na viongoz kama hawa serkalin hakika nchi hii ingekuwa tajiri..na sasa nmejua kwa nin ccm hawataki kuachia madaraka na hasa halmashauri zetu..
 
Wakikata rufaa watashinda! CCM haiwezi kuachia kata 8. Watazuga zuga then watawaachia na kurudi kwenye nafasi zao. CCM hana kifua.
 
Nimeangalia taarifa ya habari kutoka kituo cha itv usiku huu,nimesikitishwa na kushangazwa sana na taarifa ya kufuzwa kwa madiwani 8 huko Bukoba.kinachoonekana ni kwa kwamba kila anayechukizwa na wizi wa pesa za inchi hii ni adui mkubwa wa CCM,wametetea kuliwa kwa mamilioni ya pesa za wananchi badala ya kuungwa mkono na kusaidiwa wanaishia kufukuzwa?hii ni aibu kubwa kwa chama hiki.hakina huruma hata kidogo na watanzania,hii ni ishara ya wazi kuwa CCM ni wezi,ni majambazi wa mali za umma.Nawasihi wa TZ wenzangu tusikubali kufanywa wajinga na CCM tuikatae katakata,ujinga si ugonjwa hauhitaji dawa yoyote wala kwenda hosp,ni jambo la maamuzi tu.huitaji degree kutetea rasilimali za inchi hii.

hawana ubavu wa kuwafukuza hiyo ni danganya toto,,, utasikia nec imewarudisha,, ccm bwana wewe acha tu
 
Hawa madiwani watakuwa wame mkosea adabu aliye wachonga, na sasa Meya naye wata mtupa nje? usicheze na mchongaji wa wagombea udiwani, umeya na ubunge
 
Madiwani 8 ni mtaji tosha!!!

Lakini tuache utani kufukuza madiwani 8 si jambo dogo!! Kwa mara nyingine siasa zinaenda kutuingiza katika gharama za kijinga kabisa!!
Kweli kabisa, wengi hatutaliangalia hili katika mtazamo wa kiuchumi.Tutaishia kwenye nyuzi za kisiasa tu.Chaguzi zetu zinatumia nguvu nyingi mno,kazi za maana zote huwa zinasimama, watendaji karibu wote wataelekeza akili na macho yao huko.
 
Kwa ufupi
· “Msimamo wa madiwani waliotimuliwa ilikuwa ni kumtaka Meya wa Manispaa ya Bukoba kung’oka”.
· Bukoba: Chama cha Mapinduzi (CCM) mkoani Kagera kimewafukuza uanachama wa chama hicho, madiwani wake wanane kutokana na kile kilichoelezwa kuwa ni kukaidi maelekezo mbalimbali ya chama hicho, pia kushirikiana na upinzani kukihujumu.
· Madiwani waliotimuliwa ni wale Manispaa ya Bukoba ambao wamekuwa wakitajwa kumuunga mkono Mbunge wa Bukoba Mjini ambaye pia ni Waziri wa Maliasili na Utalii, Balozi Khamis Kagasheki ambaye amekuwa akivutana vikali na Meya wa Manispaa hiyo, Anatory Amani.
· Miongoni mwa waliotimuliwa ni Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Bukoba na Diwani wa Kashai, Yusuph Ngaiza, aliyepata kuwa mbunge wa muda mrefu wa Bukoba Mjini na baadaye Meya wa Manispaa hiyo, Samuel Ruhangisa ambaye ni Diwani wa Kitendagulo na Diwani wa Buhembe, Alexander Ngalinda ambaye pia alikuwa Naibu Meya.
· Katibu wa CCM wa Mkoa wa Kagera, Averin Mushi alisema uamuzi wa kuwatimua madiwani hao umefikiwa jana na halmashauri ya CCM ya Mkoa kwa kile alichosema ni kwa ajili ya “kulinda masilahi ya chama na wananchi wa Bukoba”.
· Ibara ya 93 (15) ya Katiba ya CCM inataja moja ya kazi za halmashauri ya chama hicho ngazi ya mkoa kuwa ni: “Kumwachisha au kumfukuza uongozi kiongozi yeyote ambaye uteuzi wake wa mwisho unafanywa na Halmashauri ya CCM ya Mkoa”.
· Hata hivyo kipengele cha 14 cha ibara hiyo ya 93 kinasema hatua kumwachisha au kumfukuza mtu uanachama itachukuliwa endapo halmashauri itaridhika kwamba tabia na mwenendo wake vinamwondolea sifa za uanachama.
· Hatua ya kuwafukuza uanachama madiwani hao ambao pia watakuwa wamepoteza nafasi zao za udiwani, imekuja siku chache tangu Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete alipozitaka pande zinazohusika katika mgogoro huo kumaliza kwa njia ya mazungumzo.
· “Madiwani wote wa CCM walioendelea na mgomo hata baada ya maelekezo ya Mheshimiwa Rais kwa kusaini barua ya kutaka Mkurugenzi aitishe kikao cha kumwondoa Meya tumefikia uamuzi mgumu wa kuwafukuza uanachama kwa masilahi ya chama na wananchi wa Bukoba,’’ alisema Mushi.
· Mushi aliwataja madiwani wengine waliofukuzwa ni Robert Katunzi (Hamugembe), Deus Mutakyahwa (Nyanga), Richard Gasper (Miembeni), Mulungi Kichwabuta (Viti Maalumu) na Dauda Kalumuna aliyekuwa Diwani wa Ijuganyondo.
· Katibu huyo alisema Balozi Kagasheki na Meya Amani ambao mamlaka yao ya uteuzi ni ya kitaifa na wanatakiwa kumaliza tofauti zao kama walivyoelekezwa na Rais.
· Mgogoro uliosababisha madiwani hao kutimuliwa uliibuka baada ya Kagasheki kumtuhumu Meya Amani kwamba ameingiza Manispaa katika miradi ya ufisadi hali ilioibua makundi na kukwamisha kufanyika hata vikao vya Baraza la Madiwani.

Chanzo: MWANANCHI
 
Kwa ufupi
· “Msimamo wa madiwani waliotimuliwa ilikuwa ni kumtaka Meya wa Manispaa ya Bukoba kung’oka”.
· Bukoba: Chama cha Mapinduzi (CCM) mkoani Kagera kimewafukuza uanachama wa chama hicho, madiwani wake wanane kutokana na kile kilichoelezwa kuwa ni kukaidi maelekezo mbalimbali ya chama hicho, pia kushirikiana na upinzani kukihujumu.
· Madiwani waliotimuliwa ni wale Manispaa ya Bukoba ambao wamekuwa wakitajwa kumuunga mkono Mbunge wa Bukoba Mjini ambaye pia ni Waziri wa Maliasili na Utalii, Balozi Khamis Kagasheki ambaye amekuwa akivutana vikali na Meya wa Manispaa hiyo, Anatory Amani.
· Miongoni mwa waliotimuliwa ni Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Bukoba na Diwani wa Kashai, Yusuph Ngaiza, aliyepata kuwa mbunge wa muda mrefu wa Bukoba Mjini na baadaye Meya wa Manispaa hiyo, Samuel Ruhangisa ambaye ni Diwani wa Kitendagulo na Diwani wa Buhembe, Alexander Ngalinda ambaye pia alikuwa Naibu Meya.
· Katibu wa CCM wa Mkoa wa Kagera, Averin Mushi alisema uamuzi wa kuwatimua madiwani hao umefikiwa jana na halmashauri ya CCM ya Mkoa kwa kile alichosema ni kwa ajili ya “kulinda masilahi ya chama na wananchi wa Bukoba”.
· Ibara ya 93 (15) ya Katiba ya CCM inataja moja ya kazi za halmashauri ya chama hicho ngazi ya mkoa kuwa ni: “Kumwachisha au kumfukuza uongozi kiongozi yeyote ambaye uteuzi wake wa mwisho unafanywa na Halmashauri ya CCM ya Mkoa”.
· Hata hivyo kipengele cha 14 cha ibara hiyo ya 93 kinasema hatua kumwachisha au kumfukuza mtu uanachama itachukuliwa endapo halmashauri itaridhika kwamba tabia na mwenendo wake vinamwondolea sifa za uanachama.
· Hatua ya kuwafukuza uanachama madiwani hao ambao pia watakuwa wamepoteza nafasi zao za udiwani, imekuja siku chache tangu Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete alipozitaka pande zinazohusika katika mgogoro huo kumaliza kwa njia ya mazungumzo.
· “Madiwani wote wa CCM walioendelea na mgomo hata baada ya maelekezo ya Mheshimiwa Rais kwa kusaini barua ya kutaka Mkurugenzi aitishe kikao cha kumwondoa Meya tumefikia uamuzi mgumu wa kuwafukuza uanachama kwa masilahi ya chama na wananchi wa Bukoba,’’ alisema Mushi.
· Mushi aliwataja madiwani wengine waliofukuzwa ni Robert Katunzi (Hamugembe), Deus Mutakyahwa (Nyanga), Richard Gasper (Miembeni), Mulungi Kichwabuta (Viti Maalumu) na Dauda Kalumuna aliyekuwa Diwani wa Ijuganyondo.
· Katibu huyo alisema Balozi Kagasheki na Meya Amani ambao mamlaka yao ya uteuzi ni ya kitaifa na wanatakiwa kumaliza tofauti zao kama walivyoelekezwa na Rais.
· Mgogoro uliosababisha madiwani hao kutimuliwa uliibuka baada ya Kagasheki kumtuhumu Meya Amani kwamba ameingiza Manispaa katika miradi ya ufisadi hali ilioibua makundi na kukwamisha kufanyika hata vikao vya Baraza la Madiwani.

Chanzo: MWANANCHI
Mbona sasa Hawaii inasemekana wanatetea uamuzi aw wanna hi? Sasa hizi ni me hi nyingi. Waenda CDMA, Hawaii wanafaa katika nguvu ya umma.
 
Wakati mwingine wa kushuhudia nguvu za vyama kisera umewadia, another moment for CDM kujiongezea namba za madiwani katika halmashauri ya mji wa Bukoba.
Am kweli wapambanapo mafahari wawili ziumiazo ni nyasi.
 
Back
Top Bottom