CCM ivunjike tu

Simkubali Lowassa, lakini kama ikitokea amepewa ridhaa ya chama, mimi na kundi langu kwa pamoja tutamuunga mkono katika uchaguzi mkuu. Ieleweke wazi, Lowassa yupo chini ya CCM na kamwe hawezi kulipiza visasi kwa yeyote yule aliyewahi kuwa kinyume nae au mtu yeyote katika kambi yake. Kwa mnaosubiri CCM ivunjike, mtasubiri sana.

Rai yangu: Imarisheni vyama vyenu vya upinzani ili tuwe na ushindani, hii ya kuvizia mchezaji apate jeraha ili ndio mpate ushindi ni katika kutia huruma. Imarisheni vyama vyenu.
 
Lowassa hawezi kuenguliwa na ndilo hofu na tumaini la wengi. Kama ataenguliwa basi CCM itapona japo sasa hivi ipo ICU watu hawajui tu ila wao wanajua hilo. Wala sio wasiwasi ya Lowassa kukihama chama bali vichwa haswa wamejiandaa kukihama chama kama Lowassa atapita uchaguzi CCM na hiki ndicho UKAWA wanakisubiri mwaka huu 2015 - kazi kwisha... Ya Mwanakijiji yametimia.

Mkuu Mkandara nimekuelewa kwa sana hapa.

Surprisingly watu hawajawahi kuliona hili. Time will tell.
 
Last edited by a moderator:
Niliwahi sema na nitaendela kusema tena kuwa haya yanayotokea ndani ya chama kikongwe na tawala ni lazima yatokee ili mabadiliko yatokee. Bila haya yanayotokea watanzania hawawezi fanya mabadiliko kamwe hata iweje!! Naamini ni mpango wa Muumba wetu baada ya kuona tumelalamika sana bila kuchukua hatua, na sasa anachukua hatua yeye kwa namna yake, hakika muda wa watanzania kukombolewa umefika.......Chocheeeni kuni.
 
Mzee Mwanakijiji, uliyoyaandika ni bayana. Hatimaye yaliyotabiriwa yanaelekea kutimia. Inafurahisha na ninapata amani ya moyo kwani kupasuka kwa CCM ndiyo mwanzo wa "Tanzania Mpya". Hawawezi kukatana majina kwa upande mmoja, na hawajajiandaa kushindwa kwa upande mwingine. Uongozi kwao ni kama bidhaa, Mwenye pesa nyingi ndiye mshindi. MUNGU IBARIKI TANZANIA.
 
Last edited by a moderator:
Hili ndilo tatizo kubwa la nchi hii na watu wake, hatuna uthubutu. The Boss, ni chama kipi kingine kimewahi kukamata madaraka ya nchi hii hadi useme hakuna replacement inayoaminika? Unatumia vigezo gani? Yaani unataka kuwaambia Watanzania waendelee kuongozwa na dead man walking kuliko kuwapa wengine ambao angalau wanajitutumua? What kind of thinking is this? Comments kama hizi huwa zinanikera kweli kweli kwani ni kama vile hivi tumelogwa, taifa limejaa dead men walking! Fikiria tunao watu wanaosema, hapana imetosha, hatuwezi kuendelea na watu wale wale, ni heri tufanye mabadiliko halafu anakuja mwingine anadai haoni mbadala, heri tuendelee na wale wale!

I understand, change can be scary. Doing anything for the first time or stepping into the unknown can at times be frightening and so requires courage and resolve, two ingredients most of us Tanzanians lack. But when one has hit rock bottom like we have, the only way out is up. It is insane to expect the same minds that led us into the pit to take us out of it hence the need for change; complete overhaul and complete about turn.

1.Fear of the UNKNOWN

2.Fear of DARING
 
vyombo vya dola vitakapoiacha ccm ijiendeshe kisiasa kama chama cha siasa, hapo hapo kitavunjika. ktk hali ilikoifikisha tanzania ni bora na nafuu sana ccm ikivunjika na kutoweka kabisa. hata kwa usalama wa taifa hili ccm haifai tena. ni bora iondoke iwe historia na tz ianze upya. naamini kama taifa tutaendelea zaidi kuliko kuwa tena chini ya utawala wa ccm
 
2-en-1116938c9f89284a9bf4058caef47ad7.jpg


Kuvunjika kwake kumechelewa; kulipaswa kutokea tangu Kikao cha Butiama. Na labda ingevunjika hata kabla ya uchaguzi wa 2010. Ilichelewa kwa sababu bado hakukuwa na watu waliokuwa tayari kuimegua. Sasa hivi watu hao wapo, sababu zipo na inaonekana kuvunjika huku safari hii hakuepukiki - iwe kabla ya Uchaguzi au baada ya uchaguzi (itakapopoteza kiti cha Urais).

Ni vigumu kwa wote waliomo humo ndani kuweza kurithi yaliyomo ndani; wameshindwa kukaa kwa amani na sasa inaonekana wanaelekea kugongana. Wangeweza kuepusha mambo haya miaka kadhaa iliyopita ambapo wengine tulishauri mapema tu usalama wake ni kumeguka. Tofauti ambazo zimefunuliwa ndani ya chama hasa linapokuja suala la ufisadi ni kubwa mno kiasi kwamba ni vigumu kuona jinsi gani watu hawa wataweza kuwa wamoja kuelekea Uchaguzi Mkuu.

Na hili limesababishwa kwa kiasi kikubwa na udhaifu wa mifumo na taratibu za chama kushughulikia watu maarufu kiasi kwamba watu hao sasa wamepata nguvu kubwa kiasi cha kutishia uwepo wa chama na tishio hilo haliondoki kwa mikwara tena. Mikwara ingekuwa inaondoa watu basi "operesheni vua gamba" ingekuwa tosha kabisa. ILishindwa ile, zilishindwa hotuba za mikwara za mwenyekiti na hata maneno ya baadhi ya wana CCM yalishindwa kuwaondoa 'mafisadi'. Nina uhakika hata hili la "tuachieni chama chetu" litafeli. Wanaodai chama ni chao watajiuta hawana chao tena isipokuwa kuondoka.

Na kama watabakia itakuwa ni sababu tosha kwa Watanzania kufikiria kama kweli watu hawa wana ukweli ndani yao au yatakuwa yale yale ya ya kujikomba tena. Wataanza kutulisha maneno tena kuwa "hawakumaanisha yule" au "hawakumaanisha wale". Walimaanisha wengine wote isipokuwa "wale". Tusije kuona wale wale ambao wanasema "wale" ni mafisadi ndio hao hao wakawa wa kwanza kuimba "tuvunje makundi". Makundi CCM hayawajahi kuvunjwa yavunjwe leo kwanini?

Wakati mwingine utaona ni vizuri kwa CCM kuvunjika hata kupoteza Urais na kukaa pembeni ili labda akili zitawarudia. Na inaweza kuchukua muda kweli akili kuwarudia. KANU ya Kenya ilibidi akae pembeni na ikavunjika kweli lakini ilirudi kwa namna nyingine kabisa na kundi lililomeguka. CCM inabidi iende njia hiyo.

Ni kwa sababu hiyo naiombea sana wang'atane, waumane, wachubuane, na hata ikibidi wavunjane. Ili hatimaye wameguke na kutawanyika huku wakibebeshana lawama wakiwa nje ya madaraka.

Siombei wapatane hata kidogo. Maana wakipatana itakuwa shida nyingine ya miaka mitano. Sioni ni nani anayeweza kuwapatanisha sasa hivi maana walijaribu hata vikao vya mashauriano na madudu gani sijui walishindwa. Sasa wananchi wa kawaida wanafikiria watapatana kwa nini, ili kiwe nini, kwa nani na kwa nini?

Meguka!

MMM

Na ivunjike tu! by Mizengo Pinda.
 
Shida sio CCM kufa kabisa
CCM now ni kama 'dead man walking'
shida ipo kwenye replacement tukishaizika CCM
je wananchi wanaiona na kuiamin replacement?
we umeiiona?

Hoja ya ajabu kabisa hii!

Yaani huoni walio better kuliko huyo dead man anaye walk!

Hii inashangaza sana

Tusiwe na mawazo ya aina hii
 
Ndugu yangu Pasco yawezekana mapenzi yakatufanya tusione hali halisi.

Kwa maisha ya kawaida ni lazima U-wish au kutamani au Uote kuwa na nyumba au gari au chochote kile.Na ndoto hizi zawezekana zikaja baada ya kuona mwenye nyuma ana kunyanyasa ukawa unawish ungekuwa na nyumba yako na yawezekana matamanio yako yakakupeleka kule unakotamania yaani kuwa na NYUMBA.Yawezekana jirani anakutambia na miguu minne yake yaweza kuwa Prado au benzi basi ukatamani ungekuwa na japo vitz au Suzuki na wishes zako zikigeuka kuwa ndoto na ukaifanyia kazi nina uhakika matamanio yamo yakawa kweli ukapata vitz au suzuki.

Wishes za watanzania wengi au ndoto ya watanzania ni wengi ni kuondokana na Rusbwa na ufisadi uliokithiri unaowanyima watanzania haki zao za msingi hivyo wishes zao ni pamoja na CCM kuvunjika vipandenvipande tena siyo viwili bali zaidi ya viwili.

Ndoto za watanzania wengi ni kuiondoa madarakani huyu mwizi,mbadhirifu,mfugaji wa rushwa tena kubwa,tunatamani kwa njia yoyote ile kupata uhuru wa kuwaonod hawa na moja wapo ni hawa wajamaa kusambaratika kwa namna yoyote ile ila lazima wasambaratike.

Sababu tumeshajua mbinu zao inabidi kuanza kuzifanyia kazi na mojawapo ni kutafuta plan B maana hii A yaelekea kushindwa..UHURU WA KUJIANDIKISHA tumeshanyang'anywa na hapo ndipo tunatamani vyama vya upinzani kutafuta plan B.Na siyo wao tu hata sisi dreamers na wishers tuingie tusaidiane kutafuta plan B.

Tatizo kubwa mapenzi ya watu yametufunga macho kuliko mapanzi na uzalendo wa nchi yetu.Tatizo siyo Chadema wala UKAWA tatizo watanzania hatujui nini tunataka..
 
vyombo vya dola vitakapoiacha ccm ijiendeshe kisiasa kama chama cha siasa, hapo hapo kitavunjika. ktk hali ilikoifikisha tanzania ni bora na nafuu sana ccm ikivunjika na kutoweka kabisa. hata kwa usalama wa taifa hili ccm haifai tena. ni bora iondoke iwe historia na tz ianze upya. naamini kama taifa tutaendelea zaidi kuliko kuwa tena chini ya utawala wa ccm
Wengi wetu bado wanaamini kuwa kwa sababu ccm haijabadili logo yake kutoka jembe na nyundo, basi ni chama kile kile chenye kauli mbiu ya "DAIMA NITASEMA KWELI, FITINA KWANGU MWIKO" wakati sasa uongo na fitina ndizo nguzo kuu za chama!
R.I.P Mwalimu.

 
Kingunge leo kaongea maneno mazito na katoa angalizo juu ya mpasuko
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom