Mkereketwa_Huyu
JF-Expert Member
- Feb 19, 2011
- 9,248
- 6,378
Mhadhiri mwandamizi mstaafu wa chuo kikuu cha DSM Dr Azaveli Lwaitama amesema vitendo vya kinyama vinavyofanywa sasa na Jeshi la polisi dhidi ya CHADEMA vinaashiria kukaribia kuingia Ikulu kwa chama hicho.
Dr Lwaitama amelaani vitendo vya kinyama vilivyofanywa na polisi vya kupiga watu kikatili,kupiga risasi za moto na kupora mali za raia.
Dr Lwaitama kasema CCM sasa imeshindwa siasa za majukwaani na badala yake wameamua kutumia jeshi la polisi kujihami dhidi ya CHADEMA.
Dr Lwaitama amesema kiashirio tosha kwamba CCM sasa imefikia ukingoni ni matokeo ya uchaguzi wa udiwani wa kata 22 uliopita ambapo ingawa CCM ilipata viti 16 na Chadema 6 Lakini kura za Jumla zinaonyesha Chadema imeizidi CCM ambapo CCM imejikusanyia kura 17968 na CHADEMA kura 18431.Vyama vingine ikiwemo CUF vilipata Jumla ya kura chini ya 1000.
Dr Lwaitama amesema kama ingekuwa ni uchaguzi wa Urais basi CHADEMA ingekuwa imeshinda.Pia amesema haya yote yamefanyika huku maelfu ya vijana wafuasi wa Chadema wakiwa bado hawajaandikishwa kwenye daftari la kudumu la wapiga kura kwa hujuma ya CCM na ushirika wa Tume ya Uchaguzi.
Source:MAWIO UK 2
Mkuu, siku zote ukiona mtu ana act with paranoia basi juwa huyo siku zake za kusihi duniani zinayoyoma.