CCM Ijitenge na Cyprian Musiba

mafutamingi

JF-Expert Member
Feb 14, 2011
2,772
2,171
Hivi karibuni Cyprian Musiba amekuwa akitoa matamko mitandaoni akijinasibu kana kwamba anaongea kwa niaba ya CCM/Serikali. Ushauri wangu wa bure ni kwamba kama ni kweli basi CCM na serikali vinajidhalilisha kumtumia Musiba kwa namna navyotoa matamko yake. Ni bora wamkane na kumwonya asijihusishe na CCM wala serikali. Kama anataka kutoa matamko yake ayatoe kwa niaba yake na si kwa niaba ya CCM. Humphrey Pole Pole kazi kwako
 
Kumhimiza asiyetaka, ni sawa na kupikia kuni mbichi wakati wa masika, usipolia na kutoa kamasi. Wewe ni shujaa.
 
Huyu mtu ndiye hatari zaidi katika Taifa hili

Anatoa tuhuma nzito bila kuwa na ushahidi

Angethubutu kufanya hivyo kiongozi yeyote wa upinzani, hususani toka chama cha Chadema, hivi sasa angekuwa anaozea jela
 
Msiba ni kada wa chama, wakati ule mkulu anatoa speech bunge la east africa jamaa alitupita tunasubiri motorcade pale nje tusuuze macho akazama ndani na gari yake nyeusi geti zinafunguliwa fasta bila kuoji.

Jana tunatoka darasani tukapishana nae kaja kuuza sura chuo,tulicheka sana tulipomwona.

Nimejifunza kitu kupitia huyu kaka angu maisha ni rahisi sana ni sisi wenyewe huwa tunaamua kuwa ktk hali tulizonazo
 
Hivi karibuni Cyprian Musiba amekuwa akitoa matamko mitandaoni akijinasibu kana kwamba anaongea kwa niaba ya CCM/Serikali. Ushauri wangu wa bure ni kwamba kama ni kweli basi CCM na serikali vinajidhalilisha kumtumia Musiba kwa namna navyotoa matamko yake. Ni bora wamkane na kumwonya asijihusishe na CCM wala serikali. Kama anataka kutoa matamko yake ayatoe kwa niaba yake na si kwa niaba ya CCM. Humphrey Pole Pole kazi kwako
Bro kwani na ww ni CCM???

Kama ndiyo basi Kumbuka mna namna zenu za kuonyana na kurekebishana.. Huyo ni CCM MWENZAKO.. SIYO JF

kama ww siyo CCM Yanakuhusu nini ya CCM??? Maana kuparaganyika kwao ndilo ombi la kila mtu hasa Upinzani ili NCHI ipumue.. Kumbe saidia upande uliopo ili mfanikishe MALENGO yenu kupitia mgawanyiko wao

Sorry
 
Huyu mtu ndiye hatari zaidi katika Taifa hili

Anatoa tuhuma nzito bila kuwa na ushahidi

Angethubutu kufanya hivyo kiongozi yeyote wa upinzani, hususani toka chama cha Chadema, hivi sasa angekuwa anaozea jela
Angekuwa Kenya sasa hivi tungekuwa tumeshamaliza kuanua matanga!! Kenya hawapendagi ujinga!!
 
Ngoja mwenzie amalize kufanya tathmini ya zoezi la leo Kisha amkalie kwa kalio moja ili aweze kudeal nae papendicular!
Bila Shaka alishaanza kukusanya taarifa zake!
Labda aamue kumpotezea tu!
 
Back
Top Bottom