johnthebaptist
JF-Expert Member
- May 27, 2014
- 85,617
- 145,336
Akizungumza na wajumbe wa kamati za fedha, CAG mstaafu ndugu Uttoh amesema si sawa mawaziri kujibu hoja za ukaguzi wa CAG hadharani bali wawaache watendaji wafanyie kazi ripoti hiyo.
Uttoh amesema kama Waziri ana jambo lililomgusa anaweza kumuandikia CAG na si kuitisha vikao na waandishi wa habari, kwanza ripoti yenyewe bado haijafanyiwa kazi na bunge na kamati zake aliongeza Uttoh.
Chanzo: ITV habari!
Habari zaidi...
Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC), Naghenjwa Kaboyoka amekosoa utaratibu unaoendelea wa mawaziri walioguswa katika Ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kwa mwaka unaoishia Juni 30, 2016 kuwa si sahihi kujibu hoja zake nje ya Bunge.
Mara baada ya uwasilishaji wa ripoti hiyo wiki hii, mawaziri mbalimbali wakiwamo Dk Phillip Mpango wa Fedha na Mipango, Selemani Jafo (Tamisemi), Dk Harrison Mwakyembe (Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo) na Charles Mwijage wa Viwanda, Biashara na Uwezeshaji, walianza kujibu hoja hizo kupitia mikutano na wanahabari.
Hata hivyo, Dk Mpango juzi alieleza sababu za wao kutoa maelezo kupitia mikutano ya waandishi wa habari akisema kisheria hawabanwi licha ya kuwa kipindi cha nyuma hawakufanya hivyo.
Dk Mpango alisema kuwa majibu hayo ni kwa mujibu wa Sheria ya Ukaguzi wa Umma, kifungu cha 418 (38) (3) inayowapa mamlaka ya kujibu hoja hizo licha ya kuwa zamani walitumia njia hiyo lakini iliishia bungeni.
“Awali Serikali ilikuwa ikijibu kwa kuweka hoja zote bungeni, mwenzetu CAG alikuwa anawasilisha bungeni kisha anawaita waandishi wa habari na kuzungumza nao, sasa Serikali imeamua kufuata njia anazotumia ili kuwapa ukweli Watanzania, tutafanya hivyo kila wakati na mawaziri wote watakuja,” alisema Dk Mpango.
Alisema majibu ya kimyakimya ambayo yalikuwa yanatolewa na Serikali yameonekana kutokuwa na tija kwa kuwa wanapomuacha CAG kuwaambia Watanzania na waandishi kutumia zaidi ya mwezi wakichambua hoja hizo, Serikali inashindwa kupeleka ukweli hata kama upo.
Akizungumza jana baada ya semina iliyotolewa na Taasisi ya Uwajibikaji ya Wajibu kwa kamati tatu za Bunge za Hesabu za Serikali (PAC), Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) na ile ya Uwekezaji na Mitaji ya Umma (PIC), Kaboyoka alisema utaratibu huo wa Serikali kujibu ripoti ya CAG si sahihi na watakuwa na mkutano na waandishi wa habari kesho kuelezea kwa nini hawakubaliani nao.
“Nafikiri hili tulizungumzie Jumatatu, tutalitolea maelezo maana sio sahihi kabisa. Maana nani ame-verify (amethibitisha) ndio useme hivyo. Ile ripoti ni ya kibunge na ina taratibu zake za kupokewa na kufanyiwa kazi, kwa hiyo haiwezi kujibiwa tu hivihivi,” alisema.
Awali, CAG mstaafu, Ludovick Utouh alisema mafunzo waliyoyatoa kwa wajumbe wa kamati hizo yalilenga kuwajengea uwezo wajumbe wa kuhoji juu ya ripoti za CAG.
“Tunajua ili kamati hizi zifanye kazi zake za usimamizi ipasavyo kwa niaba ya Bunge, zina umuhimu wa kuelewa fika ripoti zenyewe na ni kitu gani kinazungumzwa,” alisema.
Aprili 11, CAG Profesa Mussa Assad aliwasilisha bungeni ripoti yake inayoonekana kuwagusa kwa karibu mawaziri watano baada ya wizara zao kutajwa katika taarifa hiyo ikionyesha upungufu katika baadhi ya maeneo, aliyosema yanajenga shaka.
Maeneo mengine yaliyoonyesha shaka katika taarifa hiyo ni Mfuko wa Hifadhi ya Jamii wa Taifa (NSSF), Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Mamlaka ya Bandari (TPA) na Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (Nida).
Profesa Assad alisema taasisi hizo zimetumia fedha nyingi kufanya ununuzi ambao hauna viambatanisho, hivyo kutia hofu kubwa
Chanzo: Mwananchi
Uttoh amesema kama Waziri ana jambo lililomgusa anaweza kumuandikia CAG na si kuitisha vikao na waandishi wa habari, kwanza ripoti yenyewe bado haijafanyiwa kazi na bunge na kamati zake aliongeza Uttoh.
Chanzo: ITV habari!
Habari zaidi...
Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC), Naghenjwa Kaboyoka amekosoa utaratibu unaoendelea wa mawaziri walioguswa katika Ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kwa mwaka unaoishia Juni 30, 2016 kuwa si sahihi kujibu hoja zake nje ya Bunge.
Mara baada ya uwasilishaji wa ripoti hiyo wiki hii, mawaziri mbalimbali wakiwamo Dk Phillip Mpango wa Fedha na Mipango, Selemani Jafo (Tamisemi), Dk Harrison Mwakyembe (Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo) na Charles Mwijage wa Viwanda, Biashara na Uwezeshaji, walianza kujibu hoja hizo kupitia mikutano na wanahabari.
Hata hivyo, Dk Mpango juzi alieleza sababu za wao kutoa maelezo kupitia mikutano ya waandishi wa habari akisema kisheria hawabanwi licha ya kuwa kipindi cha nyuma hawakufanya hivyo.
Dk Mpango alisema kuwa majibu hayo ni kwa mujibu wa Sheria ya Ukaguzi wa Umma, kifungu cha 418 (38) (3) inayowapa mamlaka ya kujibu hoja hizo licha ya kuwa zamani walitumia njia hiyo lakini iliishia bungeni.
“Awali Serikali ilikuwa ikijibu kwa kuweka hoja zote bungeni, mwenzetu CAG alikuwa anawasilisha bungeni kisha anawaita waandishi wa habari na kuzungumza nao, sasa Serikali imeamua kufuata njia anazotumia ili kuwapa ukweli Watanzania, tutafanya hivyo kila wakati na mawaziri wote watakuja,” alisema Dk Mpango.
Alisema majibu ya kimyakimya ambayo yalikuwa yanatolewa na Serikali yameonekana kutokuwa na tija kwa kuwa wanapomuacha CAG kuwaambia Watanzania na waandishi kutumia zaidi ya mwezi wakichambua hoja hizo, Serikali inashindwa kupeleka ukweli hata kama upo.
Akizungumza jana baada ya semina iliyotolewa na Taasisi ya Uwajibikaji ya Wajibu kwa kamati tatu za Bunge za Hesabu za Serikali (PAC), Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) na ile ya Uwekezaji na Mitaji ya Umma (PIC), Kaboyoka alisema utaratibu huo wa Serikali kujibu ripoti ya CAG si sahihi na watakuwa na mkutano na waandishi wa habari kesho kuelezea kwa nini hawakubaliani nao.
“Nafikiri hili tulizungumzie Jumatatu, tutalitolea maelezo maana sio sahihi kabisa. Maana nani ame-verify (amethibitisha) ndio useme hivyo. Ile ripoti ni ya kibunge na ina taratibu zake za kupokewa na kufanyiwa kazi, kwa hiyo haiwezi kujibiwa tu hivihivi,” alisema.
Awali, CAG mstaafu, Ludovick Utouh alisema mafunzo waliyoyatoa kwa wajumbe wa kamati hizo yalilenga kuwajengea uwezo wajumbe wa kuhoji juu ya ripoti za CAG.
“Tunajua ili kamati hizi zifanye kazi zake za usimamizi ipasavyo kwa niaba ya Bunge, zina umuhimu wa kuelewa fika ripoti zenyewe na ni kitu gani kinazungumzwa,” alisema.
Aprili 11, CAG Profesa Mussa Assad aliwasilisha bungeni ripoti yake inayoonekana kuwagusa kwa karibu mawaziri watano baada ya wizara zao kutajwa katika taarifa hiyo ikionyesha upungufu katika baadhi ya maeneo, aliyosema yanajenga shaka.
Maeneo mengine yaliyoonyesha shaka katika taarifa hiyo ni Mfuko wa Hifadhi ya Jamii wa Taifa (NSSF), Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Mamlaka ya Bandari (TPA) na Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (Nida).
Profesa Assad alisema taasisi hizo zimetumia fedha nyingi kufanya ununuzi ambao hauna viambatanisho, hivyo kutia hofu kubwa
Chanzo: Mwananchi