CAG anapotumia ofisi ya uma kwa kampuni zake binafsi!

bushman

JF-Expert Member
Nov 1, 2010
2,411
743
hakika ni kweli nipo na mfanyakazi wa ofisi,ya CAG ananiambia JAIRO ni mtandao wa LUHANJO na wanamakampuni hewa mengi,kwa mfano ananiambia CAG Ripoti ya UDOM alichakachua k'bu kampuni yake ilifanya kazi ile nimeumia sana,ofisi ya CAG inatumia mihuri ya serikali kufanya wizi,source ni mfanyakazi wa ofisi ya CAG!
 
Thread TITLE kuubwa halafu unaongelea majungu bila ushahidi, leta ushahidi hapa kama wafanyavyo wenzio!
 
hakika ni kweli nipo na mfanyakazi wa ofisi,ya CAG ananiambia JAIRO ni mtandao wa LUHANJO na wanamakampuni hewa mengi,kwa mfano ananiambia CAG Ripoti ya UDOM alichakachua k'bu kampuni yake ilifanya kazi ile nimeumia sana,ofisi ya CAG inatumia mihuri ya serikali kufanya wizi,source ni mfanyakazi wa ofisi ya CAG!

Mod futa thread hii, haya majungu. Huyo mfanyakazi amekwambia majina ya hayo makampuni. Umekwenda blera ukakuta kweli majina ni ya kwake?
 
Unafiki huu utatua sijawahi nchi inayotegemea siasa duniani ikafanikiwa
hakika ni kweli nipo na mfanyakazi wa ofisi,ya CAG ananiambia JAIRO ni mtandao wa LUHANJO na wanamakampuni hewa mengi,kwa mfano ananiambia CAG Ripoti ya UDOM alichakachua k'bu kampuni yake ilifanya kazi ile nimeumia sana,ofisi ya CAG inatumia mihuri ya serikali kufanya wizi,source ni mfanyakazi wa ofisi ya CAG!
 
mleta mada lazima hajui kujieleza na ni natural mlalamaji...

panga hoja tena
 
hakika ni kweli nipo na mfanyakazi wa ofisi,ya CAG ananiambia JAIRO ni mtandao wa LUHANJO na wanamakampuni hewa mengi,kwa mfano ananiambia CAG Ripoti ya UDOM alichakachua k'bu kampuni yake ilifanya kazi ile nimeumia sana,ofisi ya CAG inatumia mihuri ya serikali kufanya wizi,source ni mfanyakazi wa ofisi ya CAG!

Nenda kwanza kapitie sheria ilioanzisha ofisi,majukumu na mipaka ya CAG
 
Sifikirii kama huu ni unafiki au umbeya. Aliyeleta mada nafahamu ana data lakini mkianza kumshambulia mwanzo mwanzo hivi hata hizo data hamuwezi kupata, either nyie mpo katika kufaidi na kuitetea CAG au mmetumwa au upeo wenu ni mdogo.

Mkuu
bushman weka nondo hapa wala usiwe na shaka, uozo unaoendekezwa na JK pamoja na serikali yake ya CCM hauwezi kuvumiliwa ni lazima kila kona kufanyike kazi ya kuliondoa taifa hili katika mikono ya mafisadi yaliyokubuhu.
 
Wengi mngekuwa mnajua jinsi CAG anavyofanya kazi na maadili yake kamwe msinge mlaumu huyu wa sasa. Nimeshangaa hata kamati ya bunge imemnyooshea kidole. Kama alipewa terms of reference na luhanjo unategemea nini? Anafanya kazi based on hiyo TOR na anareport back kwa aliyempa kazi ambaye ni luhanjo. Kama ukitafakari utagundua CAG hana shida.
 
CAG naye ni binadamu,anaweza kupotoka na kutenda makosa kama tulivyo sisi, hivyo basi tusiondoe uwezekano wa yeye kutumiwa na baadhi ya watu, kwa maslahi binafsi kwani hili pia linawezekana. Kuitwa Mkaguzi mkuu sio tija, naye pia anaweza kupindisha baadhi ya mambo, kwa ajili ya tumbo lake kama wafanyavyo baadhi ya watendaji wa Serikali wasio waadilifu. Tumpe nafasi ndugu yetu atoe vielelezo zaidi,yawezekana anayo mengi ya kutueleza kwenye hoja yake ya msingi,tuheshimu mawazo yake
 
No evidence amekuja kutaka info zaid kuhusu hisia zake dhidi ya ikulu.
 
Ndugu wana jamvi, kwa taarifa nilizozipata toka kwa wafanyakazi wa chuo kikuu cha Dodoma, wamefurahia sana namna ambavyo CAG na Katibu kiongozi walivyoumbuliwa na kamati teule ya bunge.
Furaha hii ya wanaudom inadaiwa ni kutokana na kuthibitishwa kwa hisia zao kuwa ukaguzi uliofanywa na CAG hapo UDOM katika kipindi cha mgomo wa wahadhiri ulilenga kuficha ukweli ndio maana CAG alitanganza kutoona ubadhirifu wowote.

Mambo yanayosababisha wanajumuiya hiyo wakose imani na CAG pamoja na Katibu kiongozi ni kutolewa kwa salary slip mbili tofauti kwa mtumishi mmoja na zote zina mishahara miwili tofauti hii kwa baadhi ya watumishi limefanyika kwa zaidi ya miaka miwili na ushahidi upo kabisa wa salary slip hizi.

Salary slip moja ni ya kutoka hazina ambayo inamshahara sahihi(mkubwa) na nyingine ni ya Udom yenye mshahara wanaojua wao(sio sahihi). katika hili pia wanajumuiya walijiuliza je uongozi wa chuo ulitumia utaratibu gani kubadilisha mishahara ya watumishi kwani hata watu wa hazina walipohojiwa juu ya hili walionekana kushangaa na kuonekana kuutambua mshahara unaotoka hazina pasipo mashaka yeyote, lakini huyu CAG hakuona tatizo lolote.

Matokeo ya kuwepo kwa salary slip mbili kumewafanya wafanyakazi wa chuo kikuu cha Dodoma kulipwa kwa kiwango cha chini tofauti na vyuo vingine vya umma. Ushahidi upo wazi, kwani mhadhiri msaidizi wa Udom(anayeanza bila kujali uzoefu PUTS 13) analipwa sawa na mkufunzi msaidizi wa chuo kingine cha uma(tutorial assistant) -angalia OUT AU UDSM

Jambo jingine linalojitokeza katika kuwepo kwa salary slip mbili ni je baada ya kuwa kata mshahara hawa wafanyakazi wa udom hicho kinachokatwa kinaenda wapi wapi?

Katika mateso yanayowakabili wafanyakazi wa UDOM imebainika kuwa katibu mkuu kiongozi ana mkono wake. Hili linadaiwa ni kutokana na mahusiano yake na makamu mkuu wa chuo ndugu Kikula hawa wote wanatokea sehemu moja huko Iringa(ukanda na ukabila). Kutokana na mahusiano haya ya karibu inadaiwa kuwa katibu mkuu kiongozi alitoa maelekezo ambayo si sahihi ya namna ambavyo ukaguzi wa kubaini ubadhirifu udom ufanyike. Matokeo yake ni kutoa mwanya wa ofisi ya fedha na utawala ya ndg Mlacha kuonekana kuwa ni safi. Kwani inadhaniwa kwamba isingekuwa rahisi kwa mlacha kuwa mchafu na kikula kawa msafi tumia mfano wa jairo na ngeleja.

Katika kutangazwa kuwa hakuna kosa lolote Pinda alionekana pia kudharirishwa(huenda ya bungeni kuhusu jairo ni ya pili) kwani alipokuja kutatua mgogoro wa wahadhiri aliwahakikishia wanajumuiya kuwa suala la Mlacha ni suala la muda. Kutokana na hali hii tunaona kwamba tabia ya katibu kiongozi kulinda au kujihusisha na ufisadi ni suala ambalo amebobea na matokeo yake ni kuidhalilisha serikali hii ya ccm.

Katika nsakata la udom, Huenda kutokana na madudu ya CAG na katibu kiongozi(mtazamo wangu) imesababisha kuleta hisia kwamba huenda mheshimiwa raisi anajikuta analinda mafisadi kwa kigezo cha udini( hoja iliyatawala kipindi fulani miongoni mwa wanajumuiya kwamba Mlacha anaandamwa kwa sababu ya dini yake), Kutokana na kazi nzuri ya kamati teule hata kwa baadhi ya waislamu wameanza kuona namna ambavyo dini yao nzuri inavyotumika kama kichaka cha kufichia mafisadi na watendaji wenye kiburi cha ajabu.

Hivyo basi wanajumuiya ya UDOM wananaiomba kamati ya bunge ya hesabu za mashirika ya umma kuipitia vema ripoti ya CAG ili kubaini ufusadi wake. CAG na Luhanjo dhambi ya UDOM imewaumbua! Ninawasilisha
 
Wengi mngekuwa mnajua jinsi CAG anavyofanya kazi na maadili yake kamwe msinge mlaumu huyu wa sasa. Nimeshangaa hata kamati ya bunge imemnyooshea kidole. Kama alipewa terms of reference na luhanjo unategemea nini? Anafanya kazi based on hiyo TOR na anareport back kwa aliyempa kazi ambaye ni luhanjo. Kama ukitafakari utagundua CAG hana shida.

Mkuu kama umesikiliza ripoti ya kamati utagundua kuwa alipewa TOR mbili tu ambazo ni nzuri nazo ni:-

1. Uhalali wa Jairo kukusanya pesa hizo?
2. Matumizi ya pesa hizo?

Hizo adidu za rejea mbili zilitakiwa zimfanye Jairo anase kwenye nyavu za CAG, na kitendo cha CAG kugundua yafuatatayo na kuayafumbia macho ni makosa:-
a. Matuzimizi mabaya ya hela zilizokusanywa
b. Uharamu wa Jairo kukusanya hela zile

Ikumbukwe conclusion ya CS ili-base kwenye riport ya CAG naye akiwepo anakubali umma udanganywe. Huyo amepoteza credibility yake ni sawa na tuliyoyaona kwa TAKUKURU wakati wa riport ya Richmond. Ni watanzania wachache mpaka leo wataamini riport itakayotolewa na Takukuru endapo itakuwa inamuhusu kigogo!

Hata mimi ni miongoni mwa watanzania waliokuwa dissappointed na CAG!

 
hakika ni kweli nipo na mfanyakazi wa ofisi,ya CAG ananiambia JAIRO ni mtandao wa LUHANJO na wanamakampuni hewa mengi,kwa mfano ananiambia CAG Ripoti ya UDOM alichakachua k'bu kampuni yake ilifanya kazi ile nimeumia sana,ofisi ya CAG inatumia mihuri yao serikali kufanya wizi,source ni mfanyakazi wa ofisi ya CAG!
Japo thread yako imekaa kiudakudaku, naona kwa umbali kuna uwezekano huo. Hii nchi bwana kila mtu ana kipande cha mkate wa taifa anakula taratibu. Kama ni ukombozi, tunahitaji maombi mazito sana Mwenyezi Mungu atuwezeshe.
 
Hii ni chanel ndefu mno,ila kuimaliza chanel hii ni kuipiga chini system yooooote vinginevyo wataendelea kulindana hivi kila siku huku tunaumia
 
Back
Top Bottom