sammosses
JF-Expert Member
- Jan 24, 2011
- 1,682
- 1,110
No longer at ease,hayumkini si shwari tena!na kimya kingi kina mshindo mkuu.Ziara za wamarekani hawa ndani ya nchi yetu zina tija kwetu?Hofu yangu isije kuwa tunauza mgodi mwingine kwa chandarua zingine ilihali nchi yetu ikiwa ni muathirika mkubwa wa ugonjwa wa malaria.Uchumi wetu leo unashikiliwa na Mmarekani(madini na nishati ya umeme).Tuna experience na ujio wa wakubwa hawa ndani ya nchi yetu.Tumeona kila ujio wao unakuja na mshindo mkuu ndo maana tunajiuliza kunani Tanzania?Tuna kumbuka ujio wa mama Hilari Clinton,alikaa kwa muda wa siku si chini ya tatu na matokeo yake ni kununuliwa mitambo ya Dowans na kusainishwa kwa mkataba wa kuzalisha umeme kwa kampuni ya kimarekani(Symbion).Lazima ifike wakati tujiulize urafiki huu una tija kwa maendeleo ya taifa au ni kwa wateule wachache waliopewa dhamana ya kuwatumikia wananchi ?
Kuna sababu gani ya rais wa nchi kwenda kumpokea mgeni asiye wa Kitaifa,wakati kuna mawaziri husika?Je ni lini wafanyabiashara wetu waliwahi kufanya ziara nchi Marekani na kupokelewa na ujmbe mzito toka serikali kuu?udhaifu unaotumiwa na wageni hawa ipo siku utakuja kuligharimu taifa letu.Na kama ni suala la utalii wapo wahusika wakuu katika wizara husika wangeweza kufanya kazi hiyo na kumuacha rais akishughulikia majukumu mazito ya kitaifa.Ni jambo la kustajaabisha sana kodi za walalahoi zinatumika kuwakarimu wageni wasio wa kiserikali.Tunaomba serikali itueleze ujio huu wa kimya kimya una tija gani katika maendeleo ya taifa hili,au ndo kaleta kibaba kutokana na safari za mh. rais kwenda kuhemea ?
Kuna tetesi kuwa African Barrick Gold mine wapo katika mchakato wa kuhakikisha mgodi wa Resolute unaingia ndani ya mikono yao,na kama ndo hivyo waweke mambo hadharani kuliko kunyamaza kimya wakati rasilimali zetu zinatoweka kwa mlango wa nyuma.Unafiki huu wa viongozi wetu utaisha lini,kwanini wasiige mfano wa Mugabe!?Naomba kuawakilisha mniongoze kujua ugeni huu wa kimya kimya una tija kwa taifa letu?
Kuna sababu gani ya rais wa nchi kwenda kumpokea mgeni asiye wa Kitaifa,wakati kuna mawaziri husika?Je ni lini wafanyabiashara wetu waliwahi kufanya ziara nchi Marekani na kupokelewa na ujmbe mzito toka serikali kuu?udhaifu unaotumiwa na wageni hawa ipo siku utakuja kuligharimu taifa letu.Na kama ni suala la utalii wapo wahusika wakuu katika wizara husika wangeweza kufanya kazi hiyo na kumuacha rais akishughulikia majukumu mazito ya kitaifa.Ni jambo la kustajaabisha sana kodi za walalahoi zinatumika kuwakarimu wageni wasio wa kiserikali.Tunaomba serikali itueleze ujio huu wa kimya kimya una tija gani katika maendeleo ya taifa hili,au ndo kaleta kibaba kutokana na safari za mh. rais kwenda kuhemea ?
Kuna tetesi kuwa African Barrick Gold mine wapo katika mchakato wa kuhakikisha mgodi wa Resolute unaingia ndani ya mikono yao,na kama ndo hivyo waweke mambo hadharani kuliko kunyamaza kimya wakati rasilimali zetu zinatoweka kwa mlango wa nyuma.Unafiki huu wa viongozi wetu utaisha lini,kwanini wasiige mfano wa Mugabe!?Naomba kuawakilisha mniongoze kujua ugeni huu wa kimya kimya una tija kwa taifa letu?