Bunge letu si bunge tukufu

Mi nilishaacha kuwaita hawa jamaa "waheshimiwa" na hicho kijiwe chao "kitukufu" kuanzia nilipobaini wezi na vibaka kama kina Mramba wakitokea Mahakamani na rumande kwenda kuhudhuria vikao "vitukufu" baadae nilipata kichefuchefu cha kumwita yeyote mheshimiwa au mtukufu nilipoona hata vibaka kama kina Chenge, EL, na wengine kibao wamo! Nasikia hata yule aliyekamatwa na rushwa red handed na kesi yake iko mahakamani bado anaitwa "mheshimiwa"! Hivi watanzania tuna akili kweli? Napata kigugumizi hata kumwita mkuu wa kaya Mheshimiwa baada ya wazungu anaowahusudu kuanika madudu yake ya kuhongwa hata nguo! Majuzi ndiyo kabisaa... karibu nizimie; eti Spika amevunja kamati iliyohusika na rushwa na kuunda nyingine huku hao jamaa wakiendelea kuitwa "Waheshimiwa"! Hivi kwa nini tusiweke katika katiba yetu mpya kwamba watu wa aina hii wasimamishwe nafasi zao za ubunge na wakithibitishwa kutenda walivyotenda - inyume cha kiapo na kuaminiwa kwao wafungwe maisha (Maana wajimba wamesema tusinyonge mtu!)? Kwa kifupi Tanzania ni nc hi ambayo huna wa kumwamini, kuanzia Rais, Polisi hadi Tarishi; kaa chonjo na "Kila abiria achunge mzigo wake". Tuitane Ndugu tu lakini hili la waheshimiwa na watukufu wezi, majambazi, vibaka na malaya kuwaita "waheshimiwa na watukufu" hapana tusubiri kidogo.
 
Bunge lenye wabunge webgi walioingia kwa kutoa rushwa kwenye vikao vya chama ili wapitishwe na kuwahonga wananchi ili wapigiwe kura haliwezi kupata uhalali wa kupambana na rushwa na ufisadi.
 
Maneno yako ni ya kweli kabisa mkuu, wala hayana ubishi hata kidogo Utukufu wa Bunge letu huko wapi????????????????????// kama watanzania wanalala na njaa,wanapata shida mbalimbali hazisikilizwi, Bunge linashindwa kuishuri serikali yake juu ya maisha ya watanzania yalivyo magumu kazi yao kugonga meza tu na kuunga mkono asilimia 100% kisha kulalama utukufu uko wapi? na kwanini tuko katika hali hiyo ni kwa sababu ya hawa Mafisadiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii.
 
Rais kapoteza utukufu na sasa amekuwa Rais fisadi. Tukumbuke msani aliingia madarakani kupitia mgomgo wa mafisadi ambao wenyewe waliijita wana mtandao. Hawa walipita huku na kule kuchangisha mabilioni ya pesa toka kwa mafisadi mbali mbali wakiwemo akina Manji, Subhash Patel, Jeetu n.k. ili kuwahonga wajumbe wa mkutano mkuu kupitisha jina la msanii kama mgombea wa CCM.

Asilimia kubwa ya Wabunge wa magamba wameingia mjengono kwa kutoa hongo kwa wapiga kura au kubebwa na tume ya uchaguzi ya magamba baada ya kuchakachua kura katika majimbo mengi.

Bunge limeoza na halistahili tena kuwa wawakilishi wa Watanzania maana yanayoendelea ndani ya Bunge hili haramu kwa kweli yanasikitisha na kushangaza sana lakini hakuna wa kuyakemea. Si Rais wa nchi, Waziri Mkuu au Spika wa Bunge wote wameamua kuangalia pembeni huku vituko ndani ya Bunge hili haramu (ikiwemo matusi, kejeli zinazofanywa na Wabunge mbali mbali dhidi ya Wabunge wa CHADEMA ikiwemo Spika na Naibu wake, uombaji na upokeaji wa rushwa ili kupitisha bajeti za wizara mbali mbali) vikiendelea kushamiri kila kukicha

Kuna kila sababu katika hii katiba mpya ambayo inategemewa kuanza kutumika 2015 Wabunge nao waruhusiwe kuwa mjengoni kwa awamu mbili tu badala ya kuachiwa kuendelea kuwa Wabunge kwa zaidi ya vipindi viwili vya miaka mitano mitano.

Bunge halina utukufu wowote, ufisadi mtupu. Na asilimia kubwa ya hao fisadi ni wabunge wenyewe ambao wanajenga bunge.
 
Namlaani Mwigulu na CCM yake

Salehe Mohamed
Tanzania Daima

LEO nimeamua kukilaani Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Naibu Katibu Mkuu wa chama hicho (Bara), Mwigulu Nchemba, kwa kulinajisi Bunge la bajeti ya mwaka 2013/2014.

Nasema Nchemba na CCM wameamua kulinajisi Bunge, wameamua kutumia muda mwingi kupambana na CHADEMA badala ya kuwapa fursa wananchi wajue bajeti za wizara mbalimbali zitawanufaishaje.

Hawa wameamua kutumia muda wa Bunge kuzungumzia masuala ya ugaidi ambayo nyumbani kwake ni mahakamani na polisi. Wameamua kuwageuza mwelekeo wabunge na wananchi.

Nchemba ameutangazia umma kuwa CHADEMA ni chama cha kigaidi, anao ushahidi wa mikanda ya video juu ya maandalizi ya kigaidi yanayofanywa na chama hicho, huyu atakuwa msaada mkubwa zaidi kwa polisi.

Natarajia polisi watakuwa wamemsikia Nchemba. Si kumsikia tu bali watafanyia kazi kile alichokizungumza, Msajili wa Vyama vya Siasa naye atakuwa amemsikia kiongozi huyo.

Naamini intelijensia ya polisi itafanya kazi vizuri zaidi kama inavyofanya ikisikia CHADEMA inaandaa maandamano na mikutano ya hadhara ambayo huizuia kwa madai ya kupata taarifa kuwa inaweza kusababisha uvunjifu wa amani.

Nchemba na makada wa CCM hawataki Watanzania wapate muda mrefu wa kutafakari kwa kina bajeti za wizara husika, wanataka porojo na itikadi za kisiasa zichukue nafasi ili kuipa ahueni serikali.

Wanakosea wanafikiri wingi wao bungeni ndio unawapa fursa ya kuamua wanalolitaka, hawajifunzi kwa kile kilichowapata katika uchaguzi wa mwaka 2010.

Nchemba na makada wa CCM wanafikiri njia sahihi ya kupambana na wapinzani ni kutumia Mahakama, Bunge, Polisi, Usalama wa Taifa na vyombo vingine vya dola.

Wamelewa madaraka, wanadhani adui yao mkubwa ni vyama vya upinzani. Adui mkubwa wa CCM ni mwananchi aliyeahidiwa maisha bora miaka saba iliyopita na serikali yao.

Wananchi wana chuki na hasira dhidi ya chama tawala kilichowaahidi neema ambayo sasa hawaioni isipokuwa njaa na mateso ya kila aina.

Wanashuhudia gharama za mafuta, sukari, mahindi, mchele na nyinginezo zikipanda maradufu kuliko ilivyokuwa miaka saba iliyopita kabla ya utawala wa Awamu ya Nne kuingia madarakani.

Kamwe vyama vya upinzani si adui wa wananchi, ndiyo maana wanaposikia kuna maandamano na mikutano ya hadhara ya vyama hivyo hujitokeza kwa wingi kiasi cha kuwatisha watawala.

Watawala ndio wenye hofu dhidi ya wapinzani kwa sababu wanajua wataanikwa udhaifu wao, hawataki wananchi waelewe wala kuhoji rasilimali lukuki za taifa zinavyotumika. Wanataka wananchi wabakie kwenye ujinga ili wawatawale kirahisi.

Wabunge wetu kiukweli hawatutendei haki wananchi, hatujawapeleka bungeni waoneshane ufundi wa vijembe, matusi na kejeli. Tumewapeleka bungeni waisimamie serikali katika utekelezaji wa majukumu yake.

Wakiisimamia vizuri serikali, huu ufisadi, matumizi mabaya ya madaraka na misamaha ya kodi inayolalamikiwa kila mara vitakoma na wananchi tutapata maisha bora tuliyoahidiwa miaka saba iliyopita.

Wabunge wetu wana muda mwingi zaidi wa kufanya siasa kabla vikao vya Bunge havijaanza. Wafanye mikutano ya hadhara kadiri watakavyo juu ya ubaya au uzuri wa serikali, wananchi watawapima huko.

Ningependa wawapo bungeni wajikite zaidi kuboresha bajeti za wizara husika kuliko kuambiwa fulani ana ushahidi juu ya ugaidi. Ushahidi huo si ungepelekwa polisi na mahakamani?

Nchemba na wenzake wanaweza kujiona wajanja hivi sasa kwa kuwadhibiti CHADEMA lakini watambue fika matunda ya hicho wanachokifanya hivi sasa yataonekana mwaka 2015 kwenye uchaguzi mkuu.

Nawalaani wabunge wote ambao watautumia muda mwingi kujadili itikadi za kisiasa na minyukano badala ya kujikita kwenye majadiliano ya bajeti za wizara husika.

Watanzania wengi hatuutaki umaskini, hatupendi rasilimali zetu zinawanufaishe wachache au wageni waliopewa jina la wawekezaji. Tunataka wabunge wawe mstari wa mbele kuandaa mazingira ya serikali kutozitumia rasilimali tulizonazo kwa manufaa ya wengi.

Kuporomoka kwa elimu, huduma hafifu za afya, maji, barabara na nyinginezo haziwezi kuboreka kama wabunge wa CCM watautumia wingi wao kulinda masilahi ya serikali yao hata pale inaposhindwa kutekeleza majukumu yake.

Inawezekana wabunge wanaona wanafanya ni siasa njema bungeni lakini huku kwenye jamii inasikitisha kulipa watu kufanya kazi ya aina hii. Hili ni tatizo letu sisi raia: hatuko makini na tunachotaka kutoka kwa viongozi wetu.

Udhaifu huu ndio unaolitafuna taifa. Hawa ni wachache sana kuamua hatima yetu kwa mtindo huu.

Wananchi tunatakiwa kukataa ujinga na porojo zinazofanywa na wabunge wenye malengo la kulinda vyama vyao ndani ya Bunge letu tukufu, tusipofanya hivyo kila kukicha tutabaki tukilalamikia ugumu wa maisha.

Ugumu huu wa maisha umechangiwa kwa kiasi kikubwa kuchagua viongozi aina ya Mwigulu Nchemba, hawa hawawezi kukisaidia chama tawala kutimiza majukumu yake kwa wananchi. Hawa kila kukicha wanawaza kupambana na upinzani.

Kwao upinzani ni uadui, wanataka wapinzani wasiwepo ili madhambi na udhaifu wa utawala wao usifichuliwe. Zama za sasa ni vigumu zaidi
kuishi maisha wanayotaka wao, hiki ni kizazi cha kuhoji kila kitu.



 
Ninaamini ccm wamepitwa na wakati propaganda za miaka ya sabini inaletwa leo?kweli if u don't change u shall be the victim of change

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
Ndugu zangu jf natumai sote wazima nimekuja humu leo ku share mawazo nanyi.Leo nilikua na tazama BUNGE Nikamsikia mh moja akasema"Kuna WaBunge humu ndani mnapata mimba zisizo tarajiwa mbona hatusemi au mnataka tuwataje?Itafikia siku tutawataja hadharani" Sasa nikakajiuliza hivi who's worked? Kaama kweli Mbunge hajitambui kiasi hicho mpaka anapata mimba isiyo tarajiwa afu ndo muakilishi wangu?Au Mbunge ambae anadiriki kumvua nguo mbunge mwenzie(wanawake)kwa kauli hiyo?mimi binafsi bado natafakari hii kauli kama ni kweli we are DEAD
 
An abusive statement and ofcourse not to be spoken in the respected place particularly in the parliament,who said so kwanza?a mad man or womam?
 
Tangu kuanza kwa phase II ya rais Kikwete na kwa mara ya kwanza Bunge letu kuongozwa na mwanamke tumeshuhudia vimbwanga vya kutosha. Sielewi tafsiri ya wanaccm kuhusu mwenendo wa bunge hili. Nachelea isije ikawa wanajidanganya kuwa umma utaendelea kuwalaumu wapinzani. Ukweli ni kwamba wananchi tuko makini kubaini chanzo cha tatizo. Tatizo ni Spika mama yetu Anna Makinda. Tunatamani ngwe ifike mwisho kuepusha upuuzi unaoeedelea usitue masikioni mwetu. Hata hivyo, tunashukuru maana kila inapotokea upuuzi unafanyika tunahamasika zaidi kuchagua chama kingine.
 
Unachokisema ni kweli tupu, kiti cha spika kimepwaya sana katika awamu hii ya Makinda na kila mtu anaona. Leo nilipita mahali fulani nikakuta kama watu 12 wanaangalia Bunge hasira waliyokuwa nayo kama spika angekatiza hapo wangemgawana. Anna Makinda anaongeza idadi ya wapinzani wa Ccm watake wasitake wanayakoroga wenyewe!
 
Tangu kuanza kwa phase II ya rais Kikwete na kwa mara ya kwanza Bunge letu kuongozwa na mwanamke tumeshuhudia vimbwanga vya kutosha. Sielewi tafsiri ya wanaccm kuhusu mwenendo wa bunge hili. Nachelea isije ikawa wanajidanganya kuwa umma utaendelea kuwalaumu wapinzani. Ukweli ni kwamba wananchi tuko makini kubaini chanzo cha tatizo. Tatizo ni Spika mama yetu Anna Makinda. Tunatamani ngwe ifike mwisho kuepusha upuuzi unaoeedelea usitue masikioni mwetu. Hata hivyo, tunashukuru maana kila inapotokea upuuzi unafanyika tunahamasika zaidi kuchagua chama kingine.

Sijaelewa uanamke wa Spika umekuwa vipi kigezo cha utendaji. Kauli yako hii inaweza kutafsiriwa kwamba unaitahadharisha jamii ili isiruhusu mwanamke mwingine awe Spika au nafasi ya juu ya uongozi, jambo ambalo linawatia kitanzini mabinti wote hata waliozaliwa leo bila kuwa na hatia.

Kuna haja ya kuwa makini na jinsi tunavyotoa hoja.
 
Tangu kuanza kwa phase II ya rais Kikwete na kwa mara ya kwanza Bunge letu kuongozwa na mwanamke tumeshuhudia vimbwanga vya kutosha. Sielewi tafsiri ya wanaccm kuhusu mwenendo wa bunge hili. Nachelea isije ikawa wanajidanganya kuwa umma utaendelea kuwalaumu wapinzani. Ukweli ni kwamba wananchi tuko makini kubaini chanzo cha tatizo. Tatizo ni Spika mama yetu Anna Makinda. Tunatamani ngwe ifike mwisho kuepusha upuuzi unaoeedelea usitue masikioni mwetu. Hata hivyo, tunashukuru maana kila inapotokea upuuzi unafanyika tunahamasika zaidi kuchagua chama kingine.



Huyu mama ni moja tu ya sababu ya upuuzi wa bunge letu. Wabunge wetu wengi ni wasanii tu, huwezi kuniambia umalaya wa wabunge wetu unachangiwa na huyu mama spika. Kusinzia na kujambajamba hovyo bungeni ni hulka ya wabunge wetu, mtu anakwenda bungeni badala ya kuchangia hoja yeye anaona bora alale ili aote ndoto akihamka anaitikia ndiyo kwa kitu asichokijuwa, hii si sababu ya huyu Mama spika ni wabunge wenyewe kwani spika hawezi kuwalazimisha wasilale wale siyo watoto.
 
[h=3][/h]

Chanzo cha umaskini wa wananchi husika husababishwa na bunge bovu na legelege ambalo kimsingi haliwezi kusimamia serikali.


Kwa sasa bunge letu limekuwa comedy show bila kujali pesa za walipa kodi wanazozitafuna kila siku.


Tangu bunge lianze mheshimiwa spika kwa makusudi amekuwa akiruhusu mijadala isiyokuwa na tija bungeni na wabunge wamekuwa wakitukanana matusi ya nguoni

Wakati leo nasikiliza bunge, Mheshimiwa mmoja alisimama tena kwa kujiamini na kudai kuwa eti umasikini wa tanzania unasababishwa na picha ya nyoka iliyoko katika pesa zetu....



"Tanzania ni nchi masikini kwasababu tumeweka picha ya nyoka kwenye hela zetu".... ni kauli ya Mh Livingstone Lusinde Mbunge wa Mtera leo bungeni.

Kauli aliyoitoa Mheshimiwa Bungeni leo haiingii akilini hata kidogo. Labda pengine kwa sababu ya upeo wangu mdogo wa kuelewa na kufikiri .....


Ni vigumu sana kuwashawishi wananchi na jumuia za kimataifa kuwa umasikini na matatizo yote yanayoikabili shillingi ya Tanzania yanasababishwa na picha za nyoka...


Baadhi ya COMEDY toka bungeni:

-Kianzishwe chuo cha kufundisha wanaume namna ya kuwafundisha namna ya kutongoza wanawake - Mbunge viti maalum Chadema!

-Tanzania ni nchi masikini kwasababu tumeweka picha ya nyoka kwenye hela zetu".. hii ni kauli ya Mh Livingstone Lusinde Mbunge wa Mtera

-Ofisi ya Waziri Mkuu, imeomba Shilingi bilioni moja kwa ajili ya kuwazika viongozi wa kitaifa watakaokufa katika mwaka wa fedha unaoanza Juni, mwaka huu.



-Bangi ihalalishwe na kua zao la Taifa!. AIBU: BUNGE LETU LIMEGEUZWA UWANJA WA "COMEDY SHOW" - MPEKUZI HURU





 
Jamani mie sielewei hivi kinachoendelea bungeni ni demokrasia au upuuzi?? hivi kweli tuliowachagua kwa kukaa mistarini tangu asubuhi mpaka jioni na njaa zetu hiki ndicho tulichowatuma wakafanye bungeni???Tofauti ya bunge na soko la karume/kariakoo shimoni ni ipi?? sokoni matusi kawaida na bungeni nako cku hizi kawaida.... nawaambiaje wabunge wahivi anzeni kuandaa CV zenu maana 2015 cyo mbali.. hatuwezi kuwakilishwa na watu ambao badala yakujadili mambo ya msingi wao nikutukanana tuu huko...
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Naogopa sana kutumia neno "Utukufu" Bunge letu siyo Tukufu kwasababu kwanza kwasababu zifuatazo:-
1. Wabunge hawalipi KODI.
2. Huko Dodoma wamejaa makahaba kwa ajili ya hao hao, utakatifu uko wapi.
3. Wanajipendelea sana kwa maslahi kuliko wananchi waliowachagua, mimi nikinung'unika maana yake natuma dhuluma hizi kwa Mungu, na Mungu hawezi kumpa utukufu mbunge wa namna hiyo.
4. Lugha ya huko Bungeni siyo hoja tena bali matusi utakatifu hapo uko wapi?
5. Wanapitisha hoja ambazo fika wanajua zinadhulumu maslahi ya wananchi badala ya kubeba UTAIFA wanabeba bendera zao, utakatifu uko wapi hapo. Yapo mengi mno muda unanibana kuyaweka hapa. Kifupi Bunge Letu Lipo kama KIJIWE CHA MAZUNGUMZO YA KAHAWA
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Ni kwa muda mrefu sasa tumeshuhudia bunge letu likitawaliwa na uzalendo wa vyama zaidi kuliko kutekeleza yale wananchi waliyowatuma.mfano badala ya wabunge kujikita ktka kuchangia hotuba ya waziri mkuu badala yake muda mwingi umekuwa ukitumika kupigana vijembe ,kejeli na matusi.haya mambo yanatakiwa yafanyike kwenye majuukwa na siyo ndani ya bunge.Bunge ni sehemu ambayo bunge linapaswa kusimamia serikali.kuweka uzalendo mbele.Wananchi wanakabiliwa na matatizo lukuki kama vile ukosefu wa maji,huduma za afya,elimu duni,umasikini. hayo ndo mambo muda wote wabunge walipaswa kuyapigania kwanza.TAIFA HILI HALITAWEZA KUENDELEA MILELE KAMA bunge litaendelea kuwa namna hii
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Hatuwezi katu kuwa na Bunge tukufu wakati majority ya waliomo humo ndo vinara wa maovu kwenye jamii. Ikitokea wabunge wengi wakatoka kwenye vyama vinavyokemea ufisadi na uozo mwingineo bunge hilo litabadilika na kuwa na hadhi ya mabunge ya nchi nyingine.
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Duh!! Mpaka matusi ya nguoni ndani ya Bunge!!! Bunge hili sasa limekuwa ni Bunge la Wahuni.
 
Back
Top Bottom