Salary Slip
JF-Expert Member
- Apr 3, 2012
- 47,098
- 144,560
Naandika haya si kwa utani bali ni kutokana na uchungu nilionao kuona jinsi watu ambao tuliwatuma waende bungeni kutetea maslahi yetu jinsi walivyogeuka wasaliti wakubwa na kutanguliza maslahi ya chama chao badala ya wale waliowatuma!Inauma sana na kusikitisha na ni bora mwenyezi Mungu achukue roho zao ili kunusuru mamilioni ya watanzania ambao sasa ni wazi wamesalitiwa kwa kiasi kikubwa.
Kilichotokea leo bungeni hakina tofauti na kile kilichomtokea mh.Mbatia.Kwa wasiofahamu ni kwamba, hoja ya mh.Mnyika nayo imepigwa chini kwa kutumia wingi wa wabunge wa ccm baada ya naibu spika kuwahoji kama wanaunga mkono hoja hiyo iondolewe.Kama kawaida ya wabunge wa ccm wao ni chama kwanza na mwananchi baadae hivyo wengi wao waliafiki hoja hiyo ya mh.Mnyika iondolewe bila hata kujali athari za kuondoa hoja hiyo muhimu.
Kwa wale wasiokuwa na taarifa ni kuwa mh.Mnyika aliwasilisha hoja yake bungeni iliolenga kuondoa tatizo sugu la maji mkoani Dar-es-salaam lakini kwa hila za ccm hoja hiyo imekuwa ikipata upinzani na hatimae leo wameiondoa kwa kutumia wingi wao bungeni.
Hili jambo ni wazi limegeuzwa la kisiasa kwa kuona kuwa kama hoja hiyo ingepita labda mh.Mnyika na chama chake wangepata sifa kwahiyo ni bora waikwamishe.
Kwa kuzingatia matendo haya ya kinyama dhidi ya watanzania wanaoteseka na shida ya maji lakini wawakilishi wao wanaona ni bora waendelee na shida hiyo na nyingine nyingi kama vile elimu isiyo na mitaala basi ni bora mwenyezi Mungu awachukue wote kwa manufaa ya taifa hili.
CCM haya ndio maisha bora mliotuahidi!
Kilichotokea leo bungeni hakina tofauti na kile kilichomtokea mh.Mbatia.Kwa wasiofahamu ni kwamba, hoja ya mh.Mnyika nayo imepigwa chini kwa kutumia wingi wa wabunge wa ccm baada ya naibu spika kuwahoji kama wanaunga mkono hoja hiyo iondolewe.Kama kawaida ya wabunge wa ccm wao ni chama kwanza na mwananchi baadae hivyo wengi wao waliafiki hoja hiyo ya mh.Mnyika iondolewe bila hata kujali athari za kuondoa hoja hiyo muhimu.
Kwa wale wasiokuwa na taarifa ni kuwa mh.Mnyika aliwasilisha hoja yake bungeni iliolenga kuondoa tatizo sugu la maji mkoani Dar-es-salaam lakini kwa hila za ccm hoja hiyo imekuwa ikipata upinzani na hatimae leo wameiondoa kwa kutumia wingi wao bungeni.
Hili jambo ni wazi limegeuzwa la kisiasa kwa kuona kuwa kama hoja hiyo ingepita labda mh.Mnyika na chama chake wangepata sifa kwahiyo ni bora waikwamishe.
Kwa kuzingatia matendo haya ya kinyama dhidi ya watanzania wanaoteseka na shida ya maji lakini wawakilishi wao wanaona ni bora waendelee na shida hiyo na nyingine nyingi kama vile elimu isiyo na mitaala basi ni bora mwenyezi Mungu awachukue wote kwa manufaa ya taifa hili.
CCM haya ndio maisha bora mliotuahidi!