Yericko Nyerere
JF-Expert Member
- Dec 22, 2010
- 16,987
- 20,271
Bilionea mkubwa nchini Urusi ametangaza kukabiliana na Vladimir Putin katika uchaguzi mkuu wa rais wa mwaka ujao. Mikhail Prokhorov amesema ataunda chama kipya cha siasa ambacho kitawalenga watu wa kawaida nchini Urusi. Tajiri huo anamiliki timu ya basketbali New Jersey Net, pamoja na biashara kubwa zinazomfanya ashike nafasi ya tatu kwa utajiri nchini humo. wakati huohuo, waziri wa zamani wa fedha Alexei Kudrin ametoa wito wa kuundwa kwa chama cha kipya huru baada ya kutokea maandamano makubwa ya kupinga serikali, kutokana na tuhuma za wizi wa kura katika uchaguzi wa bunge uliofanyika mapema mwezi huu.