Biashara ya Vifaa vya Ujenzi (Hardware Store): Ushauri wa Mtaji, Uendeshaji, Changamoto na Faida

Habari za majukumu wadau wa jukwaa hili. Mi nafanya biashara ya duka la hardware kkoo na ninauza kwa jumla na rejareja. Natafuta wateja wa mikoNi kwa ajili ya kuwauzia baadhi ya bidhaa kwa jumla. Kama wapo wadau wa masuala haya ya hardware humu tuanze kiwasiliana na kuona tunafanyaje biashara. Sio wa mikoani tu, hata kwa wa dar pia. Karibuni
una cement?
 
Asanteni wachangiaji wote ila pia naombeni muweke na vifaa vya umeme

Mmebarikiwa
 
mkuu mi hii ndyo shuhuli yng nawafanyia shopping wadau walioko mikoan wanatumia pesa nawanunulia mzigo kisha nawatumia nina wadau mpk zambia km utakuwa na interest pliiz ni pm khs uaminifu ndyo key yng ktk hii biashara ucwe na hofu
Naomba kontact zako Mkuu!!
 
Mashine za kutumia mkono zinauzwa kuanzia laki 4,mpaka tatu na nusu(Sido kipawa)tofari moja moja kuanzia nchi tano mpaka sita,pia zipo machine za haina mbalimbali za tofari,mfano luvaanz nk,juz juzi nimeona kuna kampuni nyingine inatengeneza mashine za mkono na umeme zinatoa tofari mbilimbili,ni biashara mzuri ukipata eneo zuri,
SIDO kipawa ndio wapi?
 
hii kiboko aisee yaani mfuko mmoja wa saruji utoe tofali 55 hadi 60 !!!
hii nyumba ikinyeshewa na mvua inamong'onyoka aisee...kwavile ni nyumba ya mchanga hii
Ndio wafyatuaji wengi wanafanya hivyo, wengine wanatoa matofali 70 kwa mfuko hasa hawa wanaotumia mashine za umeme kufyatulia
 
uimara wa matofali unategemea na aina ya mchanga, aina ya maji unayotumia, aina ya cement, machine inayotumika kuyatengeneza na umwagiliaji wa maji baada ya kufyatua hasa hasa siku sita za kwanza tokea kufyatua. Mchanga wa kolongoni au unaopatikana kwa kuuuzoa mitaani ni tofauti sana na ule unaochukuliwa kule bagamoyo au maeneo ya kibaha kule, nimeona maeneo ya boko dsm watu wanachukua mchanga wa bagamoyo wanauchanganya na ule wa kolongoni kwa ratio ya 2:3 kupata tofari nzuri na kafaida. nadhani ule wa bagamoyo ni mzuri zaidi. Maji yakiwa na acid au salt sana sio mazuri kwa kufyatulia matofali, wataalam wa cement wanalijua hili chumvi ni adui mkubwa wa cement kwenye quality ya kukamata udongo (binding effect), aina ya cement na zenyewe ni sababu nyingine sio kila cement inafaa ukiwaona wataalam wa cement watakushauri kwa ubora zaidi juu ya hili, Twiga, rhino na ile ya pakistan nadhani ni bora sana. suala la machine pia ni muhimu nadhani kwenye uimara tofari la machine ya mkono ni tofauti sana na aliyetumia machine ya umeme yenye vibration na hii pia inachangiwa na uchanganyaji wa cemet na mchanga kupata equal distribution(mchanganyiko ulio sawa). tofali ukiwa mzembe kuzimwagilia maji tegemea asara ya tofali kupasuka, tofali baada ya siku moja tokea ufyatue lazima ulimwagilie maji ya kutosha asubuhi na jioni kwa muda walau siku tano. huo ndio mchango wangu ahsante.
Very detailed, excellent
 
Hapana mkuu... sipo kwenye hii biashara ila nina uzoefu kidogo saana juu yake. Hivo basics za nini cha kuzingatia wakati wa kutaka kuanza, wapi mzigo ni rahisi zaidi na namna gani wewe unaweza nunua bei ya juu/chini kuliko wengine eneo moja, nini cha kuzingatia kwa ajii ya wateja wako, the do's and don'ts za biashara, namna ya kuboresha na mambo ya kufanania hivo naweza kukujibu... Kwa kina zaidi itahitaji mzoefu.

Hata hivo nashukuru kwa acknowledgements.
Mkuu najua hii habari ni ya zamani kidogo,unaweza kutupa do's and don'ts za hii biashara,wapi mali zinapatikana na kwa bei ya afadhali,atleast tuanze mwaka na idea mpya mkuu.
Have a prosperous coming year,cheers.
Hapana mkuu... sipo kwenye hii biashara ila nina uzoefu kidogo saana juu yake. Hivo basics za nini cha kuzingatia wakati wa kutaka kuanza, wapi mzigo ni rahisi zaidi na namna gani wewe unaweza nunua bei ya juu/chini kuliko wengine eneo moja, nini cha kuzingatia kwa ajii ya wateja wako, the do's and don'ts za biashara, namna ya kuboresha na mambo ya kufanania hivo naweza kukujibu... Kwa kina zaidi itahitaji mzoefu.

Hata hivo nashukuru kwa acknowledgements.
 
Habari wakuu,

Mimi Niko Mwanza, naomba ushauri jinsi ya kuanzisha biashara ya Hardware (vifaa vya ujenzi), mtaji wa kima cha chini kabisa, na changamoto zake ni zipi.

Mzigo ntanunua wapi, nk
 
Habari wakuu,Mimi Niko Mwanza,naomba ushauri jinsi ya kuanzisha biashara ya Hardware (vifaa vya ujenzi),mtaji wa kima cha chini kabisa,na changamoto zake ni zipi....<br />Mzigo ntanunua wapi,nk
 
Inategemeana na focus yako.

Ila kwa mil 5 unaweza anza na vitu vidogo vidogo...then nondo, cement na chuma ukaja kuongeza baadaye..
Ila hakikisha ununue vitu ambavyo vinatembea ili kuboost mtaji!

Kingine ni vizuri ukachanganya na vifaa vya umeme, maana tunachoangalia ni mzunguko..na vifaa vya umeme vinatembea na vinalipa zaidi kuliko vya ujenzi!
 
Changamoto ni mzunguko, jitahidi kupata location nzuri..maana kuna vitu unaweza weka na vikakaa hata mwaka hujauza kwahiyo inabidi uwe mpole huku unaendelea kulisoma soko linahitaji nini!!
 
Inategemeana an focus yako...

Ila kwa mil 5 unaweza anza na vitu vidogo vidogo...then nondo, cement na chuma ukaja kuongeza baadaye..
Ila hakikisha ununue vitu ambavyo vinatembea ili kuboost mtaji!

Kingine ni vizuri ukachanganya na vifaa vya umeme, maana tunachoangalia ni mzunguko..na vifaa vya umeme vinatembea na vinalipa zaidi kuliko vya ujenzi!
Asante mkuu,wazo lako ninalifanyia kazi..ubarikiwe
 
Inategemeana an focus yako...

Ila kwa mil 5 unaweza anza na vitu vidogo vidogo...then nondo, cement na chuma ukaja kuongeza baadaye..
Ila hakikisha ununue vitu ambavyo vinatembea ili kuboost mtaji!

Kingine ni vizuri ukachanganya na vifaa vya umeme, maana tunachoangalia ni mzunguko..na vifaa vya umeme vinatembea na vinalipa zaidi kuliko vya ujenzi!
Nalifanyia kazi wazo laki mkuu,hapa ni mahali penye mzunguko wa kutosha,watu wengi hupita kwenda mkazin na wengine kwenye mishemishe zao..kuanzia saa 11jion watu ni wengi wanaopita maeneo haya,na hasubuhi vivo hivyo mchana hupungua kiasi mkuu
 
Back
Top Bottom