Biashara ya Ubunge yawafanya Wabunge wa CCM Kuadimika Bungeni

eedoh05

JF-Expert Member
Apr 20, 2011
632
234
Bunge linaloendelea na vikao vyake mjini Dodoma, leo katika kikao chake cha jioni limelazimika kuahirishwa kutokana na mahudhurio hafifu ya wabunge hususani wa CCM. Tatizo hili limekuwa sugu, halirekebishiki. Wananchi wamekuwa wakilalamika juu ya mwenendo huu wa bunge. Wananchi wamesahau ghafla na mapema mno kwamba wabunge wa CCM (takribani wote yaani 100%) waliununua ubunge huo na hawakutumwa bungeni na wananchi.

Wabunge wa CCM waliununua ubunge huo kwenye kura za maoni ili chama chao kiwapendekeze kugombea ubunge; waliununua ubunge huo kwenye kamati kuu ya chama chao ili majina yao yapitishwe kugombea ubunge kwa tiketi ya chama chao; waliununua ubunge huo wakati wa kampeni za uchaguzi; waliununua ubunge huo wakati wa kuhesabu kura; waliununua ubunge huo wakati wa kutangazwa matokeo.

Kwa mantiki hiyo, hakuna mbunge wa CCM atakayewajibika kwa wananchi wa jimbo lake. Wabunge hawa wanawajibika kwa chama chao kwa kuwa chama ndicho huwajengea mazingira ya kuununua ubunge.

Hivyo basi, mwananchi uache kuwalaumu wabunge kwa kutokukuwakilisha bungeni. Jilaumu mwenyewe kwa kukubali kununuliwa na wabunge hao kwani, ninapomlipa mpiga zumari uchaguzi wa wimbo wa kuchezwa uko kwangu. Tujifunze kwa watu wa kusini kuanzia vijana hadi ajuza pasipokujali itikadi za vyama wala dini wameonesha kugutuka. Sauti ya radio Ujerumani inasema "VIJANA TUGUTUKE". Mwaka 2015 sio mbali tuchangamkie daftari la kudumu la wapiga kura. Duniani kote, ukombozi huanza na kutimilizwa na vijana, HAKIKA VIJANA TUGUTUKE!
 
Tatizo ni mfumo mzima.Bunge lazima libadilishe taratibu.Munge kuwa Waziri au kuwa katika Kamati za bunge ni zahili watakosekana wakati wote.Hata wange kuwa wapinzani nao wangekosekana.Tujaribu kurekebisha taratibu hizo otherwise hatutafika twendako.Mbona wakina Zito,Mrema nk muda wote hawako bungeni?
 
Wengi wa Watanzania bado ni wajinga.WATAENDELEA KUWA WAJINGA HADI YESU ATAKAPORUDI.
Mtanzania gani mwenye akili timamu anaipigia kura CCM????? Kama una akili timamu huwezi hata kutambua kwa nini naletewa kanga, chumvi, napewa hela n.k wakati wa kampeni na pasipo kujiuliza baada ya hapo kuna nini??????????????
Ujinga ukiwatoka watanzania ndipo tutakuwa na maendeleo.
Mfano, wale watu wa KUSINI, UJINGA UMESHAWATOKA TAYARI-Je na mimi ujinga umenitoka au bado??????? JIJIBU MWENYEWE.
 
Tatizo ni mfumo mzima.Bunge lazima libadilishe taratibu.Munge kuwa Waziri au kuwa katika Kamati za bunge ni zahili watakosekana wakati wote.Hata wange kuwa wapinzani nao wangekosekana.Tujaribu kurekebisha taratibu hizo otherwise hatutafika twendako.Mbona wakina Zito,Mrema nk muda wote hawako bungeni?
Wangekuwa wanakosekana kwa sababu ya kuhudhuria katika kamati za bunge sio tatizo ni sehemu ya shughuri zao bungeni. Wao ni watoro, NDIYO maana hata Spika Anne Makinda analalamika. Hawana hoja ya kujitetea wala kutetewa.
 
wabunge wa chadema washamba,wakorofi.ukiwapa nchi cha kwanza watakachofanya ni kujinunulia maipad,magari ya kifahari,majumba ya kifahari nk.mfano halima mdee anavaa dhahabu mwili mzima.hapo hajapata uwaziri lo balaa.mungu asitujaalie.2015 ni ccm tu.
 
Redarmy wewe ni kama mojawapo ya wale wapumbavu. Kama ni kurogwa, basi alokuroga keshakufa ni mwana ccm.
 
Back
Top Bottom