Biashara ya Dagaa: Mjadala wa Uendeshaji, Masoko, Faida, Hasara na Changamoto zake

Wazo lako la kupanua wigo wa kibiashara ni zuri

Nimewahi kuifanya hii biashara miaka 5 iliyopita kwa Dar, haikunipa matunda sana nikaamua kuacha.

Sababu kubwa ilikuwa udalali kama kawaida zilivyobiashara nyingi za Dar.

Sababu ya pili ni soko jinsi unavyonunua na kuuza ni tofauti.

Mwanza utanunua kwa debe ila Dar utauza kwa kilo soko halitambui kipimo cha debe.

Changamoto inakuja kwenye aina ya dagaa na uzito utakaotoa, kuna uwezekano mkubwa sana wakukupoteza mtaji.

Unakonunua unakutana na madalali lazima wakupige unakoenda kuuza pia unakutana na madalali lazima ule nao, hapo unategemea utapata nini? mbaya zaidi uwe mgeni kabisa katika hii biashara na dagaa hauwajui vizuri.

Kwa upande wa Tunduma ndipo ninapopatikana ila sijawahi kuifanya huku, lakini nimewahi kufatilia jinsi soko lilivyo ikohivi;

Tunduma wananunua na kuuza kwa debe kama ilivyo Mza, bei ya sasa sifahamu mpaka niulizie.

Unatafuta mtu wa kufanya nae biashara unamtumia mzigo anauza kisha anakutumia pesa kulingana na makubaliano yenu

Wafanyabiashara wengi huku wanamiliki stoo ila mtaji wa mzigo hawana, wenye mitaji mikubwa wanafata wenyewe na kuwasambazia wenye stoo wasiyokuwa na mtaji kwa mali kauli.

Kwahiyo usiwe na matumaini makubwa sana kwamba utapiga hela kwa muda mfupi sababu tayari kuna watu wameshatengeneza falme zao katika biashara hii, labda uje na mbinu na mawazo mapya.

Biashara ya dagaa hapa haijachangamka sana na wanunuzi wakubwa wa hii bidhaa ni jirani zetu Wazambia na Wakongo, lakini kwa upande wa Wazambia wanapendelea zaidi furu wale samaki wadogo wadogo wanaochambuliwa toka kwenye dagaa nafikiri unawafahamu.

Hivyo kama utakuja angalia soko la furu huko Mwanza na huku Tunduma, lakini ukiweza angalia pia soko la vibambara vya sangara havipo huku.

Aina ya dagaa wenye bei huku ni wale wa nyasi wanatoka Bukoba na wale wa mafuta waliyokaangwa

Kuhusu usafirishaji mwaka 2017 kwa gunia moja la dagaa toka Mwanza mpaka Tunduma ilikuwa 7000 kwasasa sifahamu, Utauliza huko Mwaloni(soko la dagaa) Mwanza.

Mwisho japo siyo kwa umuhimu;

Karibu Tunduma border ya wajanja lango kuu la nchi 8 za SADEC Tanzania.
Asante mkuu, ubarikiwe
 
k
Al a Kama unasemea wale watu was custom market research and feasibility study,nishawatumia email,nasubiri tu kam a watanijibu nitakuwa na information zote kuhusu soko la dagaa wachafu Nairobi
Mkuu ulishawapata hao jamaa utupe mrejesho, Corona inaelekea ukingoni na mwakani utalii utarudi so demand ya kukuu utarudi kwenye normal, hence chakula cha kukuu
 
Ila hii biashara nayo itakuwa inalipa sana,naona fuso kirumba mwaloni zinapakia daily,
kuna dada wa kikenya alikuwa anafuata mwaloni hao dagaa wachafu kwa ajili ya kupeleka nairobi kwenye viwanda vya chakula cha kuku ,alikuwa na pesa chafu ,
nadhani hao wanaopeleka arusha huwa wanavuka hadi Nai.

Kuna jamaa mkenya ana kampuni ya marketing research,yeye unamlipa pesa si nyingi anafanya legwork kuzunguka Nai kulitafuta chimbo,sema link yake ndo iko mbali nikiipata ntaiweka hapa,yeye anaweza kukupa infor zote kuanzia bei,procedure,mbinu na contact za hivyo viwanda vya chakula cha kuku na wala fee yake haizidi 20,000 ya kibongo
Mkuu naomba uniunganishe na huyo jamaa mkenya tufanye biashara.
 
Laki tano inatosha kwa kuanzia,itakuwa taratibu kama utakuwa na nidhamu ya fedha.,usilete kwanza mikoani...we we nenda kisiwa goziba,au kimoyomoyo,mlumo,ghana,ukawe unanunua dagaa wabichi unawaanika huko huko wakikauka unauzia huko huko mpaka mtaji utakapokuwa mkubwa kuweza kusafirisha mikoani,

AU huko huko visiwani nunua then safirisha uje uuzie kirumba mwaloni...usihangaike kupeleka mikoani...
Sina uchoyo na wazo la biashara kumsaidia mtu yoyoye.
Mwingine anayehitaji ushauri zaidi wa biashara ya kufanya sema hapa nitakupa cha kufanya ili mradi tu uwe na ule msukumo ndani ya moyo wako kufanya biashara bila kutafuta sababu.
Shukrani mkuu changamoto zake Zipi
 
Boss! Nimependa


Boss! Nimependa Sana ushauri wako,na nimependa Kwa jinsi ulivoonesha moyo wa kumsaidia mtu kimawazo.
Binafsi napenda Sana biashara ya dagaa Ila Mimi nafanya biashara ya dagaa chafu Kwa ajili ya chakula ya kuku. Niseme ukweli namtumia dalali ambaye nikinunua mzigo huku mwanza nafunga nakumkabidhi dagaa anapeleka kiwandani alafu akimaliza kuuza ananiletea mtaji na faida yangu.

Nafanya vile kwasabb nafanya kazi za serikali na siwezi kuzifanya mwenyewe. Wala siwezi kupata mda wa kupeleka dagaa mwenyewe,kwahiyo mwanza nachukua let say dagaa wa milion 3 au mil5 namkabidhi. Anaenda kuuza Arusha na sijui anapata faida kiasi gani Ila Mimi ninachojali aniletee faida nzuri. Na mpaka sasa dalali huyo Niko naye ndo tunafanya biashara wote,NAOGOPA KUMWAMBIA TWENDE WOTE MAANA ATAONA KAMA NIMEMSTUKIA NA ATAWEZA KUNIKIMBIA,KUSEMA KWELI SIJUI MASOKO YAKO WAPI ARUSHA NA SIJAWAHI KUFIKA JAPO NATAMANI NIFANYE MWENYEWE.

MWENYE KUNISAIDIA MAWAZO PLEASE 0764789563
Duu dagaa chafu unachukulia wapi
 
Habari
Ila hii biashara nayo itakuwa inalipa sana,naona fuso kirumba mwaloni zinapakia daily,
kuna dada wa kikenya alikuwa anafuata mwaloni hao dagaa wachafu kwa ajili ya kupeleka nairobi kwenye viwanda vya chakula cha kuku ,alikuwa na pesa chafu ,
nadhani hao wanaopeleka arusha huwa wanavuka hadi Nai.

Kuna jamaa mkenya ana kampuni ya marketing research,yeye unamlipa pesa si nyingi anafanya legwork kuzunguka Nai kulitafuta chimbo,sema link yake ndo iko mbali nikiipata ntaiweka hapa,yeye anaweza kukupa infor zote kuanzia bei,procedure,mbinu na contact za hivyo viwanda vya chakula cha kuku na wala fee yake haizidi 20,000 ya kibongo
Mkuu ukizipata infor zake huyo jamaa na mimi naomba unitag. Pls.
 
Habari

Mkuu ukizipata infor zake huyo jamaa na mimi naomba unitag. Pls.
Haya huyu hapa,ukitaka kumtuma ajutafutie soko la dagaa nairobi
Screenshot_20200914-143622.png

Mtumie email yako kwa namba hiyo chini.
 
Huyo mdada mkenya anaekuja kununua dagaa wa mchanga (wachafu)kwa ajili ya kutengeneza chakula cha kuku. Natafuta soko la kuuza dagaa wa mchanga (wachafu). Shukrani sana mkuu
Ha ha ha,,huyo saa hii atakuwa kishastaafu bana,,we sema nikufanyie mafekeche nikutafutie adress zote za viwanda vya chakula cha kuku huko kenya,ila inahitaji nipate mda kidogo..
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom