UmkhontoweSizwe
Platinum Member
- Dec 19, 2008
- 8,529
- 7,733
Juzi nimeenda benki kwa nia ya kutuma pesa kidogo kwenda US lakini masharti niliyoyakuta huko sikuamini. Kwanza, Nikaambiwa kama natuma fedha kwa madhumuni ya kibiashara ni lazima nipeleke pro-forma invoice. Nikashindwa kuelewa. Pro-forma invoice ya nini wakati mimi sifanyi manunuzi yoyote ya kiserikali? Mimi siyo taasisi au kitengo cha serikali bwana. Mliwaacha kina Chenge wakanunua ndege ya serikali kwa pro-forma invoice za kughushi mnakuja kutubana sisi watu binafsi?!
Pili, nikaambiwa kama natuma kwa mtu binafsi lazima nilete barua toka kwa mtu ninayemtumia kuonyesha kuwa anahitaji pesa. Kama ni mwanafunzi basi barua itoke shuleni kwake, I-20 yake, Visa etc.
Goooosh, yaani masharti mengine hayana hata msingi. Personal issue yangu mpaka nikawatangazie watu waandike barua! Yaani pasa yangu, kuitumia mpaka Benki Kuu watake! Upuuzi wa hali ya juu. Wamezoea enzi za ujamaa wanadhani dunia bado imesimama kuwasubiri wao na sera zao zisizoleta ufanisi wowote. Nikihamisha akaunti yangu kupeleka Kenya ambako hakuna masharti watu wataniona siyo mzalendo. Lakini sera zetu zinakirihisha na kukatisha tamaa.
Benki Kuu: Fungueni milango itakayohamasisha watu kuingiza $$ zaidi nchini, badala ya kubana njia za kutumia ili kulinda tu kidogo kilichopo. Hizo sera zimepitwa na wakati.
Ombi: jamani nahitaji kutuma $$ kiasi kwenda US. Kama kuna mtu anajua njia nzuri na salama, tafadha naomba un-PM, I'll contact you. For those in the US, I can give the money here (Bongo), and you deliver the same amount to my colleague in the US. He needs money before Thursday next week.
Note: Ni kwa shughuli ambayo ni LEGAL, so shouldn't have to worry.
Thanks in advance.
Pili, nikaambiwa kama natuma kwa mtu binafsi lazima nilete barua toka kwa mtu ninayemtumia kuonyesha kuwa anahitaji pesa. Kama ni mwanafunzi basi barua itoke shuleni kwake, I-20 yake, Visa etc.
Goooosh, yaani masharti mengine hayana hata msingi. Personal issue yangu mpaka nikawatangazie watu waandike barua! Yaani pasa yangu, kuitumia mpaka Benki Kuu watake! Upuuzi wa hali ya juu. Wamezoea enzi za ujamaa wanadhani dunia bado imesimama kuwasubiri wao na sera zao zisizoleta ufanisi wowote. Nikihamisha akaunti yangu kupeleka Kenya ambako hakuna masharti watu wataniona siyo mzalendo. Lakini sera zetu zinakirihisha na kukatisha tamaa.
Benki Kuu: Fungueni milango itakayohamasisha watu kuingiza $$ zaidi nchini, badala ya kubana njia za kutumia ili kulinda tu kidogo kilichopo. Hizo sera zimepitwa na wakati.
Ombi: jamani nahitaji kutuma $$ kiasi kwenda US. Kama kuna mtu anajua njia nzuri na salama, tafadha naomba un-PM, I'll contact you. For those in the US, I can give the money here (Bongo), and you deliver the same amount to my colleague in the US. He needs money before Thursday next week.
Note: Ni kwa shughuli ambayo ni LEGAL, so shouldn't have to worry.
Thanks in advance.