Ng'wanza Madaso
JF-Expert Member
- Oct 21, 2008
- 2,268
- 333
Uchunguzi umeanika uovu ambao umekita mizizi.
Hii imekuwa wiki yenye shughuli muhimu katika harakati za serikali ya Tanzania kupambana na vitendo vya mauaji ya Albino katika maeneo ya kanda ya Ziwa Victoria.
Uovu huo umejikita katika mikoa ya Mwanza, Mara, Shinyanga na Kagera.
Maeneo hayo ya historia ya kisirani cha kuwaua vikongwe katika miaka ya 1970, hasa kutokana na macho yao mekundu.
Mauaji hayo ya Albino, vikongwe na wanaume wenye upara yalichochewa na imani za kishirikina.
Uhalifu huu umekuwa ukiendelea kana kwamba serikali haina uwezo au mbinu mwafaka za kuuangamiza.
Mapema mwaka uliopita, Mwandishi wa BBC, Vicky Ntetema alianza kudadisi kiini cha mauaji ya Albino katika maeneo hayo ya Ziwa Victoria.
Albino wanaishi kwa hofu
Ilikuwa safari ndefu, nyeti, yenye utelezi na hatari huku ikihitaji subira na ujasiri.
Siku baada ya siku, Vicky alikutana na wahusika mbalimbali katika biashara hiyo ya kiza.
Ukitaka kujua ni nani anawaua Albino, kwa nini wanauawa basi soma Blog ya Vicky. Una uhuru wa kuchangia mada.
Soma Blog ya Vicky Ntetema
Source BBC
Hii imekuwa wiki yenye shughuli muhimu katika harakati za serikali ya Tanzania kupambana na vitendo vya mauaji ya Albino katika maeneo ya kanda ya Ziwa Victoria.
Uovu huo umejikita katika mikoa ya Mwanza, Mara, Shinyanga na Kagera.
Maeneo hayo ya historia ya kisirani cha kuwaua vikongwe katika miaka ya 1970, hasa kutokana na macho yao mekundu.
Mauaji hayo ya Albino, vikongwe na wanaume wenye upara yalichochewa na imani za kishirikina.
Uhalifu huu umekuwa ukiendelea kana kwamba serikali haina uwezo au mbinu mwafaka za kuuangamiza.
Mapema mwaka uliopita, Mwandishi wa BBC, Vicky Ntetema alianza kudadisi kiini cha mauaji ya Albino katika maeneo hayo ya Ziwa Victoria.
Albino wanaishi kwa hofu
Ilikuwa safari ndefu, nyeti, yenye utelezi na hatari huku ikihitaji subira na ujasiri.
Siku baada ya siku, Vicky alikutana na wahusika mbalimbali katika biashara hiyo ya kiza.
Ukitaka kujua ni nani anawaua Albino, kwa nini wanauawa basi soma Blog ya Vicky. Una uhuru wa kuchangia mada.
Soma Blog ya Vicky Ntetema
Source BBC