Ibrah
JF-Expert Member
- Mar 22, 2007
- 2,729
- 528
Katika redio za kimataifa zinazopendwa nchini ni Idhaa ya Kiswahili ya BBC LOndon. Kwa kweli tangu aondoke Tido Mhando kama Mkuu wa Idhaa hiyo, viwango vyao vimeporomoka sana na ingawa husikiliza BBC Idhaa ya Kiswahili kila siku bado sivutiwi na utendaji wao wa kazi hasa Watangazaji wao wa siku hizi huko London na Nariobi.
Kuna baadhi ya watangazaji wa Idhaa hiyo ambao lugha yao ya kwanza si Kiswahili na hutumia Kiswahili kibovu (simaanishi lafudhi bali broken swahili). Kama ingekuwa ni Wawakilishi wao wa nchi za Uganda, Somalia au Kongo nisingeshangaa lakini ni baadhi yao ni Waajiriwa kabisa hapo HQ London!
Kero nyingine ni tabia iliyozuka siku hiozi ya Idhaa hii kuturushia matangazo yalliyorekodiwa siku moja au mbili. Mfano ni kipindi cha michezo siku moja kabla ya mechi ya Man Utd na Arsenal ambacho walikirusha tena siku ya jumatatu asubuhi!
Kwa kweli walini-bore sana. Yaani walishindwa kuandaa kipindi! Ni afadhali wasingekuwa na kipindi cha michezo siku hiyo kuliko kutuambia ati kesho kutakuwa na mechi kali baina ya Man U na Arsenal wakati mechi ilichezwa jana!
Kuna baadhi ya watangazaji wa Idhaa hiyo ambao lugha yao ya kwanza si Kiswahili na hutumia Kiswahili kibovu (simaanishi lafudhi bali broken swahili). Kama ingekuwa ni Wawakilishi wao wa nchi za Uganda, Somalia au Kongo nisingeshangaa lakini ni baadhi yao ni Waajiriwa kabisa hapo HQ London!
Kero nyingine ni tabia iliyozuka siku hiozi ya Idhaa hii kuturushia matangazo yalliyorekodiwa siku moja au mbili. Mfano ni kipindi cha michezo siku moja kabla ya mechi ya Man Utd na Arsenal ambacho walikirusha tena siku ya jumatatu asubuhi!
Kwa kweli walini-bore sana. Yaani walishindwa kuandaa kipindi! Ni afadhali wasingekuwa na kipindi cha michezo siku hiyo kuliko kutuambia ati kesho kutakuwa na mechi kali baina ya Man U na Arsenal wakati mechi ilichezwa jana!