Zak Malang
JF-Expert Member
- Dec 30, 2008
- 5,404
- 234
Mgombea ubunge kwa ticketi ya CCM Jimbo la Arusha Mjini Dkt. Batilda Buriani, anadaiwa kufanikiwa kuukwepa mtego uliowekwa na maafisa wa TAKUKURU Arusha wa kumkamata kwa tuhuma za kutoa fedha kwa wapambe wake jana usiku.
Habari zinasema Bi Burian aliruka mtego wa maafisa hao baada ya kuchelewa kufika kwenye hoteli ya Cet Garden ambapo wapambe wake wanaodaiwa kuwa zaidi ya 10 waliishia mkononi mwa maafisa wa TAKUKURU.
Tukio hilo lilitokea juzi majira ya saa mbili na nusu usiku hoteli ya Cet Garden ambapo inadaiwa TAKUKURU walienda kwenye hoteli hiyo baada ya kupata taarifa kuwa Bi Burian alikuwa na kikao cha siri baina ya wapambe hao usiku huo .
.Habari zaidi katika Majira ya leo.