Barua ya Wazi kwa Rais Samia kuhusu Bomoa Bomoa ya Madanguro

BARD AI

JF-Expert Member
Jul 24, 2018
3,377
8,121
Ndugu Rais, naamini una uzima wa kutosha asubuhi ya leo. Ukiiangalia video hii kwa haraka haraka utawaona “wahuni” na “watu wasiokuwa na maadili” wakifanya biashara ya “ukahaba.” Lakini ukiangalia kwa umakini, hautowaona wahuni, utaona kundi kubwa la watanzania maskini wanaoishi maisha ya tabu na mateso. Ukiangalia kwa umakini zaidi, utawaona wapiga kura wako ambao umaskini umewalazimisha leo waonekane kama wadhambi kuliko watanzania wote.

Mhe. Rais, kinachofanywa na Mkuu wa Mkoa hapa wala sio kukamata “makahaba” na “kufungia madanguro,” kinachofanyika ni kumdhalilisha maskini kwa sababu ya umaskini wake. Nasema hivi kwa sababu wenzao wanaofanyia “ukahaba” kwenye guest houses za elfu thelathini kule Sinza kuhudumia wateja wa tabaka la kati au wale wanaofanyia kwenye mahoteli yaliyopo ufukweni wakihudumia wateja wa tabaka la wenye nacho, wao hawabughudhiwi. Kwa hiyo hawa kwenye video wanaadhibiwa kwa sababu umaskini wao unaonekana wazi na unawakera viongozi.

Mhe. Rais, usinielewe vibaya. Sipingi kinachofanywa na Mhe. Mkuu wa Mkoa, ila najiuliza, kwa nini viongozi mnakerwa na muonekano wa maisha ya watu wenu lakini hamkerwi na mambo yanayosababisha hawa watu waishi maisha haya? Kwa mujibu wa taasisi ya UNAIDS, Tanzania kuna zaidi ya wanawake 150,000 wanaojihusisha na biashara ya ukahaba. Wametoka wapi wote hawa? Wala usiumize kichwa sana Mhe. Rais, nitakukumbusha. Hawa ndio wale vijana waliomaliza kidato cha nne wakarudi nyumbani bila maarifa yoyote yenye tija. Ndio wale ambao NECTA wanasemaga “asilimia 75% wamepata Division Four na Zero.” Wengine ndio wale waliomaliza vyuo vikuu wakakosa ajira na elimu waliyopewa haijawaandaa kujiajiri, waende wapi? Walio pambana sana ndio wale wamekuwa waendesha bodaboda na wengine mama ntilie, hizo ndio zimekuwa kazi za ndoto zao.

Mhe. Rais, kama hawa wangeweza kupewa mafunzo mbadala, kukuzwa na kuendeleza vipaji vyao, na kukopeshwa mitaji, labda leo wasingekuwa wanatweza utu wao kwa kiwango hiki. Hata hivyo zile fedha za kufanyia haya ndio serikali yako imeamua iwanunulie viongozi magari ya kifahari; iwaongezee wabunge mishahara kimono; na hivi karibuni itawagawia wake wa viongozi ambao tayari wanaogelea kwenye utajiri. Fedha nyingine ndio zile zimepigwa kwa mabilioni kwenye report ya kamati ya kudumu ya bunge hesabu za serikali (PAC). Hizi ndio fedha zinazotumika kutengeneza wale vijana mashuhuri unaowaona kule Israel, Singapore, China, Finland, etc. Hawana uchawi wowote Mhe. Rais, wameamua kujali tu.

Nihitimishe Mhe. Rais, hawa maskini ambao leo wanasambazwa kwenye media kama object of mockery kwa taifa hawakuchagua kufanya haya. Nikuone basi, tunapoenda kuwanyanyasa kwa umaskini wao, basi angalau hata tuwatunzie utu wao kwa kuficha sura zao. Kuwapa adhabu ya public shame juu ya mzigo wa umaskini wanaoubeba ni sawa na kuwaua angali bado wapo hai. Na la mwisho, Mhe. Rais, ikikupendeza, basi mwambie mkuu wa Mkoa anapowaambia waondoke na waache kufanya wanachokifanya, basi awaambie pia waende wapi na wakafanye nini kama mbadala wa hiki.

Nakushuru sana kwa muda wako.

Wako
Onesmo Mushi
 
Ndugu Rais, naamini una uzima wa kutosha asubuhi ya leo. Ukiiangalia video hii kwa haraka haraka utawaona “wahuni” na “watu wasiokuwa na maadili” wakifanya biashara ya “ukahaba.” Lakini ukiangalia kwa umakini, hautowaona wahuni, utaona kundi kubwa la watanzania maskini wanaoishi maisha ya tabu na mateso. Ukiangalia kwa umakini zaidi, utawaona wapiga kura wako ambao umaskini umewalazimisha leo waonekane kama wadhambi kuliko watanzania wote.

Mhe. Rais, kinachofanywa na Mkuu wa Mkoa hapa wala sio kukamata “makahaba” na “kufungia madanguro,” kinachofanyika ni kumdhalilisha maskini kwa sababu ya umaskini wake. Nasema hivi kwa sababu wenzao wanaofanyia “ukahaba” kwenye guest houses za elfu thelathini kule Sinza kuhudumia wateja wa tabaka la kati au wale wanaofanyia kwenye mahoteli yaliyopo ufukweni wakihudumia wateja wa tabaka la wenye nacho, wao hawabughudhiwi. Kwa hiyo hawa kwenye video wanaadhibiwa kwa sababu umaskini wao unaonekana wazi na unawakera viongozi.

Mhe. Rais, usinielewe vibaya. Sipingi kinachofanywa na Mhe. Mkuu wa Mkoa, ila najiuliza, kwa nini viongozi mnakerwa na muonekano wa maisha ya watu wenu lakini hamkerwi na mambo yanayosababisha hawa watu waishi maisha haya? Kwa mujibu wa taasisi ya UNAIDS, Tanzania kuna zaidi ya wanawake 150,000 wanaojihusisha na biashara ya ukahaba. Wametoka wapi wote hawa? Wala usiumize kichwa sana Mhe. Rais, nitakukumbusha. Hawa ndio wale vijana waliomaliza kidato cha nne wakarudi nyumbani bila maarifa yoyote yenye tija. Ndio wale ambao NECTA wanasemaga “asilimia 75% wamepata Division Four na Zero.” Wengine ndio wale waliomaliza vyuo vikuu wakakosa ajira na elimu waliyopewa haijawaandaa kujiajiri, waende wapi? Walio pambana sana ndio wale wamekuwa waendesha bodaboda na wengine mama ntilie, hizo ndio zimekuwa kazi za ndoto zao.

Mhe. Rais, kama hawa wangeweza kupewa mafunzo mbadala, kukuzwa na kuendeleza vipaji vyao, na kukopeshwa mitaji, labda leo wasingekuwa wanatweza utu wao kwa kiwango hiki. Hata hivyo zile fedha za kufanyia haya ndio serikali yako imeamua iwanunulie viongozi magari ya kifahari; iwaongezee wabunge mishahara kimono; na hivi karibuni itawagawia wake wa viongozi ambao tayari wanaogelea kwenye utajiri. Fedha nyingine ndio zile zimepigwa kwa mabilioni kwenye report ya kamati ya kudumu ya bunge hesabu za serikali (PAC). Hizi ndio fedha zinazotumika kutengeneza wale vijana mashuhuri unaowaona kule Israel, Singapore, China, Finland, etc. Hawana uchawi wowote Mhe. Rais, wameamua kujali tu.

Nihitimishe Mhe. Rais, hawa maskini ambao leo wanasambazwa kwenye media kama object of mockery kwa taifa hawakuchagua kufanya haya. Nikuone basi, tunapoenda kuwanyanyasa kwa umaskini wao, basi angalau hata tuwatunzie utu wao kwa kuficha sura zao. Kuwapa adhabu ya public shame juu ya mzigo wa umaskini wanaoubeba ni sawa na kuwaua angali bado wapo hai. Na la mwisho, Mhe. Rais, ikikupendeza, basi mwambie mkuu wa Mkoa anapowaambia waondoke na waache kufanya wanachokifanya, basi awaambie pia waende wapi na wakafanye nini kama mbadala wa hiki.

Nakushuru sana kwa muda wako.

Wako
Onesmo Mushi
Point ya kuipa uzito huruma haiko vizuri, rejea yako haijasema nini kifanyike. Yajayo yanafurahisha
 
Ndugu Rais, naamini una uzima wa kutosha asubuhi ya leo. Ukiiangalia video hii kwa haraka haraka utawaona “wahuni” na “watu wasiokuwa na maadili” wakifanya biashara ya “ukahaba.” Lakini ukiangalia kwa umakini, hautowaona wahuni, utaona kundi kubwa la watanzania maskini wanaoishi maisha ya tabu na mateso. Ukiangalia kwa umakini zaidi, utawaona wapiga kura wako ambao umaskini umewalazimisha leo waonekane kama wadhambi kuliko watanzania wote.

Mhe. Rais, kinachofanywa na Mkuu wa Mkoa hapa wala sio kukamata “makahaba” na “kufungia madanguro,” kinachofanyika ni kumdhalilisha maskini kwa sababu ya umaskini wake. Nasema hivi kwa sababu wenzao wanaofanyia “ukahaba” kwenye guest houses za elfu thelathini kule Sinza kuhudumia wateja wa tabaka la kati au wale wanaofanyia kwenye mahoteli yaliyopo ufukweni wakihudumia wateja wa tabaka la wenye nacho, wao hawabughudhiwi. Kwa hiyo hawa kwenye video wanaadhibiwa kwa sababu umaskini wao unaonekana wazi na unawakera viongozi.

Mhe. Rais, usinielewe vibaya. Sipingi kinachofanywa na Mhe. Mkuu wa Mkoa, ila najiuliza, kwa nini viongozi mnakerwa na muonekano wa maisha ya watu wenu lakini hamkerwi na mambo yanayosababisha hawa watu waishi maisha haya? Kwa mujibu wa taasisi ya UNAIDS, Tanzania kuna zaidi ya wanawake 150,000 wanaojihusisha na biashara ya ukahaba. Wametoka wapi wote hawa? Wala usiumize kichwa sana Mhe. Rais, nitakukumbusha. Hawa ndio wale vijana waliomaliza kidato cha nne wakarudi nyumbani bila maarifa yoyote yenye tija. Ndio wale ambao NECTA wanasemaga “asilimia 75% wamepata Division Four na Zero.” Wengine ndio wale waliomaliza vyuo vikuu wakakosa ajira na elimu waliyopewa haijawaandaa kujiajiri, waende wapi? Walio pambana sana ndio wale wamekuwa waendesha bodaboda na wengine mama ntilie, hizo ndio zimekuwa kazi za ndoto zao.

Mhe. Rais, kama hawa wangeweza kupewa mafunzo mbadala, kukuzwa na kuendeleza vipaji vyao, na kukopeshwa mitaji, labda leo wasingekuwa wanatweza utu wao kwa kiwango hiki. Hata hivyo zile fedha za kufanyia haya ndio serikali yako imeamua iwanunulie viongozi magari ya kifahari; iwaongezee wabunge mishahara kimono; na hivi karibuni itawagawia wake wa viongozi ambao tayari wanaogelea kwenye utajiri. Fedha nyingine ndio zile zimepigwa kwa mabilioni kwenye report ya kamati ya kudumu ya bunge hesabu za serikali (PAC). Hizi ndio fedha zinazotumika kutengeneza wale vijana mashuhuri unaowaona kule Israel, Singapore, China, Finland, etc. Hawana uchawi wowote Mhe. Rais, wameamua kujali tu.

Nihitimishe Mhe. Rais, hawa maskini ambao leo wanasambazwa kwenye media kama object of mockery kwa taifa hawakuchagua kufanya haya. Nikuone basi, tunapoenda kuwanyanyasa kwa umaskini wao, basi angalau hata tuwatunzie utu wao kwa kuficha sura zao. Kuwapa adhabu ya public shame juu ya mzigo wa umaskini wanaoubeba ni sawa na kuwaua angali bado wapo hai. Na la mwisho, Mhe. Rais, ikikupendeza, basi mwambie mkuu wa Mkoa anapowaambia waondoke na waache kufanya wanachokifanya, basi awaambie pia waende wapi na wakafanye nini kama mbadala wa hiki.

Nakushuru sana kwa muda wako.

Wako
Onesmo Mushi
Ngoja madanguro yafungwe na vibunti vikibakwa na vijana wakiume wakilawitiwa tusisikie mayowe yao. Hii biashara ni kongwe tangu BC imeshindikana kuimaliza wataweza hawa washamba.
 
Huyu raisi analeta mambo ya imani kwenye uongozi jambo ambalo halipaswi kuchanganywa

Hao madada poa sehemu yeyote wapo hata huko wanakoenda kuhiji na kupaona kama sehemu takatifu bado hawakosekani hawa watu.

Alianza kwenye kufungia porn sites na saizi kaja kwenye kubomoa nyumba za wanaojiuza.

Anaweza akawa anafanya jambo zuri kwa imani yake ya kidini lakini likawa na madhara kwa Taifa.

Kama ni jambo zuri kwa dini basi awape suluhu ya kuwawezesha waondokane na hiyo biashara ambayo ni chukizo kwa imani yake.

Na kwakua yeye yupo pale kwa ajili ya Taifa inabidi aangalie kipaumbele cha kwanza ambacho ni Taifa.

Huwezi ukabomoa nyumba za madada poa kisha ukawaacha high way bila kuwapa chochote kama alternative ya kuwafanya wawe na kitu cha kuwaingizia kipato ili wasirudi tena kwenye kazi hiyo.
 
Mushi bana, Usonga hulka mnama

Kwahiyo unaamini waliofeli ndio wanajiuza??

Labda kama umeingia dar leo

Ukahaba ni wa kukemewa uwe wa kiamasikin, kitajiri

Hao wanaolala kwenye hizo gest, hotel ni sehemu private ila Hawa wanaosimama barabarani kama digidig ndioo wa kuwafuta kabisa
 
Bro
Huyu raisi analeta mambo ya imani kwenye uongozi jambo ambalo halipaswi kuchanganywa

Hao madada poa sehemu yeyote wapo hata huko wanakoenda kuhiji na kupaona kama sehemu takatifu bado hawakosekani hawa watu.

Alianza kwenye kufungia porn sites na saizi kaja kwenye kubomoa nyumba za wanaojiuza.

Anaweza akawa anafanya jambo zuri kwa imani yake ya kidini lakini likawa na madhara kwa Taifa.

Kama ni jambo zuri kwa dini basi awape suluhu ya kuwawezesha waondokane na hiyo biashara ambayo ni chukizo kwa imani yake.

Na kwakua yeye yupo pale kwa ajili ya Taifa inabidi aangalie kipaumbele cha kwanza ambacho ni Taifa.

Huwezi ukabomoa nyumba za madada poa kisha ukawaacha high way bila kuwapa chochote kama alternative ya kuwafanya wawe na kitu cha kuwaingizia kipato ili wasirudi tena kwenye kazi hiyo.
Ndg mtamwonea huyo Mama tu

Ukiishi Mtaa wenye danguro utajua kwanini madanguro yanapaswa kuvunjwa vunjwa
 
Bro

Ndg mtamwonea huyo Mama tu

Ukiishi Mtaa wenye danguro utajua kwanini madanguro yanapaswa kuvunjwa vunjwa
Nimeishi mitaa hiyo na sijaona tatizo

Unachokiona wewe kuwa ni tatizo, hakisabanishwi na danguro bali ni malezi mabovu ya wazazi kwa watoto.

Hicho unachotaka kukisema kimesababishwa na danguro utaweza kukikuta hata mitaa ambayo haina madanguro.

Malezi yasiwe kisingizio cha madanguro
 
Nimeishi mitaa hiyo na sijaona tatizo

Unachokiona wewe kuwa ni tatizo, hakisabanishwi na danguro bali ni malezi mabovu ya wazazi kwa watoto.

Hicho unachotaka kukisema kimesababishwa na danguro utaweza kukikuta hata mitaa ambayo haina madanguro.

Malezi yasiwe kisingizio cha madanguro
Basi Madanguro yapewe ulinzi

Sawa Mzee
 
Zanzibar madanguro hamna japo wapo wanaojiuza ila takwimu za matukio ya udhalikishaji ni nyingi kupita kiasi naungana na mdau hapo juu Hawa machangu wakati mwingine wanapunguza haya matukio ya ubakaji kwa watoto.
 
Ndo muoe sasa mshazoea vya kununua na huku mtaani mnajigamba wanawake wamejaa tele, sasa mnacholalamika nini kwa kubomolewa madanguro?na hapo mnasema wanawake ni wengi kuliko wanaume
 
Ndo muoe sasa mshazoea vya kununua na huku mtaani mnajigamba wanawake wamejaa tele, sasa mnacholalamika nini kwa kubomolewa madanguro?na hapo mnasema wanawake ni wengi kuliko wanaume
Wateja wa madanguro wameguswa sehemu za siri 🤣 🤣 🤣 🤣 🤣 🤣 🤣 🤣
 
Ndugu Rais, naamini una uzima wa kutosha asubuhi ya leo. Ukiiangalia video hii kwa haraka haraka utawaona “wahuni” na “watu wasiokuwa na maadili” wakifanya biashara ya “ukahaba.” Lakini ukiangalia kwa umakini, hautowaona wahuni, utaona kundi kubwa la watanzania maskini wanaoishi maisha ya tabu na mateso. Ukiangalia kwa umakini zaidi, utawaona wapiga kura wako ambao umaskini umewalazimisha leo waonekane kama wadhambi kuliko watanzania wote.

Mhe. Rais, kinachofanywa na Mkuu wa Mkoa hapa wala sio kukamata “makahaba” na “kufungia madanguro,” kinachofanyika ni kumdhalilisha maskini kwa sababu ya umaskini wake. Nasema hivi kwa sababu wenzao wanaofanyia “ukahaba” kwenye guest houses za elfu thelathini kule Sinza kuhudumia wateja wa tabaka la kati au wale wanaofanyia kwenye mahoteli yaliyopo ufukweni wakihudumia wateja wa tabaka la wenye nacho, wao hawabughudhiwi. Kwa hiyo hawa kwenye video wanaadhibiwa kwa sababu umaskini wao unaonekana wazi na unawakera viongozi.

Mhe. Rais, usinielewe vibaya. Sipingi kinachofanywa na Mhe. Mkuu wa Mkoa, ila najiuliza, kwa nini viongozi mnakerwa na muonekano wa maisha ya watu wenu lakini hamkerwi na mambo yanayosababisha hawa watu waishi maisha haya? Kwa mujibu wa taasisi ya UNAIDS, Tanzania kuna zaidi ya wanawake 150,000 wanaojihusisha na biashara ya ukahaba. Wametoka wapi wote hawa? Wala usiumize kichwa sana Mhe. Rais, nitakukumbusha. Hawa ndio wale vijana waliomaliza kidato cha nne wakarudi nyumbani bila maarifa yoyote yenye tija. Ndio wale ambao NECTA wanasemaga “asilimia 75% wamepata Division Four na Zero.” Wengine ndio wale waliomaliza vyuo vikuu wakakosa ajira na elimu waliyopewa haijawaandaa kujiajiri, waende wapi? Walio pambana sana ndio wale wamekuwa waendesha bodaboda na wengine mama ntilie, hizo ndio zimekuwa kazi za ndoto zao.

Mhe. Rais, kama hawa wangeweza kupewa mafunzo mbadala, kukuzwa na kuendeleza vipaji vyao, na kukopeshwa mitaji, labda leo wasingekuwa wanatweza utu wao kwa kiwango hiki. Hata hivyo zile fedha za kufanyia haya ndio serikali yako imeamua iwanunulie viongozi magari ya kifahari; iwaongezee wabunge mishahara kimono; na hivi karibuni itawagawia wake wa viongozi ambao tayari wanaogelea kwenye utajiri. Fedha nyingine ndio zile zimepigwa kwa mabilioni kwenye report ya kamati ya kudumu ya bunge hesabu za serikali (PAC). Hizi ndio fedha zinazotumika kutengeneza wale vijana mashuhuri unaowaona kule Israel, Singapore, China, Finland, etc. Hawana uchawi wowote Mhe. Rais, wameamua kujali tu.

Nihitimishe Mhe. Rais, hawa maskini ambao leo wanasambazwa kwenye media kama object of mockery kwa taifa hawakuchagua kufanya haya. Nikuone basi, tunapoenda kuwanyanyasa kwa umaskini wao, basi angalau hata tuwatunzie utu wao kwa kuficha sura zao. Kuwapa adhabu ya public shame juu ya mzigo wa umaskini wanaoubeba ni sawa na kuwaua angali bado wapo hai. Na la mwisho, Mhe. Rais, ikikupendeza, basi mwambie mkuu wa Mkoa anapowaambia waondoke na waache kufanya wanachokifanya, basi awaambie pia waende wapi na wakafanye nini kama mbadala wa hiki.

Nakushuru sana kwa muda wako.

Wako
Onesmo Mushi
biashara ya ukahaba ndiyo biashara kongwe kuliko zote
 
Back
Top Bottom