Herbalist Dr MziziMkavu
JF-Expert Member
- Feb 3, 2009
- 42,318
- 33,125
[h=2][/h]
Waziri wa Ujenzi, Dk. John Magufuli
Baraza la Maadili la Kiislamu Tanzania, limelaani kitendo cha kuzomewa Waziri wa Ujenzi, Dk. John Magufuli, kilichofanywa na baadhi ya wakazi wa Kigamboni, huku likiwaonya pia wabunge wa Mkoa wa Dar es Salaam, kwa kumshambulia waziri huyo, kutokana na uamuzi wake wa kuongeza nauli ya huduma ya kivuko cha Magogoni-Kigamboni.
Tamko hilo lilitolewa na Baraza hilo kupitia Mwenyekiti wake, Sheikh Athuman Mkambaku jana.
Alisema hawana budi kutoa tamko kila wanapoonza maadili yanakiukwa na baadhi ya watu katika jamii, hivyo akasema wakazi hao hawakustahili kumfanyia kitendo hicho Waziri Magufuli kwani uamuzi wake wa kuongeza nauli ya huduma hiyo ulifanywa kwa kuzingatia sheria za nchi.
Hivyo, Baraza linalaani kitendo kilichofanywa na wakazi hao wa Kigamboni wasiostaarabika cha kumzomea Waziri Magufuli, alisema Sheikh Mkambaku.
Alisema Baraza limeridhika na maelezo yaliyotolewa na waziri huyo kuhusu sababu zilizofanya kufikia uamuzi huo, ambazo ni kupanda kwa gharama za uendeshaji, ikiwamo bei ya mafuta.
Sheikh huyo alisema sababu hizo haziwezi kupuuzwa na ndio maana vyombo vyote vya usafiri kuanzia ule wa anga, nchi kavu na majini, vimeongeza nauli na kuhoji iweje leo ionekeane ni ajabu kwa kivuko cha Kigamboni?
Alisema kitendo cha wabunge wa mkoa wa Dar es Salaam kuungana na kumshambulia Wazuiri Magufuli ni cha kinafiki na ajenda ya siri dhidi yake kwa kuwa kuna vitu vingi, ambavyo bei zake imependa Dar es Salaam, kama vile nauli za mabasi ya mikoani, daladala na umeme, lakini hawajaonekana wakiungana na kumshambulia waziri yeyote mwenye dhamana.
Ina maana vitu vyote vilivyopanda bei hapa Dar es Salaam ilikuwa ni sahihi kasoro nauli ya kivuko tu? Maandiko matakaifu yanasema unawezaje kutoa kibanzi katika jicho la mwezio na ile boriti iliyoko katika jicho lake usiitoe? Mnafiki wewe. Alisema Sheikh Mkambaku.
Aliongeza: Kwa mfano, wakazi wa Kiluvya walioko katika Jimbo la Ubungo wanalipa nauli Sh. 900 kutoka Kiluvya hadi Ubungo wakati wakazi wa Mbagala wanalipa Sh 450 kutoka Mbagala hadi Mwenge. Iweje Mbunge wa Ubungo, John Mnyika akawatetee wakazi wa Kigamboni wanaolipa Sh. 200 badala wapigakura wake ambao hulipa Sh 1,200 kutoka Kiluvya hadi Posta. Je, huo sio unafiki?
Alimpongeza Waziri Magufuli kwa uchapakazi hodari unaodhihirisha kwa vitendo kwamba analipenda taifa na kusema laiti kama serikali ingelikuwa na mawaziri watano wachapakazi mfano wake, nchi isingetafunwa na mafisadi, hivyo akawataka Watanzania kumuunga mkono na kumtia moyo badala ya kumkatisha tamaa.
CHANZO: NIPASHE
Waziri wa Ujenzi, Dk. John Magufuli
Baraza la Maadili la Kiislamu Tanzania, limelaani kitendo cha kuzomewa Waziri wa Ujenzi, Dk. John Magufuli, kilichofanywa na baadhi ya wakazi wa Kigamboni, huku likiwaonya pia wabunge wa Mkoa wa Dar es Salaam, kwa kumshambulia waziri huyo, kutokana na uamuzi wake wa kuongeza nauli ya huduma ya kivuko cha Magogoni-Kigamboni.
Tamko hilo lilitolewa na Baraza hilo kupitia Mwenyekiti wake, Sheikh Athuman Mkambaku jana.
Alisema hawana budi kutoa tamko kila wanapoonza maadili yanakiukwa na baadhi ya watu katika jamii, hivyo akasema wakazi hao hawakustahili kumfanyia kitendo hicho Waziri Magufuli kwani uamuzi wake wa kuongeza nauli ya huduma hiyo ulifanywa kwa kuzingatia sheria za nchi.
Hivyo, Baraza linalaani kitendo kilichofanywa na wakazi hao wa Kigamboni wasiostaarabika cha kumzomea Waziri Magufuli, alisema Sheikh Mkambaku.
Alisema Baraza limeridhika na maelezo yaliyotolewa na waziri huyo kuhusu sababu zilizofanya kufikia uamuzi huo, ambazo ni kupanda kwa gharama za uendeshaji, ikiwamo bei ya mafuta.
Sheikh huyo alisema sababu hizo haziwezi kupuuzwa na ndio maana vyombo vyote vya usafiri kuanzia ule wa anga, nchi kavu na majini, vimeongeza nauli na kuhoji iweje leo ionekeane ni ajabu kwa kivuko cha Kigamboni?
Alisema kitendo cha wabunge wa mkoa wa Dar es Salaam kuungana na kumshambulia Wazuiri Magufuli ni cha kinafiki na ajenda ya siri dhidi yake kwa kuwa kuna vitu vingi, ambavyo bei zake imependa Dar es Salaam, kama vile nauli za mabasi ya mikoani, daladala na umeme, lakini hawajaonekana wakiungana na kumshambulia waziri yeyote mwenye dhamana.
Ina maana vitu vyote vilivyopanda bei hapa Dar es Salaam ilikuwa ni sahihi kasoro nauli ya kivuko tu? Maandiko matakaifu yanasema unawezaje kutoa kibanzi katika jicho la mwezio na ile boriti iliyoko katika jicho lake usiitoe? Mnafiki wewe. Alisema Sheikh Mkambaku.
Aliongeza: Kwa mfano, wakazi wa Kiluvya walioko katika Jimbo la Ubungo wanalipa nauli Sh. 900 kutoka Kiluvya hadi Ubungo wakati wakazi wa Mbagala wanalipa Sh 450 kutoka Mbagala hadi Mwenge. Iweje Mbunge wa Ubungo, John Mnyika akawatetee wakazi wa Kigamboni wanaolipa Sh. 200 badala wapigakura wake ambao hulipa Sh 1,200 kutoka Kiluvya hadi Posta. Je, huo sio unafiki?
Alimpongeza Waziri Magufuli kwa uchapakazi hodari unaodhihirisha kwa vitendo kwamba analipenda taifa na kusema laiti kama serikali ingelikuwa na mawaziri watano wachapakazi mfano wake, nchi isingetafunwa na mafisadi, hivyo akawataka Watanzania kumuunga mkono na kumtia moyo badala ya kumkatisha tamaa.
CHANZO: NIPASHE