BigTall
JF-Expert Member
- Mar 9, 2022
- 426
- 1,071
Watu wameshapiga kelele sana kuhusu hii Barabara inayoanzia Kituo cha Sheli kuelekea Muheza hadi Mpiji, sasa hivi magari hayapiti kwa urahisi, yakipita ni kwa tabu na mengine yanakwama.
Bodaboda ndio kila siku watu waanguka kutokana na ubovu wa Barabara.
Tunateseka hivi Mbunge wetu Koka yupo, Mkuu wa Wilaya yupo, Mkuu wa Mkoa na watendaji wengine wapo.
Wakiwa na jambo lao la kukimbiza Mwenge na kuzindua miradi yao mingine ya mchongo wanavizia wakati ambao sio msimu wa mvua, wakijua wataleta katapira litachonga Barabara kisha wao wapite, baada ya hapo ni vumbi.
Ndio maana mimi huwa sina shobo za kwenye kwenye mishe zao kama hizo kwa kuwa najua hakuna cha maana kitakachozungumzwa, ukiwambia kuhusu Barabara wanarukaruka tu, ahadi nyingi hakuna utekelezaji.