Barabara ya tandale inasikitisha

Foundation

JF-Expert Member
Nov 25, 2010
1,421
596
Siku za karibuni nimekuwa nikipita barabara inayounganisha barabara ya Kawawa na bararabara ya Shekilango maarufu kama barabara ya Tandale. Hii barabara imeanza kuharibika kwa kasi sana,ina mashimo mengi,Ikinyesha mvua maji yanajaa barabarani hadi kwenye majumba.
Inakoelekea bararbara hii itakuwa kama ilie ya shekilango ilivyokuwa kero kwa watumiaji wa barabara miaka ya nyuma, kwa juhudi za Lowasa ile barabara ikatengenezwa ( Simpigii debe ila ndio ukweli ) na hadi sasa ni nzuri ingawa huwa inaelemewa na msngamano wa magari.
Najiuliza na majibu sipati, je Mamlaka husika hawajaona huo uharibifu au wanasubiri iharibike kabisa. Mamlaka husika iwe Manispaa ya Kinondoni au TANROAD wafanye utaratibu wa kuifanyia matengenezo ili kuepusha usumbufu wa watumiaji na upotevu wa pesa ya kufanyia ujenzi mpya hapo baadae.
Ukitoa hiyo kero, nashauri serikali ipanue barabara za shekilango na Tandale ili ziweze kumudu ongezeko la watumiaji wa barabara. Kuna msongamano wa Magari huwa unatokea mara kwa mara. Pia itasaidia kupunguza msongamano kwenye bararbara za Kawawa na Morogoro.

Nawasilisha






9









9
 
Siku za karibuni nimekuwa nikipita barabara inayounganisha barabara ya Kawawa na bararabara ya Shekilango maarufu kama barabara ya Tandale. Hii barabara imeanza kuharibika kwa kasi sana,ina mashimo mengi,Ikinyesha mvua maji yanajaa barabarani hadi kwenye majumba.
Inakoelekea bararbara hii itakuwa kama ilie ya shekilango ilivyokuwa kero kwa watumiaji wa barabara miaka ya nyuma, kwa juhudi za Lowasa ile barabara ikatengenezwa ( Simpigii debe ila ndio ukweli ) na hadi sasa ni nzuri ingawa huwa inaelemewa na msngamano wa magari.
Najiuliza na majibu sipati, je Mamlaka husika hawajaona huo uharibifu au wanasubiri iharibike kabisa. Mamlaka husika iwe Manispaa ya Kinondoni au TANROAD wafanye utaratibu wa kuifanyia matengenezo ili kuepusha usumbufu wa watumiaji na upotevu wa pesa ya kufanyia ujenzi mpya hapo baadae.
Ukitoa hiyo kero, nashauri serikali ipanue barabara za shekilango na Tandale ili ziweze kumudu ongezeko la watumiaji wa barabara. Kuna msongamano wa Magari huwa unatokea mara kwa mara. Pia itasaidia kupunguza msongamano kwenye bararbara za Kawawa na Morogoro.

Nawasilisha






9









9

Masahihisho kidogo, haiitwi barabara ya Tandale, inaitwa Barabara ya Uzuri.
Kuhusu kuharibika ni kweli, sehemu ambayo imeharibika sana, mpaka imekuwa kama kipande cha barabara ya vumbi ni pale kuanzia Shule ya Sekondari Manzese mpaka Muhalitani Praimari... Nadhani hatujachelewa sana kumwajibisha mkandarasi kwa kuwa ile barabara hata miaka 10 haina.
 
Masahihisho kidogo, haiitwi barabara ya Tandale, inaitwa Barabara ya Uzuri.
Kuhusu kuharibika ni kweli, sehemu ambayo imeharibika sana, mpaka imekuwa kama kipande cha barabara ya vumbi ni pale kuanzia Shule ya Sekondari Manzese mpaka Muhalitani Praimari... Nadhani hatujachelewa sana kumwajibisha mkandarasi kwa kuwa ile barabara hata miaka 10 haina.

Haa ndo najua leo hilo jina la barabara ya Tandale! Thanks for that mkuu!

Ni kweli ile barabara ikiachwa hivi hivi itaharibika sana na gharama ya matengenezo itakuwa kubwa sana, bora wawahi kurekebisha na gharama inapungua!
 
... Tandale, inaitwa Barabara ya Uzuri... kuanzia Shule ya Sekondari Manzese mpaka Muhalitani Praimari...
Tandale, Uzuri, Sekondari ya Manzese, Muhalitani Primari ....... their thinking is, come on, who cares? The blue blooded class wanakaa Oyster Bay, wanafanya kazi downtown, wanapita Salender Bridge na Toure Drive, barabara yenu isiyo na jina ya kuunganisha kwa Mtogole na kwa Bi Nyau is an afterthought.
 
Aisee nimepita majuzikati, ni aibu. Sijaelewa kwanini haikarabatiwi na kuwekewa vile vimikeka vya kizushi. Hivi kunani mnajenga barabara za lami huko sijui Mbweni sijui wapi wakati hakuna wakazi wa kutosha na wanashindwa kukarabati haka kabarabara ambako nakarahisisha sana mawasiliano kwa wavuja jasho?
 
Masahihisho kidogo, haiitwi barabara ya Tandale, inaitwa Barabara ya Uzuri.
Kuhusu kuharibika ni kweli, sehemu ambayo imeharibika sana, mpaka imekuwa kama kipande cha barabara ya vumbi ni pale kuanzia Shule ya Sekondari Manzese mpaka Muhalitani Praimari... Nadhani hatujachelewa sana kumwajibisha mkandarasi kwa kuwa ile barabara hata miaka 10 haina.

Hiyo sehemu uliyotaja ni pabovu muda mrefu sana, sasa hivi tatizo limeongezeka mpaka maeneo ya Yemeni, Chama na TANESCO
 
Tandale, Uzuri, Sekondari ya Manzese, Muhalitani Primari ....... their thinking is, come on, who cares? The blue blooded class wanakaa Oyster Bay, wanafanya kazi downtown, wanapita Salender Bridge na Toure Drive, barabara yenu isiyo na jina ya kuunganisha kwa Mtogole na kwa Bi Nyau is an afterthought.

hilo nalo neno! Madhila yetu hayawagusi kihivyo kwa kuwa hatuko nao, ipo siku!
 
Aisee nimepita majuzikati, ni aibu. Sijaelewa kwanini haikarabatiwi na kuwekewa vile vimikeka vya kizushi. Hivi kunani mnajenga barabara za lami huko sijui Mbweni sijui wapi wakati hakuna wakazi wa kutosha na wanashindwa kukarabati haka kabarabara ambako nakarahisisha sana mawasiliano kwa wavuja jasho?

nini Mbweni? Sasa hivi Mikocheni ya Regent ina lami karibu yote...
We acha tu yani!
 
Back
Top Bottom