Barabara ya Akachube - Kijitonyama inaharibika hata mwaka bado!!!!

Elisha Ray

JF-Expert Member
Mar 19, 2012
323
94
Wadau, mimi ninasikitika sana na mambo ya ulipuaji katika idara za hii serikali. Hii barabara ya Akachube (inayoanzia kijitonyama off Kajenge road, kuelekea upande wa Mwananyamala) imekwishaanza kuharibika hata kabla ya mwaka kuisha toka ijengwe!! sasa hivi lami yake ina mabonde mabonde na mashimo tayari yameshaanza kutokea. Sijui ni nani wanahusika na mambo ya quality katika idara hizi zinazohusika na barabara au hawaoni/wameuchuna? Barabara ina kiwango cha hali ya chini na kodi zetu ndo zishapotea pale.. Hata barabara ya Sam Nujoma walojenga wachina imeshaaza kuwa na mabonde!!!! Wahusika hawaoni haya mambo? au ndo wamechukua cha juu???
 
Hii barabara imeanza kuharibika toka sehemu gani mpaka wapi?

barabara yote in vibonde vidogo vidogo mwanzo hadi mwisho ingawa vingine havisumbui sana ila ukiwa pale maeneo ya yard ya magari ya Akachube na msikiti kama umetokea Kajenge road kuna mashimo tayari na vibonde vikubwa sana ambavyo ndo vinaelekea kutoa makorongo!!!
 
Baadhi ya watumiaji wa barabara ya Akachube iliyopo Kijitonyama jijini Dar es Salaam wameiomba manispaa ya Kinondoni kuikarabati barabara hiyo ambayo imeharibika vibaya kutokana na mvua zilizopita hali ambayo inasababisha usumbufu mkubwa kwa madereva pamoja na kuhatarisha usalama wao.

Channel ten imetembelea barabara hiyo na kushuhudia mashimo makubwa kwenye barabara hiyo huku magari ,pikipiki na bajaji zikipita kwa shida kutokana na jitihada za madereva kukwepa mashimo hayo.
Hawa ni baadhi ya watumiaji wa barabara hiyo kama wanavyoelezea.


Mvua za msimu zilizonyesha hivi karibuni zimeathiri barabara nyingi katika jiji la Dar es Salaam ikiwemo barabara ya Akachube hivyo kusababisha kero kubwa kwa wakazi wa jiji hususan madereva wa vyombo vya moto

Chanzo:
Channel Ten
 
Wadau, mimi ninasikitika sana na mambo ya ulipuaji katika idara za hii serikali. Hii barabara ya Akachube (inayoanzia kijitonyama off Kajenge road, kuelekea upande wa Mwananyamala) imekwishaanza kuharibika hata kabla ya mwaka kuisha toka ijengwe!! sasa hivi lami yake ina mabonde mabonde na mashimo tayari yameshaanza kutokea. Sijui ni nani wanahusika na mambo ya quality katika idara hizi zinazohusika na barabara au hawaoni/wameuchuna? Barabara ina kiwango cha hali ya chini na kodi zetu ndo zishapotea pale.. Hata barabara ya Sam Nujoma walojenga wachina imeshaaza kuwa na mabonde!!!! Wahusika hawaoni haya mambo? au ndo wamechukua cha juu???


...........wameyataka wenyewe.........CCM ni ile ile oooooh!ni ile ile mbele kwa mbele mpaka kuzimu.
 
Back
Top Bottom