Bandari: Ukweli ni Kwamba, CCM Imetupotosha Kupitia Bunge Lake!

voicer

JF-Expert Member
Jul 13, 2020
5,553
11,885




Angalieni pia hizo video clips!
Kwanza ieleweke kwamba watanzania hawapingi uwekezaji wenye tija,ambao ni Win- Win situation!
Uwekezaji wa miundombinu na teknolojia kwenye miradi kama bandari kuu.Ni suala muhimu sana!hasa katika Dunia ya sasa ambapo mambo yanaenda kwa kasi sana!
Tunachokipigia kelele watanzania ni
"Aina ya mkataba na vifungu vyake tata na vya kinyonyaji!"

Wabunge badala ya kuongelea vifungu vya mkataba, wao walijikita kuongelea teknolojia ya Bandari!

Watanzania jana tulishuhudia "Uhuni" wa wanaojiita "waheshimiwa" ndani ya Jengo la bunge letu.
Badala ya kujadili hoja iliyokuwa mezani, wao waliingia kuipigia upatu.Ni wazi maamuzi walikwisha yaamua huko kwenye vikao vya "Party caucus" vilivyofanyika mfululizo tangia siku ya Alhamisi/Ijumaa hadi usiku.

Ni kwa mara ya kwanza katika historia ya nchi hii,ambapo spika amelazimika kumsimamisha mbunge ili afunguwe bahasha kuepuka tuhuma za rushwa ndani ya bunge!

Hii ni baada ya tukio la kuonekana wakipewa bahasha mfululizo huku mjadala ukiendelea ndani ya bunge la CCM.

Kituko kikuu:
Wabunge wote walijikita kuutolea sifa mkataba na faida zake, bila kutaja vielelezo vyake!
Kwa ujumla wabunge waligeuka makuwadi wa madalali wa Deep world
(DP- world).

Shame on all of waheshimiwa......nikianza na Mwita Waitara,Nape Nnauye,Jerry Slaa,Dk Mollel na wenzao woote waliotumia muda wa serikali kushambulia watu binafsi.
Ila waelewe jana sio leo,watanzania wanazidi kujitambua kila uchao!

My Take:
Ni wakati sahihi kuwaonyesha watawala na CCM yao kwamba wananchi wanapaswa kusikilizwa na kupewa kipaumbele!

Pale linapokuja suala nyeti kama hili la ubinafsishaji wa Bandari zetu.

Wabunge hata wameshindwa kututoa hofu WANANCHI ni kwa nini mkataba huu umeletwa kwa njia ya zimamoto,tena siku ambayo siyo ya kazi kwa mujibu wa sheria na katiba ya nchi hii.

Hao wanaoitwa wadau 76 waliofika Dodoma kutoa maoni kwenye kamati ya pamoja ni kina nani.

Na je!

Ni asilimia ngapi ya idadi ya watanzania milioni 60?

Ukweli ni kwamba bunge limetumika kama "Muhuri" tu!

Maamuzi yamekwishqfanyika siku nyingi.

Na hivyo nimeamini kwamba ninaishi Jaa-mihuri ya TANZANIA.

AHSANTENI na Jumapili njema!
 
Bunge limechaguliwa na wananchi ndo wakilishi wa raia haiwezekani kuuliza raia moja moja, inatubidi tukubaliane na matokeo, kwasbb mda wote hatujawahi kupinga bunge kwamba sio wakilishi wetu sahihi.
 
Bunge limechaguliwa na wananchi ndo wakilishi wa raia haiwezekani kuuliza raia moja moja, inatubidi tukubaliane na matokeo, kwasbb mda wote hatujawahi kupinga bunge kwamba sio wakilishi wetu sahihi.
Eti watu 76 kufika Dodoma kwa dharula,wakati issue inahusu maamuzi ya karne!
Maajabu makubwa haya!
 
Eti watu 76 kufika Dodoma kwa dharula,wakati issue inahusu maamuzi ya karne!
Maajabu makubwa haya!
Ndo bunge linavyofanya kazi wote hawawezi kujitokeza wengine wanakua na kazi maalumu uko majimboni au nje ya nchi, huo ndo mfumo tulio pokea siku zote, na hamna mtanzania alijitokeza kupinga bunge hilo tangu lichaguliwe na mwendazake.
 
Unamaliza mb zetu alafu kumbe hata huo mkataba hujausomi na huujui. Chiz kabisa wewe. Umepotoshwa nini wakati hata mkataba hujausoma?
Mimi sio kilaza kama wewe!
Mimi sio mchumia tumbo kama wewe na ukoo wako!
Mimi sijashikiwa akili kama wewe!
Mimi nawaza nje ya Boksi!

Mkataba huo au makubaliano hayo,pamoja na mimi kuwa nao,lakini pia hata ukiingia youtube au ukisikiliza bunge kikao cha jana utaelewa!

Ndio maana nimeweka video clips hizi
 
Ndo bunge linavo fanya kazi wote hawawezi kujitokeza wengine wanakua na kazi maalumu uko majimboni au nje ya nchi, huo ndo mfumo tulio pokea siku zote, na hamna mtanzania alijitokeza kupinga bunge hilo tangu lichaguliwe na mwendazake.
Unachoongea na ninachoongea ni vitu viwili tofauti.

Wewe unaongelea bunge mimi ninaongelea wadau au watanzania waliofika Dodoma ili kutoa maoni yao mbele ya kamati jumuishi.

Ilipaswa kutoa muda ili hiyo kamati ndio izunguke nchi nzima kukusanya maoni toka kwa wananchi.

Usikurupuke ku comment opposite kabla ya kuelewa jambo husika
 
Watanzania jana tulishuhudia "Uhuni" wa wanaojiita "waheshimiwa" ndani ya Jengo la bunge letu.
Badala ya kujadili hoja iliyokuwa mezani, wao waliingia kuipigia upatu.Ni wazi maamuzi walikwisha yaamua huko kwenye vikao vya "Party caucus" vilivyofanyika mfululizo tangia siku ya Alhamisi/Ijumaa hadi usiku.
Tukisema hii ngoma ishamalizwa kitambo pale ilikua geresha wanatutukana!!
 
Wewe Popoma tulia kazi iendelee🐒🐒🐒
AAPP0t.jpeg
 
Nimesoma na nimejiridhisha mkataba uko sawa kabisa
Una kichwa kigumu kama jiwe 🤓 unaelekezwa wewe unakomaa umesoma mkataba?

Wewe ulie soma tueleweshe basi kuliko kukomalia hii pointless yako...............

"IF YOU WILL USE THIS ENERGY FOR YOUR LIFE, THEN YOU WILL NOT BEGGING FOR FOOD"
 
Mkuu na kuelewa vizuri ila ilifanywa sampling wa chache kwa niamba ya wengi kwasbb haikua referendum au kula ya maoni.
Wakati wewe unaongelea "Kula"... kura ya maoni na mimi naongelea"maoni ya wadau "
Je!
Ni sahihi kwa watu 76 kutoa maoni na kuwakilisha watu milioni 60?
 
Kuna maswali mengi kuhusu huu ubinafishaji wa Bandari.
Mbona shughuli kubwa kama hii inasukumwa ikamilike haraka haraka? Nani anatupelekesha? Ni bosi wa nje au wa ndani?
Mbona mambo mengine muhimu yamerukwa? Kmf.ushindani wa Bandari ametaja Mombasa na Durban tu. Bandari ya Lamu, Kenya haikutajwa. Hii inajengwa na Kenya, Ethiopia na Sudan Kusn.Imeanza kufanya kazi na itakuwa kubwa kama Bandari ya Mombasa na Lamu in sifa za ziada.
Kusema meli za watalii zitakuja kwa wingi kuliko sasa haina ukweli, ni kupamba tu.
Kusema tehama ya kisasa itatumika na ajira zitaongezeka ni kukinzana. Tehama kama hiyo lengo ni kupunguza gharama ikiwemo gharama za waajiriwa.
Tehama DP -World Sio ya kipekee na tehama mpya zinatoka kila mwaka. Hivyo kuwafundisha watz tehama Sio 'big deal'.
Kwa nini Watanzania matajiri na masikini kupitia mifuko yao ya pamoja hawapewi fursa ya kuwekeza kwenye mradi huo kama alivyofanya Margaret Thatcher wa Uingereza alipobinafisha kila shirika?
Je Tz imeamua kunzisha 'monopolies' nchini?
Watumishi wa TPA wanastahili kuheshimiwa - chanzo cha tatizo sio wao.
Mwisho tungekuwa na demokrasya ya kweli ungeitishwa uchaguzi mkuu mara moja.
 
Kuna maswali mengi kuhusu huu ubinafishaji wa Bandari.
Mbona shughuli kubwa kama hii inasukumwa ikamilike haraka haraka? Nani anatupelekesha? Ni bosi wa nje au wa ndani?
Mbona mambo mengine muhimu yamerukwa? Kmf.ushindani wa Bandari ametaja Mombasa na Durban tu. Bandari ya Lamu, Kenya haikutajwa. Hii inajengwa na Kenya, Ethiopia na Sudan Kusn.Imeanza kufanya kazi na itakuwa kubwa kama Bandari ya Mombasa na Lamu in sifa za ziada.
Kusema meli za watalii zitakuja kwa wingi kuliko sasa haina ukweli, ni kupamba tu.
Kusema tehama ya kisasa itatumika na ajira zitaongezeka ni kukinzana. Tehama kama hiyo lengo ni kupunguza gharama ikiwemo gharama za waajiriwa.
Tehama DP -World Sio ya kipekee na tehama mpya zinatoka kila mwaka. Hivyo kuwafundisha watz tehama Sio 'big deal'.
Kwa nini Watanzania matajiri na masikini kupitia mifuko yao ya pamoja hawapewi fursa ya kuwekeza kwenye mradi huo kama alivyofanya Margaret Thatcher wa Uingereza alipobinafisha kila shirika?
Je Tz imeamua kunzisha 'monopolies' nchini?
Watumishi wa TPA wanastahili kuhedhimiwa - chanzo cha tatizo sio wao.
Mwisho tungekuwa na demokrasya ya kweli ungeitishwa uchaguzi mkuu mara moja.
Wewe ulitaka ichukue mda gani kwa mfano? Nchi inahitaji pesa kuhudumia watu wake kwanini tusubiri wakati kila kitu kiko menzani tangu 2021
 
Kuna maswali mengi kuhusu huu ubinafishaji wa Bandari.
Mbona shughuli kubwa kama hii inasukumwa ikamilike haraka haraka? Nani anatupelekesha? Ni bosi wa nje au wa ndani?
Mbona mambo mengine muhimu yamerukwa? Kmf.ushindani wa Bandari ametaja Mombasa na Durban tu. Bandari ya Lamu, Kenya haikutajwa. Hii inajengwa na Kenya, Ethiopia na Sudan Kusn.Imeanza kufanya kazi na otakuwa kubwa kama Bandari ya Mombasa na Lamu on sifa za ziada.
Kusema meli za watalii zitakuja kwa wingi kuliko sasa haina ukweli, ni kupamba tu.
Kusema tehama ya kisasa itatumika na Akira zitaongezeka ni kukinzana. Tehama sina hiyo lengo ni kupunguza gharama ikiwemo gharama za waajiriwa.
Tehama Yao Sio ya kipekee na tehama mpya zinatoka kila mwaka. Hivyo kuwafundisha watz tehama Sio 'big deal'.
Kwa Nini Watanzania matajiri na masikini kupitia mifuko Yao ya pamoja hawapewi fursa ya kuwekeza kwenye mradi huko kama alivyofanya Margaret Thatcher sa Uingereza alipobinafisha kila shirika?
Je Tz imeamua kunzisha 'monopolies' nchini?
Watumishi wa TPA wanastahili kuheshimiwa - chanzo cha tatizo sio wao.
Mwisho tungekuwa na demokrasya ya kweli ungeitishwa uchaguzi mkuu mara moja.
 
Back
Top Bottom