Bado nina mashaka kuhusu kitabu hiki cha Biblia

Tunaogopa tu miaka ya 2500 huko wasije wakaandika kitabu kuwa kulikuwa na nabii akiitwa Spider man alikuwa anaruka kwenye maghorofa.
Kutakuwa na kitabu kinachoelezea manabii kama super man, wonder woman, the flash, hulk, captain america, iron man, huku taifa la USA litatajwa kama Taifa teule, na uhakika kizazi kijacho kitaaminishwa haya mambo, huku movies za hollywood zikiwa kama refference ya watu kuamini hayo mapokeo na sehem zao ibada itakuwa kumbi za starehe za viwanja vya maonesho ya sinema kama theaters.

Dini ni michezo ya akili ambayo kila nyakat huibuka na stories za kusadikika kuwaaminisha watu uongo
 
Wewe una matatizo,kivyovyote vile wewe ni mhaya.
Una kiburi lakini kiburi chenyewe kinatokana na uwelewa mdogo wa mambo

Unajadili Biblia ukilinganisha tafsiri za kimadhehebu na unasumbuliwa na Doctrines.

Mimi nafikiri usingekosoa Bible badala yake ungejikosoa wewe mwenyewe kutokana na kutokujua misingi ya neno la Mungu na zaidi ya yote Roho Mtakatifu ndio anayepaswa kuwa Mwalimu wako

Tafsiri ya pombe na mvinyo ndio inakusumbua?mbona hayo ni mepesi sana?

Dunia imeshuhudia masayantisti wakubwa na mafilosofa waliokuwa na mawazo ya kijinga kama wewe hapo lakini mwisho wa uhai wao waliandika vitabu na kutoa ushuhuda juu ya Biblia.

Uwe mwanafunzi wa Biblia
Acha kukimbilia huko
Jifunze maandiko na uwe mwanafunzi mzuri.

Achana na mapokeo na ushindani wa kimadhehebu
 
Watakambia hauna imani. Yaani kicho kitabu huwa kinabadilishwa na watu kwa jinsi wanavyojisikia wao. Kuna mzungu mmoja ni Proffesa anaitwa Paul William kutoka UK na yeye aliishia kusilimu baada ya kuona mikanganyiko katika Bible. Badae alikuja kusoma Quran akaona ipo straight na haina mikanganyiko. Huyo hapo mcheki


View: https://youtu.be/0zZUEgtBGjY?si=dvoQ9i6z5250YbK9
 
Walokole wanakatazwa kunywa pombe na wachungaji wao ili ile fedha ikatolewe sadaka na iwafaidishe hao wachungaji.

Kula kupita kiasi ni ulafi.
Kunywa kupita kiasi ni ulevi.
Hivi ndivyo chimbuko la dhambi.
Kila kitu fanya kwa kiasi.

Vinywaji vingi vina kilevi ila hutofautiana tu kiwango. Kama utatafsiri kuwa pombe hubebwa kilevi, basi, kunywa tu maji.

Wema huwa unajulikana na ubaya hujulikana pia. Angalia mwenendo wako na uubadili pale pasipofaa. Ukisubiri kila kitu uelewekezwa utaishia kutapeliwa na hawa viongozi wa dini.

Kupanga ni kuchagua.

God needs us to be Spiritual and not Religious ones.
 
Pole sana ndugu yangu!!, kabla ya yote ningependa kujua kama umempa Bwana Yesu Kristo na umebatizwa ubatizo sahihi??

Well kama bado unaweza ni dm nikakupa mwongozo wote.

Biblia haijichanganyi wala haijipinhi na haitakaa ijipinge kamwe!, ila akili zetu sisi ndio zinapingana na biblia na ndio maana tunaona huku ni tofauti na kule ni tofauti,

Haya yote Bwana Yesu aliyatambua na ndio maana wakati ule anatwaliwa kwenda mbinguni aliwaambia mitume kwamba "ninaenda kwa Baba ila sitawaacha yatima" na kuondoka kwa Yesu ndio kulileta Msaidizi yaani Roho Mtakatifu ndio maana akasema "huyo msaidizi atakapokuja atatwaa yaliyo yangu na kuwapasha ninyi Habari " maana yake yale yote tusiyoyaelewa Roho Mtakatifu yuko kuyusaidia kuyaelewa.

Hakuna binadamu yeyote anaeweza kuielewa jiblia pasipokuwa na Roho Mtakatifu never ever, maana biblia ni neno la Mungu maana yake ni Mungu mwenyewe au (wazo la Mungu), maana yake hakuna yeyote anaeeza kulielewa wazo la Mungu isipokuwa yeye mwenyewe aamue kukufunulia, yaani hakuna mtu awezae kuyajua mawazo yako wewe pasipo kumwambia, wazo lako. Na ndio maana utaona Yesu kuna muda alikuwa anazungumza kwa mifano wanafunzi wanashindwa kuelewa pamoja na makutano na mafarisayo waandishi,makuhani na wanasheria hawakuwa wanaelewa ile mifano mpaka Wanafunzi wanamfuata Bwana Yesu awafafanulie mifano ile ilikuwa na maana gani(kama ni mtu smart na unatamani kujua kweli nafikili kuna kitu utakuwa uanaanza ku gain).

Ukishindwa kulielewa agano na kale itakuwa ngumu kulielewa agano jipya, ni lazima ujue agano la kale vizuri na kisha utaelewa kuwa kumbe agano la kale ni kivuri cha agano jipya soma Waebrania 11 yote utapata jambo hapo, kwahiyo kitu halisi ndicho hichi kilicho katika agano jipya na agano la kale lilikuwa likifunua agano jipya na ndio maana Yesu kuna mahali anasema "MLISIKIA IMENENWA" maana yake nini?? Inabidi tuelewee agano la kale lilikuwa kwa jinsi ya mwilini na agano jipya ni rohoni hii kumaanisha Mungu alianza kujenga msingi kabla

Ni kama mtoto mdogo huwezi ukaanza kumfundisha hesabu za kuzidisha kabla hata hajajua moja ni nini na mbili ni nini na inaandikwaje nk itakuwa ni mafumbo kwa yule mtoto na hatakuelewa.

Lakini ukianza nae kwa hesabu za kujumlisha tena kwa kutumia mawe na kutoa kwa kutumia mawe au vijiti utaona itakuwa ni rahisi kwa yule mtoto hata akienda kufanya hesabu za magazi juto haitakuwa mafumbo kwake.
 
Waefeso 5:18 "Tena msilewe kwa mvinyo, ambamo mna ufisadi; bali mjazwe Roho;"

Kumbe ndani ya mvinyo/pombe kuna ufisadi na ndio maana leo ukinywa pombe ni rahisi wewe kufanya jambo lolote baya, utataka kuzini nk,

Soma
Matendo ya mitume 2:1-47 utaona ni mvinyo gani unaozungumziwa, mvinyo tunatakiwa kulewa nao ni mmoja tu nao ni ROHO MTAKATIFU basi hakuna mwingine,

Lakini ukitaka biblia tukiifuata kwa akili zetu tutapotea pasipo Roho Mtakatifu hatutaweza kitu ndio maana Yesu anasem "Hamwezi jambo lolote pasipo mimi."

Na ndio maana Yesu anasema katika kile kitabu cha Luka "mtu atakae kunifuata ajikane nafsi yake na ajitwike msalaba wake"

Maana yake kujikana nafsi ni kuachana na mambo yote yale unayoyapenda na ni machukizo mbele za Bwana unaviacha kwa sababu unataka kuiponya Roho yako

MUNGU KUTWAMBIA TUSITENDE DHAMBI AU TUSINYWE POMBE,KUVUTA SIGARA NK SIO KWAMBA ANATUONEA WIVU ILA NI KWA FAIDA YETU.

Mpe Kristo maisha yako tuko nje ya Muda kama hulioni hili kasome Mathayo 24 utajionea mwenyewe ni wakati mchache sana

Biblia inasema "Shangwe ya waovu ni ya kitambo tu" fikilia leo kugeuka kesho au leo unaweza kuondoka lakini je umejiuliza hili swali "UTAELEKEA WAPI??, UTAKUWA MGENI WA NANI? na je UMEJIANDAAAA??" make a choice today anyone who read this post REPENT your sin.
 
Labda nina ufinyu wa fikra au ujinga wangu umefunika. Lakini mjinga kugundua na kukubali ujinga wake si ni hatua ya mwanzo ya kuacha ujinga na kuerevuka?

Nasema hivi kwa sababu sielewi, hivi, mtu anaposema Ukristo au Uislamu huwa anamaanisha nini? Je, kama Wapentekoste ni Wakristo, Wakatoliki nao ni Wakristo?

Mfano ; Wakatoliki wanaamini ubatizo wa mtoto mdogo na Kristo ndiye anawaongoza kufanya hivyo wakati Wapentekoste wanaamini ubatizo ni kwa mtu wazima tu tena kwa kuzamishwa ndani ya maji mengi kama alivyobatizwa Yesu (mwasisi wa Ukristo) katika mto Jordan.

Sasa inawezekana ukatoliki ni upentekoste vikawa ni Ukristo kweli?

Je, wale Wa-Adventista Wasabato wanaoamini kuwa siku takatifu ya ibada ni Jumamosi tu ni Wakristo sawa na Walutheri wanaoabudu siku ya Jumapili?

Je, Mashahidi wa Yehova wasioamini utatu mtakatifu kuwa ni Mungu Baba, Mungu Mwana na Roho Mtakatifu ni sawa na wanaoamini utatu mtakatifu kama mafundisho ya kweli ya Biblia?

Kama wote ni Wakristo, kwa nini wengine waamini kuwa Yesu ni mwana wa Mungu na wengine wadai Yesu ni Mungu? Kwa nini wengine waamini Yesu alitumwa duniani kuwaokoa wanadamu na wengine waamini alijituma binafsi kumwokoa mwanadamu aliyepotea?

Inawezekana vipi mitizamo hii miwili inayokinzana yote kuwa ya Kikristo ilhali wote wakitumia msaafu wa Biblia?

Yapo madhehebu yanayoruhusu wanawake kuwa wachungaji, wainjilisti, wahubiri: yapo mengine yanayokataza, yapo madhehebu yanayoruhusu ndoa za jinsia moja lakini wote wanapunga mapepo kwa jina la Yesu Kristo, Je, huyo Kristo hana falsafa moja inayoongoza dini yake?

Kama ndio hivyo,neno “Ukristo” linaweza kuwa na maana moja huku wafuasi wake wakitofautiana kiteolojia, kifalsafa, matendo, tambiko na tafsiri ya maandiko?

Leo kila kona ya nchi yetu hasa maeneo yenye mwamko wa kiuchumi kumeoteshwa madhehebu lukuki kila moja ikiwa na staili yake ya kuwahadaa wafuasi wake kwa jina la Yesu Kristo.
 
Labda nina ufinyu wa fikra au ujinga wangu umefunika. Lakini mjinga kugundua na kukubali ujinga wake si ni hatua ya mwanzo ya kuacha ujinga na kuerevuka?

Nasema hivi kwa sababu sielewi, hivi, mtu anaposema Ukristo au Uislamu huwa anamaanisha nini? Je, kama Wapentekoste ni Wakristo, Wakatoliki nao ni Wakristo?

Mfano ; Wakatoliki wanaamini ubatizo wa mtoto mdogo na Kristo ndiye anawaongoza kufanya hivyo wakati Wapentekoste wanaamini ubatizo ni kwa mtu wazima tu tena kwa kuzamishwa ndani ya maji mengi kama alivyobatizwa Yesu (mwasisi wa Ukristo) katika mto Jordan.

Sasa inawezekana ukatoliki ni upentekoste vikawa ni Ukristo kweli?

Je, wale Wa-Adventista Wasabato wanaoamini kuwa siku takatifu ya ibada ni Jumamosi tu ni Wakristo sawa na Walutheri wanaoabudu siku ya Jumapili?

Je, Mashahidi wa Yehova wasioamini utatu mtakatifu kuwa ni Mungu Baba, Mungu Mwana na Roho Mtakatifu ni sawa na wanaoamini utatu mtakatifu kama mafundisho ya kweli ya Biblia?

Kama wote ni Wakristo, kwa nini wengine waamini kuwa Yesu ni mwana wa Mungu na wengine wadai Yesu ni Mungu? Kwa nini wengine waamini Yesu alitumwa duniani kuwaokoa wanadamu na wengine waamini alijituma binafsi kumwokoa mwanadamu aliyepotea?

Inawezekana vipi mitizamo hii miwili inayokinzana yote kuwa ya Kikristo ilhali wote wakitumia msaafu wa Biblia?

Yapo madhehebu yanayoruhusu wanawake kuwa wachungaji, wainjilisti, wahubiri: yapo mengine yanayokataza, yapo madhehebu yanayoruhusu ndoa za jinsia moja lakini wote wanapunga mapepo kwa jina la Yesu Kristo, Je, huyo Kristo hana falsafa moja inayoongoza dini yake?

Kama ndio hivyo,neno “Ukristo” linaweza kuwa na maana moja huku wafuasi wake wakitofautiana kiteolojia, kifalsafa, matendo, tambiko na tafsiri ya maandiko?

Leo kila kona ya nchi yetu hasa maeneo yenye mwamko wa kiuchumi kumeoteshwa madhehebu lukuki kila moja ikiwa na staili yake ya kuwahadaa wafuasi wake kwa jina la Yesu Kristo.
Nimejifunza muda mrefu sana kuhusu madhehebu ya kikristo lakini Kila dhehebu linakuwa kivyake na lijiongoza kivyake ukiuliza unaambiwa imeandikwa inanipa ugumu sana kuielewa hiki kitabu Cha biblia Ina maana hakuna mwongozo mmoja Kwa dini zote!
Kwa mfano kuhusu ubatizo pale Kenya Kuna makanisa yanabatiza Kwa kunywa supu ya kondoo
Mengine kuruka moto ubatizo ulio niacha hoi ni ubatizo wa Tone la mkojo wa mchungaji!! Bado sijapata majibu acha kwanza niwe mpagani
 
Nimeshuhudia vyakula vikiwapa watu ulemavu wa kudumu kama KISUKARI, PRESURE, SHINIKIZO LA MOYO, KIRUBA TUMBO, FIGO n.k

Mavyakula kama Bugger, pizza, mavyakula ya sukari sana, UNYWAJIBWA MASODA, MAJUICE YA SUKARI yamewapa watu matatizo makubwa na wengi wamepoteza maisha, tunaona saiv kijana miaka 30 ana tumbo kama kifutu, akiumwa utasikia ana presha, kisukari, sio pombe bali mavyakula.

We umeona pombe tu,
Kwa sababu pombe ndo imeandikwa hizo burger au chips sijawahi kuona kama zimekatazwa au kukubaliwa. Ahsantee
 
Je, unaelewa Yesu kwanini alikufa?

Agano 1 - TORATI
Agano 2 - Neema na Kweli

Leo hii Tupo agano la 2, soma zaidi kuhúsu Kristo Yesu.

Hauzuiliwi na chochote, kuwa huru kufanya chochote.

Kwani umeokolewa bure kabisa, huna ulicho changia na hauwezi kuchangia wokovu. Wewe amini aliye kuokoa.
 
Je, unaelewa Yesu kwanini alikufa?

Agano 1 - TORATI
Agano 2 - Neema na Kweli

Leo hii Tupo agano la 2, soma zaidi kuhúsu Kristo Yesu.

Hauzuiliwi na chochote, kuwa huru kufanya chochote.

Kwani umeokolewa bure kabisa, huna ulicho changia na hauwezi kuchangia wokovu. Wewe amini aliye kuokoa.
"Fanya chochote" ukiwa unamanisha hata kuua,kuzini kufanya lolote kisa huchangaia kitu katika wokuvu!?

Inamaana Agano la kale hamlitaki Tena? Ndo nazidi kutokuelewana zaidi Kwa maana hata Amri kumi.zipo agano la kale manake tuachane nazo?
 
"Fanya chochote" ukiwa unamanisha hata kuua,kuzini kufanya lolote kisa huchangaia kitu katika wokuvu!?

Inamaana Agano la kale hamlitaki Tena? Ndo nazidi kutokuelewana zaidi Kwa maana hata Amri kumi.zipo agano la kale manake tuachane nazo?
Jibu swali kwanza, unaelewa Yesu kwanini alikufa?
 
Je, unaelewa Yesu kwanini alikufa?

Agano 1 - TORATI
Agano 2 - Neema na Kweli

Leo hii Tupo agano la 2, soma zaidi kuhúsu Kristo Yesu.

Hauzuiliwi na chochote, kuwa huru kufanya chochote.

Kwani umeokolewa bure kabisa, huna ulicho changia na hauwezi kuchangia wokovu. Wewe amini aliye kuokoa.
Umeokolewa nini? Umeokolewa wapi? Kwanini uokolewe na nani alikuingiza huko mpaka uje uokolewe? Ninani aliesababisha wewe kuhitaji kuokolewa? Au yesu yupo kama wamarekani anakugonga kwanza vita anahakikisha njaa inawashika vyema then analeta misaaada anatangaza kuwa nimewaokoa, kwahyo yesu alituletea shetan duniani jamaa akatupaka madhambi weeee then yesu akashuka akampiga,sijui katupa silaha then kasema katuokoa, huyu yesu nimsanii sanii pia kama ni hivyo, kama utapinga hoja yangu utatuambia sasa, kwann atuokoe amekuokoa na nn amekuokolea wapi na kwann?
 
Umeokolewa nini?
Je wewe ni mtu wa mataifa(yani tofauti na taifa la Mungu) au wewe ni mmoja wa kabila 12 za Israel...

Kama wewe ni mtu wa mataifa(yani waliokuwa hawana Mungu au wanaabudu kisicho julikana):
  • Umeokolewa kutoka huko mwanzo ambapo hukuwa na Mungu. Mpaka leo watu wa Mataifa wanamjua Mungu kwa sababu hiyo.
  • Hapo mwanzo taifa la Mungu na watu wa Mataifa walikuwa hawachangamani(utengano) mfano Kutokuoana, Hivyo Yesu alitoa hicho kilichokuwa kinatutenganisha na hivyo kutufunya kuwa wamoja.
Soma waefeso 2 : 11 - 22.

Kama wewe ni mmoja wa wana wa Israel umeokolewa kutoka katika dhambi na Leo huna dhambi wala huwezi kutenda dhambi kwa sababu kilichokuwa kinakufanya utende dhambi kiondolewa.
Mathayo 26:28
kwa maana hii ndiyo damu yangu ya agano, imwagikayo kwa ajili ya wengi kwa ondoleo la dhambi.

Cha kuongozea, hauhitaji kufanya mchango wowote ili uokolewe bali umeokolewa kwa Neema.(waefeso 2 :8-10)

Kwanini uokolewe na nani alikuingiza huko mpaka uje uokolewe? Ninani aliesababisha wewe kuhitaji kuokolewa?
Uliokolewa kwa sababu Mungu alikupenda hakutaka uangamie yani Ufe bali aliamua akupe uzima wa milele.
Yohana 3 : 16-17

Dhambi ndio ilisababisha wewe kuhitaji kuokolewa

kwann atuokoe amekuokoa na nn amekuokolea wapi na kwann?
Bila shaka nimejibu.

Kibwagizo:
Luka 18:16-17
Bali Yesu akawaita waje kwake, akasema, Waacheni watoto wadogo waje kwangu, wala msiwazuie, kwa kuwa watu kama hao ufalme wa Mungu ni wao.
Amin, nawaambia, Mtu ye yote asiyeupokea ufalme wa Mungu kama mtoto mdogo hauingii kamwe.

Kristo Yesu awe nawe.
 
Back
Top Bottom