Mediaman,
Mungu ni mmoja. Unataka amtaje Yesu ili iweje? Yeye amesema ameoteshwa na Mungu. Mungu alimuumba mwanadamu kwa mfano wake. Kutokana na kutenda dhambi Mungu alimtuma mwokozi Yesu ili aje kuwaepusha wanadamu na dhambi. Naam, vivyo hivyo Mungu alipoona binaadamu wanateswa na magonjwa na kwa kuwa Yesu alikufa na kufufuka na kupaa mbinguni na kuwa atakuja tena siku ya hukumu kuwahukumu wazima na wafu... akamtokea Ambilikile Mwasapile kule Samunge na kumpa maono ni jinsi gani anaweza kuwaponya wanadamu na magonjwa sugu yanayowasumbua.
Kwa hivyo basi, Yesu kazi yake kubwa ilikuwa ni kuwaokoa wanadamu dhidi ya dhambi. Ambilikile Mwasapile kazi yake ni kuwaponya wanadamu dhidi ya magonjwa yanayowasumbua. Kwanini basi usiamini kuwa kila mmoja ana kazi yake aliyotumwa na Mungu?
Ukuweza kwenda kwa Ambilikile Mwasapile ukapona maradhi yako na ukamfuata Yesu ukaacha dhambi zako utauona ufalme wa mbinguni siku Yesu atakapokuja kutoa hukumu.
Kumtibu mtu kwa kutumia jina la Yesu kwangu naona sio sahihi. Kwa kuwa Yesu kazi yake ni kukuondolea dhambi na magonjwa sio dhambi...
Elewa hivyo katika jina la Mungu.
Si vizuri kupotosha maneno ya Mungu. Soma injili utaona Yesu alisema nini kuhusu dhambi, alipomwambia yule mgonjwa 'Nenda umesamehewa dhambi zako' Waliokuwepo wakakwazika akawauliza mnashangaa nini? Je hamjui kuwa mwana wa Adamu aweza kusamehe dhambi? Je ni kipi rahisi kusema umesamehwewa dhambi zako au enenda umepona? Hapo alikuwa anamaanisha nini? Go back to Genesis; kabla ya anguko la mwandamu hakukuwa na ugonjwa wala kifo kwani roho ya Mungu ilikuwa ndani ya mwanadamu. Alipokosa utii dhambi (roho ya Ibilisi) iliingia ndani yake na roho ya Mungu ikaondoka na ndipo magonjwa adha na shida yakwa ndiyo matunda ya kazi ya roho ya Ibilisi ndani yake. Bila dhambi hakuna magonjwa na wala Mungu hata siku moja haleti magonjwa bali maovu yetu. Ndiyo maana Yesu anaweza kusame dhambi maana yeye ndiyo huo utakaso kwani damu yake aliyomwaga msalabani ndiyo yenye nguvu ya kutusafisha dhambi zetu zilizo nyekundu kama bendera kuwa nyeupe kama theluji na miyo yetu migumu kama jiwe kuwa laini kama sufi.
Unaongelea asitumie jina la Yesu je wajua kwamba hakuna njia kweli ama uzima pasipo Yesu? Jina la Yesu ndiyo jina kuu kuliko majina yote. Kwa serikali ya Tanzania Jina la Jakaya Kikwete ndilo jina kuu kupita yote siyo kwasababu ni mtoto Wa Kikwete no kwasababu ya authority aliyonayo ya kuamri majeshi yote nayo yakafanya kama atakavyo amuru kwa kufuata katiba ya Jamuhuri ya Tanzania. Basi na kwajinsi hiyo hiyo jina la Yesu ndilo jina pekee mbinguni na duniani lenye uwezo wa kuamrisha majeshi yote ya Mungu kufanya kama anavyoelekeza kwafuata wisdom ya Mungu (Roho mtakatifu). Ndiyo maana kwa jina hilo tunaujasiri wote maana tukilitumia twaweza fanya chochote kama tu tutafanya kufuatana kwa maelekezo ya roho mtakatifu ambaye anakaa ndani yetu; kwa hivyo kwa neno au kwa tendo twaenenda sawa sawa na mapenzi yake. Na mapenzi yake ni haya kila roho ya mwanadamu iirithi uzima wa milele ambao haupatikani katika jinsi yoyote isipokuwa kwa kuliamini hili jina.
Mimi nikisema kwajina la Yesu hakuna uponyaji utakao fanywa na Babu wa Semunge na ndani yake Mungu akaona nimefanya kwa sifa na utukufu wake na siyo kwaajili ya self motives kama kukosa wateja wa kanisa langu au mafungu yao ya kumi na sadaka; inakuwa hivyo no less or more. Maana kila malaika atafuata order yangu. Neno la Mungu linasema hatupati tuviombavyo kwasababu twaomba vibaya kwaajili ya tamaa zetu za kimwili na kuwa maovu yetu yametufarakanisha na Mungu hivyo hata tukiomba yeye hasikii. Ndipo akasema ninyi mkiwa ndani yangu na maneno yangu yakiwa ndani yenu ndipo sasa ombeni lolote kwa jina langu baba atawapeni; hata sasa hamjaomba lolote ombeni nanyi mtapokea ili furaha yenu iwe kamili. Kwa ufupi wengi wetu tunaomba kwa selfish motives, kwamba ili mimi ndiyo nionekane mtakatifu kuliko wote na watumishi wengine wawe second class; ili kuwaumiza wengine e.g mimi ni mkristo naomba nguvu za Mungu ziwe juu yangu ili waislamu na wale wasio wa dini yangu wakome; niwe na afya ili nistarehe na wanawake na ulevi bar; nipate cheo ili watoto wangu wasipate shida na mimi niukate. Nifaulu ili watu wote waniite mimi genious na hivyo nikiwa profesor basi wanikome hapo University hasa wale wanaojidai wao ndo vichwa; Nioe mke mzuri kupita wote ili watu wote wajue mimi pamoja na sura yangu mbaya ni mwanaume wa nguvu etc..Hatusemi hadharani lakini Mungu ajuaye roho ya mwanadamu ajua yote ndiyo maana kwa upendo wake hutunyima hizo zote ili hatimaye tubaki tukimtegemea yeye na kuurithi uzima wa milele.
Amri ya Mungu imekamilika katika upendo maana katika pendo hakuna awezaye kutenda dhambi. Ukimwadhibu mtu kwasababu hiyo tabia inamsababisha huyo kutenda dhambi na kuumiza wengine Mungu yuko pamoja na wewe na ndipo utashangaa binadamu wote watakuchukia lakini baraka zitakufuata na kupitiliza hata usiwe na sehemu ya kuziweka. Lakini ukiacha kuadhibu mtu kwasababu unajua ukifanya hivyo utavuruga mahusiano yako na deal zako za kifisadi basi hata kama ukijipa kila aina ya heshima zote zitageuka kukuzomea na hatimaye utajiona mpweke usiyependwa na yeyote na hatimaye kuishia kulipiza kisasi ambacho nacho hatima yake ni kukugeukia wewe na njia zote ulizotumia kukumaliza wewe mwenyewe huku wale uliowatuhumu pasipo sababu wakiendelea kuheshimiwa na kuinuliwa mbele ya macho yako.
Be blessed!