Baadhi za Hekima na Methali za Kiarabu

Mandago

JF-Expert Member
Feb 8, 2008
238
99
Baadhi za Hekima na Methali za Kiarabu

1) Si vigumu kujitolea kwa kumsaidia rafiki yako,lakini ni vigumu kupata rafiki ajitolee kwa ajili yako.

2) Usiache ulimi wako ukafuata macho yako kwa kueleza aibu za watu, kumbuka kuwa watu nao wana macho na ulimi kama wewe.

3) Mambo yasiyokuwa na umuhimu huzungumzwa kwa muda mrefu kwani sote tuna yafahamu kuliko mambo muhimu.

4) Ikiwa una mikate miwili kula mmoja na mwingine utowe sadaka.

5) Mtu akisifiwa watu wachache huamini,lakini akikashifiwa wengi huamini.

6) Hakuna mtu ambaye hakufanikiwa kabisa,bali ameanzia na sifuri akabakia hapohapo.

7) Binaadamu ambaye amefaulu ni yule anaye nyamaza kabla ya watu hawaja ziba masikio yao, na anafunguwa masikio yake kabla ya watu hawajafunguwa midomo yao.

8) Kabla ya kuzungumza chaguwa neno la kusema, na uchukuwe muda wa kusema ili maneno yako yachipuwe kama linavyo chipuwa tunda.

9) Jihadhari na mtu ambaye ni mkarimu ukimdharau,na mtu mbaya ukimkarimu,na mwenye akili ukimkosowa na mjinga ukimrehemu.

10) Ukifikia kilele mwangalie jambazi ili upate mtu wa kukusaidia,na angalia mbinguni ili Mwenyeezi Mungu akuweke imara usianguke.

11) Si kufaulu kugunduwa mambo wanayo yapenda watu,lakini kufaulu ni kuwa na ujuzi wa kuwafanya watu wakakupenda.

12) Shujaa anaye jitahidi kutatuwa matatizo yake,anafaidika na uwezo wake

13) Ukipanda jabali angalia kilele chake,wala usiangalie upande wowote na ulipande kwa makini,wala usiruke ukavunja mguu wako.

14) Shujaa ni yule ambaye anauwezo wa kukuza ujuzi wake,na kuweza kukuza ujuzi wa watu na pengine kuwabadilisha.

15) Usiache utajiri ukakufanya ukakosana na watu,kwani kuwa pamoja na watu ndio njia ya kuupata utajiri.

16) Badali ya kukaa na kutukana kiza,jaribu kutengeneza umeme.

17) Ukitabasamu tabasamu kwa mtu masikini, kwani kunakuongezea malipo mema kwa Mwenyeezi Mungu.

18) Mwanamke humsubiria mume wake kwa umasikini wake,ubaya wake na kutokumjali kwake ,lakini hamsubirii kwa tabia mbaya yake.

19) Mtoto ni kama udongo(wa ufinyanzi) tuna mlea kwa jinsi tunavyo ona sisi.

20) Watendee watu kama wao ni binaadamu si kwa sura zao wala pesa zao wala vyeo vyao.

21) Uzuri wa mtu ni ndani ya nafsi yake,si sura yake.

22) Ukisema neno litakumiliki,na usipolisema utalimiliki.

23) Anaye ishi na sura mbili,hufa bila ya sura

24) Adui yako akikuomba ushauri mpe nasiha,kwani ukimpa ushauri ataondosha uadui wake kwako na kukusaidia.

25) Ukizungumza wakati ukiwa na hasira,utasema neno ambalo utajutia maisha yako.

26) Usijadiliane na mtu mjeuri wala asiyekuwa na haya, kwani jeuri hutomuweza na asiye na haya atakuudhi.

27) Tabia njema ina sitiri mambo mengi mabaya,na tabia mbaya ina ziba mambo mengi mazuri.

28) Mwenye kumuamini Mwenyeezi Mungu humpa,mwenye kutawakal kwake humtosha,mwenye kumuogopa huacha aliyo yakataza na mwenye kumjuwa humuenzi.


29) Kunyamaza ni dalili ya kukubali jambo.

30) Jihadhari na ulimi wako,usiiponze shingo yako.

31) Fimbo ya muongo ni fupi.

32) Si kila wakati mtu husalimika na jirani.

33) Ulimi wako ni kama farasi wako,ukiuchunga vizuri nao utakuchunga na ukiuachia nao utakuponza.

34) Ndege mmoja aliye mkononi mwako ni bora,kuliko kumi waliyoko katika mti.

35) Kila kimya kina jambo lake.

36) Ukitaka kutiiwa,amrisha mambo yanayo weza kufanywa.

37) Wezi wawili wakigo mbana ,vitajulikana vitu vilivyo ibwa.

38) Jihadhari na shari hata kwa mtu uliye mfanyia mema.

39) Upanga umeshinda kanuni.

40) Mwanzo wa mavuno ni tone la mvuwa.

41) Kuwa na haya ni katika imani.

42) Mazungumzo mazuri huwa mafupi na yanayo eleweka.

43) Mwaka ni kama siku mbili,siku kupata na siku kukosa.

44) Huto pata hasara ukimshauri mtu.

45) Haraka hutokana na shetani.

46) Kila kiongozi,na hotuba yake.

47) Mwenye kuingilia jambo lisilo muhusu,husikia yasiyo mridhisha.

48) Wakati ni kama upanga usipo ukata utakukata.

49) Haurushiwi mawe,isipokuwa mti wenye matunda.

50) Mwenye kuwachunguza watu hufa kwa kiroro(hamu).

51) Watu bora zaidi ni wale wanao towa daawa kwa vitendo vyao kabla ya maneno yao.

52) Uwezo wa kuathiri nyoya za watu,na kupata pendo lao la kweli hutuletea furaha kubwa katika maisha yetu.

53) Nia nzuri ni kufanya ujuzi wa kuwafanyia watu mambo ya ibada,kwani hukukurubisha na Mwenyeezi Mungu(huwa karibu na Mweyeezi Mungu)

54) Usifikirie watu wote ni sawa,kwani kuna watu wenye tabia tofauti kuliko aina za rangi

55) Zungumza na watu kwa mambo ambayo wana penda kuyasikia,siyo kwa mambo ambayo unaya penda wewe.

56) Mkutano wa kwanza huchukuwa asilimia thamanini ya tabia ya mtu anavyo onekana, wafanyie watu wote kama kwamba huo ni mkutano wa kwanza na wa mwisho kati yenu.

57) Kuijuwa tabia ya mtu ndio kuna kupa uwezo wa kupata pendo lake.

58) Kila mtu ana ufunguo wake,kwa kujuwa tabia ya mtu ndio kujuwa njia ya kuelewana nae.

59) Binaadamu hufanya mambo yote kwa moyo wake siyo kwa mwili wake.

60) Ukimiliki nyoyo za watu hupendeka

61) Mtu kujitahidi kutoingilia mambo yasiyo muhusu ni vigumu lakini humpumzisha.

62) Kuwa kama nyuki anatuwa juu ya kitu kizuri na kujiepusha na kitu kibaya, usiwe kama inzi kutuwa juu ya vidonda.

63) Huwezi kula asali bila ya kuvunja nyumba ya nyuki.

64) tukifanya watu wajuwe kwamba tunaangalia mazuri yao kabla ya mabaya yao watakubali kupokea nasiha.

65) Ni bora mtu kujuwa kosa lake si sharti kulisahihisha mbele ya watu.
 
Asante sana ndugu Mandago kwa haya maneno yenye hekima kubwa, nimejifunza mengi katika meneno haya ya hekima.
 
Baadhi za Hekima na Methali za Kiarabu

1) Si vigumu kujitolea kwa kumsaidia rafiki yako,lakini ni vigumu kupata rafiki ajitolee kwa ajili yako.

2) Usiache ulimi wako ukafuata macho yako kwa kueleza aibu za watu, kumbuka kuwa watu nao wana macho na ulimi kama wewe.

3) Mambo yasiyokuwa na umuhimu huzungumzwa kwa muda mrefu kwani sote tuna yafahamu kuliko mambo muhimu.

4) Ikiwa una mikate miwili kula mmoja na mwingine utowe sadaka.

5) Mtu akisifiwa watu wachache huamini,lakini akikashifiwa wengi huamini.

6) Hakuna mtu ambaye hakufanikiwa kabisa,bali ameanzia na sifuri akabakia hapohapo.

7) Binaadamu ambaye amefaulu ni yule anaye nyamaza kabla ya watu hawaja ziba masikio yao, na anafunguwa masikio yake kabla ya watu hawajafunguwa midomo yao.

8) Kabla ya kuzungumza chaguwa neno la kusema, na uchukuwe muda wa kusema ili maneno yako yachipuwe kama linavyo chipuwa tunda.

9) Jihadhari na mtu ambaye ni mkarimu ukimdharau,na mtu mbaya ukimkarimu,na mwenye akili ukimkosowa na mjinga ukimrehemu.

10) Ukifikia kilele mwangalie jambazi ili upate mtu wa kukusaidia,na angalia mbinguni ili Mwenyeezi Mungu akuweke imara usianguke.

11) Si kufaulu kugunduwa mambo wanayo yapenda watu,lakini kufaulu ni kuwa na ujuzi wa kuwafanya watu wakakupenda.

12) Shujaa anaye jitahidi kutatuwa matatizo yake,anafaidika na uwezo wake

13) Ukipanda jabali angalia kilele chake,wala usiangalie upande wowote na ulipande kwa makini,wala usiruke ukavunja mguu wako.

14) Shujaa ni yule ambaye anauwezo wa kukuza ujuzi wake,na kuweza kukuza ujuzi wa watu na pengine kuwabadilisha.

15) Usiache utajiri ukakufanya ukakosana na watu,kwani kuwa pamoja na watu ndio njia ya kuupata utajiri.

16) Badali ya kukaa na kutukana kiza,jaribu kutengeneza umeme.

17) Ukitabasamu tabasamu kwa mtu masikini, kwani kunakuongezea malipo mema kwa Mwenyeezi Mungu.

18) Mwanamke humsubiria mume wake kwa umasikini wake,ubaya wake na kutokumjali kwake ,lakini hamsubirii kwa tabia mbaya yake.

19) Mtoto ni kama udongo(wa ufinyanzi) tuna mlea kwa jinsi tunavyo ona sisi.

20) Watendee watu kama wao ni binaadamu si kwa sura zao wala pesa zao wala vyeo vyao.

21) Uzuri wa mtu ni ndani ya nafsi yake,si sura yake.

22) Ukisema neno litakumiliki,na usipolisema utalimiliki.

23) Anaye ishi na sura mbili,hufa bila ya sura

24) Adui yako akikuomba ushauri mpe nasiha,kwani ukimpa ushauri ataondosha uadui wake kwako na kukusaidia.

25) Ukizungumza wakati ukiwa na hasira,utasema neno ambalo utajutia maisha yako.

26) Usijadiliane na mtu mjeuri wala asiyekuwa na haya, kwani jeuri hutomuweza na asiye na haya atakuudhi.

27) Tabia njema ina sitiri mambo mengi mabaya,na tabia mbaya ina ziba mambo mengi mazuri.

28) Mwenye kumuamini Mwenyeezi Mungu humpa,mwenye kutawakal kwake humtosha,mwenye kumuogopa huacha aliyo yakataza na mwenye kumjuwa humuenzi.


29) Kunyamaza ni dalili ya kukubali jambo.

30) Jihadhari na ulimi wako,usiiponze shingo yako.

31) Fimbo ya muongo ni fupi.

32) Si kila wakati mtu husalimika na jirani.

33) Ulimi wako ni kama farasi wako,ukiuchunga vizuri nao utakuchunga na ukiuachia nao utakuponza.

34) Ndege mmoja aliye mkononi mwako ni bora,kuliko kumi waliyoko katika mti.

35) Kila kimya kina jambo lake.

36) Ukitaka kutiiwa,amrisha mambo yanayo weza kufanywa.

37) Wezi wawili wakigo mbana ,vitajulikana vitu vilivyo ibwa.

38) Jihadhari na shari hata kwa mtu uliye mfanyia mema.

39) Upanga umeshinda kanuni.

40) Mwanzo wa mavuno ni tone la mvuwa.

41) Kuwa na haya ni katika imani.

42) Mazungumzo mazuri huwa mafupi na yanayo eleweka.

43) Mwaka ni kama siku mbili,siku kupata na siku kukosa.

44) Huto pata hasara ukimshauri mtu.

45) Haraka hutokana na shetani.

46) Kila kiongozi,na hotuba yake.

47) Mwenye kuingilia jambo lisilo muhusu,husikia yasiyo mridhisha.

48) Wakati ni kama upanga usipo ukata utakukata.

49) Haurushiwi mawe,isipokuwa mti wenye matunda.

50) Mwenye kuwachunguza watu hufa kwa kiroro(hamu).

51) Watu bora zaidi ni wale wanao towa daawa kwa vitendo vyao kabla ya maneno yao.

52) Uwezo wa kuathiri nyoya za watu,na kupata pendo lao la kweli hutuletea furaha kubwa katika maisha yetu.

53) Nia nzuri ni kufanya ujuzi wa kuwafanyia watu mambo ya ibada,kwani hukukurubisha na Mwenyeezi Mungu(huwa karibu na Mweyeezi Mungu)

54) Usifikirie watu wote ni sawa,kwani kuna watu wenye tabia tofauti kuliko aina za rangi

55) Zungumza na watu kwa mambo ambayo wana penda kuyasikia,siyo kwa mambo ambayo unaya penda wewe.

56) Mkutano wa kwanza huchukuwa asilimia thamanini ya tabia ya mtu anavyo onekana, wafanyie watu wote kama kwamba huo ni mkutano wa kwanza na wa mwisho kati yenu.

57) Kuijuwa tabia ya mtu ndio kuna kupa uwezo wa kupata pendo lake.

58) Kila mtu ana ufunguo wake,kwa kujuwa tabia ya mtu ndio kujuwa njia ya kuelewana nae.

59) Binaadamu hufanya mambo yote kwa moyo wake siyo kwa mwili wake.

60) Ukimiliki nyoyo za watu hupendeka

61) Mtu kujitahidi kutoingilia mambo yasiyo muhusu ni vigumu lakini humpumzisha.

62) Kuwa kama nyuki anatuwa juu ya kitu kizuri na kujiepusha na kitu kibaya, usiwe kama inzi kutuwa juu ya vidonda.

63) Huwezi kula asali bila ya kuvunja nyumba ya nyuki.

64) tukifanya watu wajuwe kwamba tunaangalia mazuri yao kabla ya mabaya yao watakubali kupokea nasiha.

65) Ni bora mtu kujuwa kosa lake si sharti kulisahihisha mbele ya

Yaukweli zimetuliai
 
Back
Top Bottom