100 others
JF-Expert Member
- Aug 5, 2017
- 3,626
- 12,057
Kuna kijana mtaani kwangu alikuwa anatoka kazini usiku, amepanda boda anaelekea nyumbani, ikatokea gari kwa nyuma na kuanza kumfuatilia, jamaa kafika nyumbani na kuingia ndani, sekunde chache tu akasikia mlango ukigongwa kwa nguvu na sauti za kibabe "fungua!!!, fungua!!!".
Jamaa akahoji nyie akina nani? Baada ya majibizano ya hapa na pale, jamaa wakavunja mlango, wakaingia ndani, wakamtandika jamaa haswa.
Wakamchukua jamaa mpaka kituoni, jamaa anawauliza askari mmenipiga hivi na mmenileta kituoni tatizo nini? Nina kesi gani? Polisi wakamwambia ana kesi ya wizi wa simu.
Jamaa kalala ndani hadi kesho, akaletwa dada mmoja anayedaiwa kaibiwa simu aje kuangalia mtuhumiwa na kuthibitisha, jamaa alipoletwa tu mbele ya yule dada, yule dada mpaka alikua analia huku akisema "ndio huyu!"
Jamaa alipigwa na mshangao, hofu na sintofahamu kwa wakati mmoja.
Jamaa akarudi selo, baada ya familia kufuatilia ili kumuokoa, familia ya jamaa ilibidi walipe laki nne, maskini ya Mungu kijana mwenyewe ndio kwao anategemewa.
Huyu kijana kwa kweli namfahamu, ana kibanda chake cha chips, hana hio michezo, lakini polisi walimkamata, wakampiga, wakachukua na pesa yake laki nne, hii ni dhuluma ya kiasi gani?
Kuna kijana mwingine tena ni boda, alikamatwa, akapelekwa kituoni akapewa kesi hio hio ya wizi wa simu, akaletwa mdada akathibitisha huyo boda ndio mwizi,lakini hawa vijana wote wamenihadithia mimi kwa nyakati tofauti na kiukweli hawana hizo tabia.
Baadhi ya askari hawana nia njema, wanawatesa wananchi na kudhulumu mali zao, hawa wanasababisha polisi wote waonekane ni wale wale.
Najua kuna wengi tu humu wana mikasa ambayo imewatokea au ndugu jamaa na marafiki wanaowafahamu.
Askari dumisheni ukaribu na wananchi, shirikianeni na wananchi, hata raisi kawaambieni... hakuna kitu kibaya kama wananchi kuwachukieni.
Huwa mkipanda kwenye hilo defender mnajiona kama dunia ni yenu, lakini kama hamna ushirikiano na wananchi ni kazi bure!
Jamaa akahoji nyie akina nani? Baada ya majibizano ya hapa na pale, jamaa wakavunja mlango, wakaingia ndani, wakamtandika jamaa haswa.
Wakamchukua jamaa mpaka kituoni, jamaa anawauliza askari mmenipiga hivi na mmenileta kituoni tatizo nini? Nina kesi gani? Polisi wakamwambia ana kesi ya wizi wa simu.
Jamaa kalala ndani hadi kesho, akaletwa dada mmoja anayedaiwa kaibiwa simu aje kuangalia mtuhumiwa na kuthibitisha, jamaa alipoletwa tu mbele ya yule dada, yule dada mpaka alikua analia huku akisema "ndio huyu!"
Jamaa alipigwa na mshangao, hofu na sintofahamu kwa wakati mmoja.
Jamaa akarudi selo, baada ya familia kufuatilia ili kumuokoa, familia ya jamaa ilibidi walipe laki nne, maskini ya Mungu kijana mwenyewe ndio kwao anategemewa.
Huyu kijana kwa kweli namfahamu, ana kibanda chake cha chips, hana hio michezo, lakini polisi walimkamata, wakampiga, wakachukua na pesa yake laki nne, hii ni dhuluma ya kiasi gani?
Kuna kijana mwingine tena ni boda, alikamatwa, akapelekwa kituoni akapewa kesi hio hio ya wizi wa simu, akaletwa mdada akathibitisha huyo boda ndio mwizi,lakini hawa vijana wote wamenihadithia mimi kwa nyakati tofauti na kiukweli hawana hizo tabia.
Baadhi ya askari hawana nia njema, wanawatesa wananchi na kudhulumu mali zao, hawa wanasababisha polisi wote waonekane ni wale wale.
Najua kuna wengi tu humu wana mikasa ambayo imewatokea au ndugu jamaa na marafiki wanaowafahamu.
Askari dumisheni ukaribu na wananchi, shirikianeni na wananchi, hata raisi kawaambieni... hakuna kitu kibaya kama wananchi kuwachukieni.
Huwa mkipanda kwenye hilo defender mnajiona kama dunia ni yenu, lakini kama hamna ushirikiano na wananchi ni kazi bure!