Baada ya serikali kuondoa fao la kujitoa, ianzishe fao la kukosa ajira

mahololelo

Member
Oct 11, 2011
32
5
Wadau nawarudisha nyuma kidogo turejee kwenye hoja ya fao lakujitoa ambalo Serikali imeamua kuliondoa miongoni mwa mafao yanayotolewa na mifuko ya hifadhi ya jamii, mijadala mbalimbali ilifanywa na washikadau lakini mpaka sasa hakuna taarifa njema kwa sisi wahanga juu ya fao la kujitoa.

Mapendekezo ya serikali ni kuanzisha fao la kukosa ajira ambalo malipo yake hayana tija kwa wafanyakazi wanaotoka kwenye sekta zisizo na ajira ya kudumu au ajira za mikataba ya muda mfupi, hivyo basi rai yangu ni kwa wale wote ambao tunaona umuhimu wa fao hili kiuchumi baada ya ajira kukoma tutumie uzi huu kumuomba Mh.Rais,Dkt J.P.Magufuli atuangalie kwa jicho la pili ili tuweze kujiajiri pindi ajira zinapokwisha.

Ninayo imani kuwa mh.rais atatusikia na kutufanya tuendelee kuwa walipa kodi kwa maendeleo ya Taifa.naomba kuwasilisha
 
Asante ndugu mleta hoja,namie na declare intrest kua ni miongoni mwa watu tusio kua na ajira za uhakika na zenye hatari kubwa kiafya.nafanya kazi kwenye mgodi wa dhahabu,namuomba mh rais alitazame hili kwa jicho la tatu tuweze kupata pesa yetu pindi kazi inapokwisha ili tujiajiri na kuijenga nchi yetu.
 
Hata ukimalizia kwa lugha nzuri inayompendeza Rais ya kulipa kodi, yeye alishasema hafanyii kazi maneno ya mtandao
 
Wabongo tuache kuiamini mitandao kama ndo taarifa kamili ya kila ktu,

Nilitembelea LAPF january hii na wakaniambia wao bado wana fao la kujitoa, na hata NSSF pia lipo la kujitoa na GEPF ndo hawana mjadala katika hilo maana wao waliwekwa specially kwa watu wa mikataba so hilo fao haliwez ondolewa kwao.

Tofaut na zaman, fao hilo limeongezewa masharti lukuki ili wale wanaohama makampuni wasiweze chukua hela zao kila baada ya miaka mi3/5. ila kwa mtu anayehitaji kujitoa sheria bado inaruhusu kujitoa.
 
Kama Una Baba yako, Mama Yako, Bibi Babu, Dada Na Hata wewe Mwenyewe na Wanyonge Wote Serikali ya Awamu ya Tano Imekaribia kuleta Mkong'oto Huu Huu hapa (Kilio na kusaga Meno)

Kuna mswada unakuja na kwa Bunge letu la Wangapi wanakubali Waseme Ndiyooooo "Ndiyoooooo" waliosema ndiyo wameshinda "Utapita"

MSWADA HUO Unaenda kuua wastaafu Na sisi Tunao karibia kustafu

Ni hivi Mafao ya wastafuu yatakuwa hivi Tega sikio, utalazimika kulipwa 38% tu na 62% utakuwa unalipwa kila Mwezi (monthly) hapa ili unielewe nikupe mfano. kama ilikuwa ulipwe milioni 100 kama hela yako ya kustafia maana yake kwa mswada mpya utalipwa pension ya mkupuo 38 milioni halafu milioni 62 ulipwa kila mwezi.

Ukistafu na umri wa miaka 61 utakula hicho kiasi cha million 38 kigingine utalipwa kidogo kidogo kila mwezi

Ubaya wa hili siku ukifa tu kila kitu kimekufa malipo kila mwezi nayo yanakufa. Hivyo hela nyingi zitabaki kwenye mifuko maana rekodi inaonyesha wastaafu wengi hawaishi muda mrefu na hasa ukizingatia mafao yatapungua.

2. Mume akifa Mke na wategemezi watahudumiwa miaka 3 tu kisha huduma itakoma wakati ungepewa yote ungewaachia miradi familia wakaishi hata kama haupo

3. March 2018 mifuko itaunganishwa kubaki mifuko 2 tu. Yaani LPF, NSSF PPF sijui nani sijui nani itafungwa na kubaki mifuko miwili tu (Vibarua vinaenda kuota nyasi)

4. April 2018 sheria itaanza kutumika Yaani Mwakani Kuna kilio kikuu kwa watumishi wa mifugo na wastafuu

My Take

Kwa ufupi bila kupindisha muswada huu utaumiza watumishi wote ,Bunge Mkafanye kazi yenu, sasa Hiki ni kipimo chenu cha kudhibitisha Mpo huru na kwamba ni muhimili unajitegemea ,Wabunge wetu msipoliona hili kuwasemea watumishi basi Mtawasononesha watumishi

Yaani Ufanye kazi miaka 61 ukitumikia umma uzeeni uporwe haki itasikitisha

Alloyce Nyanda
Mtozi
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom