Azam Media mmekosa washauri? Punguzeni bei za vifurushi kunusuru bidhaa yenu

Nimewachoka hawa Azam na silipii hicho kingamuzi chao tena!!!
Wangeongezea channels za movie na documentaries kufidia zile local channels walizofungiwa lakini wao wanatujazia machannel za kiganda.
 
Nimewachoka hawa Azam na silipii hicho kingamuzi chao tena!!!
Wangeongezea channels za movie na documentaries kufidia zile local channels walizofungiwa lakini wao wanatujazia machannel za kiganda.
Sina hamu na kisimbuz cha Azam tena, samahani hivi ni visimbuzi gani alivyo twambia Mwakyembe kuwa ni bure nikanunue hivyo
 
Nakushangaa sana wewe unayewatakia mema wakati sisi wenzio ving'amuzi hivyo tangu channel za ndani zilipoondolewa tumevitia kabatini. Uliona kituo gani cha luninga ambacho taarifa yake ya habari inatazamwa na wateja wenye Smartphone tu?
 
Ni jambo la muda tu nina imani watakuwa bora na kurudi kwenye superbrand nadhani management yao iko vzuri sana
1-tido
2-baruan muhuza
3-abdul mohd
4-chaz hilal
 
Nimekuwa nikijiuliza hichi kitengo hakina washauri au ni jeuri tu waliyonayo ndio inawafanya wasibadilike?, Azam media baada ya kupoteza chanel za ndani na pia baada ya kutoonyesha taarifa za Habari, mlitakiwa mjitafakari kuwa hadi sasa nshawapoteza wateja wangapi

Mlitakiwa mpunguze bei ya vifurushi vyenu kutoka 23k angalau bei ipungue hadi 15k ili kufidia chanel zilizopotea, ili kulinda biashara yenu mnatakiwa mpunguze bei ya hivyo vifurushi vyenu la sivyo mtajikuta mnaanza kupunguza wafanyakazi kwa ukata

Mtajikuta mnabakiwa na watazamaji wa ligi kuu na tamthilia ya Hurem maana ndio vitu vilivyobakia vyenye watazamaji, Ni swala la muda tu kama msipochukua hatua mapema mapato yenu yatapungua na mtajikuta mkipunguza wafanyakazi Badilikeni, la sivyo mda utaongea
Umeona mbali sana ! mimi ninalipa kifurushi cha elfu 28 lakini nimeanza kutafakari upya
 
Back
Top Bottom