1979Magufuli
JF-Expert Member
- Feb 20, 2023
- 438
- 1,752
Ni kipa mzuri kwa sababu rekodi zake kule F A Rabat zinajulikana, naona amesifiwa sana tangu alipopangua penati vs Wydad, hata hivyo Ayoub licha ya uzuri wake golini lakini ana tatizo kubwa ambalo asiporekebishwa atakuja kuigharimu timu.
Mwangalieni Ayoub vizuri, ana tatizo katika upigaji wa mipira mbele, anaweza kupiga mbelee juu ukaenda nje au akadhamiria kupiga ndefu juu lakini mpira ukakataa ukaenda ndefu chini na ukamkuta adui, hilo ni tatizo kubwa alilokuwa nalo, lingine hajui kuanzisha mpira pale anaporudishiwa na beki, ukimrudishia mpira Ayoub ana kitete cha kumwanzishia beki wake, wakati mwingine hadi adui amsogelee ndio anapiga mpira, akikutana na adui mjanja anampokonya mpira kizembe na anafunga.
Makosa hayo huwezi kumkuta Diarra wa Yanga, ana control na anajua kupiga mipira mirefu, Manula naye anaweza kupiga ndefu ila hana control kama Diarra, otherwise muda wa kusema Ayoub ni kipa wa ukweli tuendelee kusubiri, ndumba nyingi hapa bongo.
Mwangalieni Ayoub vizuri, ana tatizo katika upigaji wa mipira mbele, anaweza kupiga mbelee juu ukaenda nje au akadhamiria kupiga ndefu juu lakini mpira ukakataa ukaenda ndefu chini na ukamkuta adui, hilo ni tatizo kubwa alilokuwa nalo, lingine hajui kuanzisha mpira pale anaporudishiwa na beki, ukimrudishia mpira Ayoub ana kitete cha kumwanzishia beki wake, wakati mwingine hadi adui amsogelee ndio anapiga mpira, akikutana na adui mjanja anampokonya mpira kizembe na anafunga.
Makosa hayo huwezi kumkuta Diarra wa Yanga, ana control na anajua kupiga mipira mirefu, Manula naye anaweza kupiga ndefu ila hana control kama Diarra, otherwise muda wa kusema Ayoub ni kipa wa ukweli tuendelee kusubiri, ndumba nyingi hapa bongo.