Atletico Madrid na fainali mbili

Petro E. Mselewa

JF-Expert Member
Dec 27, 2012
10,197
25,517
Klabu Atletico Madrid ya Hispania imejichomoza mwaka huu wa ligi 2013/2014 kama timu ya ushindani na inayotaka kubeba makombe. Ikiwa chini ya Diego Simeone,kiungo wa zamani wa Argentina, Atletico imeonyesha kuiva na kuimarika kwake katika kusakata kandanda la nguvu,kasi,ufundi na ushindi.

Sasa inakabiliwa na fainali mbili.Ya kwanza ni ya La Liga.Ikiwa inaongoza kwa alama 89 na huku Barcelona ikifuatia kwa alama 86,Atletico itahitaji sare ya iana yoyote au ushindi dhidi ya Barcelona hapo tarehe 17/5/2014 katika uwanja wa Camp Nou ili kutwaa ubingwa wa La Liga. Ikifungwa,Barcelona itatwaa ubingwa kwakuwa ina uwiano mzuri kuliko Atletico katika mabao ya kufunga.

Fainali ya pili itacheza mnamo tarehe 24/5/2014 katika jiji la Lisboni,Ureno.Itakuwa ni fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya Real Madrid.Katika mechi hii,Atletico itahitaji ushindi kutwaa kombe hilo la vilabu bingwa Barani Ulaya. Atletico itajaribu kutwaa kombe hilo kwa mara ya kwanza katika historia yake.

Katika fainali zake mbili,Atletico anapambana na wababe wa Hispania na Ulaya. Atachomoza na kutwaa makombe yote au hata moja?
 
Anakosa yote kwani baca na real hawatamwacha , ila msijenge chuki ni itani tu ila hamwezi amin game mbili kali sana yeyote anaweza lia!


Kama utakua unafuatilia la liga mechi za karibuni utajua kua lolote linaweza kutokea na mechi zote mbili zinaweza zisiwe na mvuto. Wachezaji wengi wenye majina wanaogopa kuumia wakakosa kombe la dunia na ndio maana karibu mechi nyingi za mwisho hawajaoonyesha kujituma(A.Madrid/R.Madrid/Bac) wamekua wakipata matokeo mabaya.
 
barca hatokubali tena kupigwakwa mara ya pili msimu huu ukizingatia gem inapigwa pale camp nou chini ya washabiki wasiopungua 900000 visca barca
 
Mechi ya Barca vs At Madrid,barca akishinda atakuwa bingwa kwa sababu game ya kwanza ilikuwa sare,mshindi huamuliwa katika mechi 2 mlizocheza na si vinginevyo,kila la kheri Atretico...piga wote wawili...
 
barca hatokubali tena kupigwakwa mara ya pili msimu huu ukizingatia gem inapigwa pale camp nou chini ya washabiki wasiopungua 900000 visca barca

Duuh mkuu ni 90,000 sio 900,000. I hope ni typing error.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom