Askofu Shoo: Kuna watu wanajaribu kuwajaza wengine hofu ili wasiseme ukweli na wasikae katika kweli

Mwanahabari Huru

JF-Expert Member
Mar 9, 2015
14,243
34,896
SALAMU ZA MWAKA MPYA.!

Siku chache baada ya Askofu Zacharia Kakobe wa FGBF kutishiwa na vyombo vya dola baada ya kutoa maoni yake kuhusu imani yake na nchi yake, Mkuu wa kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Askofu Dr.Frederick Shoo (PhD) amesema Watanzania hivi sasa wanajengewa hofu ili wasiseme ukweli wa kile wanachokiamini.

“Kuna watu wanajaribu kuwajaza wengine hofu ili wasiseme ukweli na wasikae katika kweli. Watu wanajazwa hofu ili wasitetee kile wanachokiona ni cha haki. Watu wanajazwa hofu ili wasiwe huru kutoa mawazo yao kuhusu Kristo. Wengine wanajazwa hofu ili wasiweze kutoa maoni yao kuhusu nchi yao. Na wengine wanapotoa maoni yao kuhusu imani yao wanatishiwa. Hii si sawa. Ni lazima tuikubali kweli. Na tukidumu katika kweli tutakuwa na uhuru wa kusema na kutembea bila woga.” amesema Askofu Shoo.

shoo.jpg
 
SALAMU ZA MWAKA MPYA.!

Siku chache baada ya Askofu Zacharia Kakobe wa FGBF kutishiwa na vyombo vya dola baada ya kutoa maoni yake kuhusu imani yake na nchi yake, Mkuu wa kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Askofu Dr.Frederick Shoo (PhD) amesema Watanzania hivi sasa wanajengewa hofu ili wasiseme ukweli wa kile wanachokiamini.

“Kuna watu wanajaribu kuwajaza wengine hofu ili wasiseme ukweli na wasikae katika kweli. Watu wanajazwa hofu ili wasitetee kile wanachokiona ni cha haki. Watu wanajazwa hofu ili wasiwe huru kutoa mawazo yao kuhusu Kristo. Wengine wanajazwa hofu ili wasiweze kutoa maoni yao kuhusu nchi yao. Na wengine wanapotoa maoni yao kuhusu imani yao wanatishiwa. Hii si sawa. Ni lazima tuikubali kweli. Na tukidumu katika kweli tutakuwa na uhuru wa kusema na kutembea bila woga.” amesema Askofu Shoo.

View attachment 665421


Huyo naye ni Askofu pia, waumini wana kazi, Full vilaza!

Hivi hawa Maaskofu hupatikanaje? Huwa mnapiga kura au husukumiziwa tu kwenu ktk mahali kwa maana, Duh!
 
Back
Top Bottom