BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,789
- 288,015
NINAKWENDA KATIKA MSAFARA WA LISSU PAMOJA NA UWEZEKANO WA KUPIGWA MAWE AU KURUSHIWA MABOMU NA RISASI!
Wiki iliyopita Jeshi la Polisi lilizuia Msafara wa Mheshimiwa Lissu eneo la Kiluvya jijini Dar es Salaam pasipo sababu za msingi kwani kama kungelikuwa na ukiukwaji wa taratibu za Kampeni basi Tume ingelimchukulia hatua. Nilipokwenda kumuona, Polisi waliokuwa na silaha walinitisha wakitaka kunizua nisiende kumuona Lissu. Kilikuwa ni kituko cha aina yake! Utamzuiaje kwa kumtisha Askofu huru katika nchi huru ili kumkataza kumuona raia huru katika mazingira huru? Walilenga kuficha nini kwa Askofu na kwa jumuiya ya kimataifa? Watu wengi hawajui kuwa Askofu ni jicho pia la Jumuiya ya Kimataifa katika nchi ye yote ile. Vitisho na zuio lao hata hivyo havikufanikiwa!
Jana tarehe 13 Oktoba 2020, nilipata muda wa kuongea kwa simu na baadhi ya walinzi wa Lissu baada ya kupata taarifa kuhusu shambulio dhidi ya Mheshimiwa Lissu kule Chato! Mmoja alikuwa ana maumivu makali katika bega baada ya kurushiwa mawe. Niliarifiwa kuwa watu kadhaa waliumizwa katika tukio lile.
Bado tunajiuliza maswali mengi kuhusu vurugu za Chato na Geita kwa ujumla dhidi ya Mheshimiwa Lissu. Hivi inakuwaje Mgombea Urais kufanyiwa chuki na vurugu kubwa kama zile nyumbani kwa Rais? Hivi ni nani na nini kilichokuwa nyuma ya hayo yote? Je, ni wivu, uhuni, chuki, wivu, au ukabila? Hiki ni kiashirio gani katika eneo ambalo asilimia kubwa ya wakazi wake ni Wakristo? Viongozi wakuu wa Kanisa katika Mkoa wa Geita wamelichukuliaje jambo hilo?
Tangu kampeni zianze, Lissu na Mgombea Mwenza wake wamekuwa wakilengwa kwa vurugu dhidi yao kutoka kwa makundi yanayoandaliwa kimkakati. Kama hilo halitoshi, manyanyaso kutoka Jeshi la Polisi katika baadhi ya maeneo na mikakati ya Tume kuengua Wagombea wa CHADEMA na ACT Wazalendo vimetumika kama mbinu ya kudhoofisha na kuhujumu upinzani katika Uchaguzi huu. Hii si HAKI hata kidogo.
Kama Askofu ninakemea vitendo hivyo na ninaomba viongozi wote wa dini tukiwa kama sauti ya maadili nchini tuungane katika kuonya na kukemea uovu huu na uporaji wa haki nchini.
Pamoja na vitisho hivyo, nipo njiani kwenda katika Msafara wa Mheshimiwa Lissu. Haki huinua taifa!
Mwana Kondoo Ameshinda! Tumfuate!
+Emmmaus Bandekile Mwamakula - Kanisa la Moravian la Uamsho Tanzania & Afrika Mashariki.
Wiki iliyopita Jeshi la Polisi lilizuia Msafara wa Mheshimiwa Lissu eneo la Kiluvya jijini Dar es Salaam pasipo sababu za msingi kwani kama kungelikuwa na ukiukwaji wa taratibu za Kampeni basi Tume ingelimchukulia hatua. Nilipokwenda kumuona, Polisi waliokuwa na silaha walinitisha wakitaka kunizua nisiende kumuona Lissu. Kilikuwa ni kituko cha aina yake! Utamzuiaje kwa kumtisha Askofu huru katika nchi huru ili kumkataza kumuona raia huru katika mazingira huru? Walilenga kuficha nini kwa Askofu na kwa jumuiya ya kimataifa? Watu wengi hawajui kuwa Askofu ni jicho pia la Jumuiya ya Kimataifa katika nchi ye yote ile. Vitisho na zuio lao hata hivyo havikufanikiwa!
Jana tarehe 13 Oktoba 2020, nilipata muda wa kuongea kwa simu na baadhi ya walinzi wa Lissu baada ya kupata taarifa kuhusu shambulio dhidi ya Mheshimiwa Lissu kule Chato! Mmoja alikuwa ana maumivu makali katika bega baada ya kurushiwa mawe. Niliarifiwa kuwa watu kadhaa waliumizwa katika tukio lile.
Bado tunajiuliza maswali mengi kuhusu vurugu za Chato na Geita kwa ujumla dhidi ya Mheshimiwa Lissu. Hivi inakuwaje Mgombea Urais kufanyiwa chuki na vurugu kubwa kama zile nyumbani kwa Rais? Hivi ni nani na nini kilichokuwa nyuma ya hayo yote? Je, ni wivu, uhuni, chuki, wivu, au ukabila? Hiki ni kiashirio gani katika eneo ambalo asilimia kubwa ya wakazi wake ni Wakristo? Viongozi wakuu wa Kanisa katika Mkoa wa Geita wamelichukuliaje jambo hilo?
Tangu kampeni zianze, Lissu na Mgombea Mwenza wake wamekuwa wakilengwa kwa vurugu dhidi yao kutoka kwa makundi yanayoandaliwa kimkakati. Kama hilo halitoshi, manyanyaso kutoka Jeshi la Polisi katika baadhi ya maeneo na mikakati ya Tume kuengua Wagombea wa CHADEMA na ACT Wazalendo vimetumika kama mbinu ya kudhoofisha na kuhujumu upinzani katika Uchaguzi huu. Hii si HAKI hata kidogo.
Kama Askofu ninakemea vitendo hivyo na ninaomba viongozi wote wa dini tukiwa kama sauti ya maadili nchini tuungane katika kuonya na kukemea uovu huu na uporaji wa haki nchini.
Pamoja na vitisho hivyo, nipo njiani kwenda katika Msafara wa Mheshimiwa Lissu. Haki huinua taifa!
Mwana Kondoo Ameshinda! Tumfuate!
+Emmmaus Bandekile Mwamakula - Kanisa la Moravian la Uamsho Tanzania & Afrika Mashariki.