Askari wa Jeshi la Sudan wamechukua hatua ya kuwalinda waandamanaji mjini Khartoum baada ya vikosi vya usalama kufyatua mabomu ya gesi

SACO

JF-Expert Member
Jul 25, 2011
2,321
2,914
WANAJESHI SUDAN WAWALINDA WAANDAMANAJI: Askari wa Jeshi la Sudan wamechukua hatua ya kuwalinda waandamanaji mjini Khartoum baada ya vikosi vya usalama kufyatua mabomu ya gesi ya kutoa machozi ili kuwatawanya waandamanaji hao.

Hatua hiyo imekuja kwa mshangao baada ya wanajeshi hao kuyakimbiza magari yaliyokuwa yakifyatua gesi ya kutoa machozi, katika siku ya pili ya waandamanaji waliokusanyika na kumtaka Rais Omar al-Bashir kujiuzulu.

Waandamanaji wamepata hifadhi katika kambi ya askari wa jeshi la wanamaji, ambapo inaoneka wazi kuwepo kwa mgawanyiko miongoni mwa majeshi ya nchi hiyo.

Rais Bashir mpaka sasa amekataa maombi ya kutaka kuwepo kwa serikali ya mpito atakapojiuzulu.

Rais wa Chama cha Madaktari wa Sudan Tawi la Uingereza, Sara Abdelgalil amesema kilichotokea nchini Algeria kimekuwa chachu ya wananchi wa Sudan kutaka Rais Bashir ajiuzulu kama ilivyotokea kwa Rais Bouteflika wa Algeria.
 
Ikiwa ni kweli basi zama za Bashir ziko ukingoni

USOGA WI KUA KATI MWINA NSONGOO
 
Nashangaa nyuzi kama hizi wachangiaji wengi huingia mitini, watu wanapenda zile zilizojaa unafiki wa kuunga mkono juhudi.

All in all, the fugitive Al Bashir is a spent force and it's high time he went, in thirty years of his misrule, Sudan has nothing to show in development terms. The high cost of living has left many people as paupers when the incumbent is ducking his ugly head under the shelter of state house to avoid the ICC's arrest warrant.

Time is up for the disenchanted people of Sudan to tighten the noose so as to bring about the dictator's downfall and hence pave the way for his eventual indictment by The Hague based ICC.
 
Jana hiyo
FB_IMG_1554728266412.jpeg
FB_IMG_1554728259344.jpeg
GBWA-20190407191249.jpeg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom