KIBURUDISHO
JF-Expert Member
- Mar 28, 2011
- 1,002
- 274
Nikiwa Mwanza mtaani maeneo ya bandarini nimeiona gari ya polisi ikiwa imefika ikiwa na mwili wa marehemu tayari kwa usafiri wa meli wa saa nne usiku kwenda Bukoba.Kwa bahati nzuri kati ya askari waliokuwa katika gari ile kulikuwa na askari mmoja ninae mfahamu tulisalimiana na kumuuliza wapi wanakotoka na wanakokwenda.Akaniambia wanatoka Serengeti wanaelekea Bukoba na aliyefariki ni askari mwenzao aliyemtaja kwa jina moja la Upendo(kiume) wa kituo cha polisi cha Mugumu Serengeti na alikutwa na mkasa huo jana usiku maeneo ya huko Tarime alipigwa risasi ya shingoni walikokuwa wamekwenda kumkamata jambazi sugu.