Bavaria
JF-Expert Member
- Jun 14, 2011
- 53,102
- 53,357
ASKARI wawili wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) kambi ya Mirambo mkoani hapa ni miongoni mwa watu tisa waliokamatwa na kikosi cha kuzuia ujangili wakiwa na mbao 630 bila kibali.
Wanajeshi hao Koplo Moshi Jumanne na Praiveti Mustapha Yusuf, walikamatwa wakiwa na gari kubwa la JWTZ aina ya Iveco likiwa limesheheni mbao ndani ya Pori la Akiba la Kigosi mkoani hapa.
Walikamatwa Ijumaa saa mbili usiku wakiwa na gari hilo pamoja na mwanamke aitwaye Sophia Shigemela ndani ya pori hilo eneo la Ulyankulu wilayani Urambo.
Mkurugenzi wa Mipango na Matumizi ya Rasilimali Misitu (TFS), Vallentine Msusa aliwaambia waandishi wa habari jana kuwa alipewa taarifa juu ya kukamatwa kwa watumishi hao wa Serikali wakiwa na maliasili hizo bila kuwa na kibali, kitendo ambacho ni cha aibu kwa Taifa. Msusa alisema gari lililokamatwa bado linashikiliwa katika kambi ya ndani ya pori hilo likiwa na mbao hizo.
Alisema siku za karibuni watu wengi wamekuwa wakitumia magari ya Serikali kusafirisha maliasili za misitu kwa vile hayakaguliwi kwenye vizuizi na kusababisha kupakwa matope watumishi wa wizara hiyo kuwa wahusika wa uvunaji holela wa maliasili.
Msusa alisema kitendo cha watendaji wa Serikali kutumia magari yao kusafirishia mazao ya maliasili, kimesaidia majangili kuingia ndani ya mapori na kuvuna mali zilizopo kwa kujiamini.
"Tulitarajia taasisi za umma zingesaidia ulinzi wa misitu na raslimali zilizomo, lakini kumbe sivyo," alisema Msusa.
Kwa mujibu wa Msusa, wanajeshi hao na watu wengine waliokamatwa na magari yakiwa na mbao hizo wanatarajiwa kufikishwa mahakamani kujibu tuhuma zinazowakabili.
Vitisho Katika hatua nyingine, Msusa alisema kumekuwa na matukio yasiyofurahisha kwani wiki mbili zilizopita, askari wa JWTZ wa kikosi cha Mirambo walimpiga mtumishi wa Idara ya Misitu huku wakimtishia kumuua.
Habari zilizopatikana kutoka ya kambi Kikosi cha Kuzuia Ujangili katika pori hilo, zilidai kuwa magari ya JWTZ yamekuwa yakibeba mbao ndani ya pori hilo mara mbili kwa wiki, wakidai kuwa wanakwenda kutumia katika ofisi zao. Inadaiwa kuwa askari hao wawili baada ya kukamatwa wakiwa na Sophia, walidai kuwa wamekodishwa.
Hata hivyo, kwa mujibu wa madai hayo, baada ya mahojiano, askari hao walidai kutoka Biharamulo na walikuwa wamesafirisha maiti lakini wakakosa mafuta ya kuwarudisha kwao, ndipo wakakubali kukodishwa ili wapate fedha za mafuta ya kurudia.
Watu wengine waliokamatwa siku hiyo wakiwa na gari namba T 761 BCV aina ya Fuso likiwa na mbao zaidi ya 350, ni Kiwele William na Sultan Hamda dereva wa Fuso, Richard Samwel, Msina John, Bashiba Lugaka na Gaspar Kugatwa.
SOURCE: HabariLeo
Wanajeshi hao Koplo Moshi Jumanne na Praiveti Mustapha Yusuf, walikamatwa wakiwa na gari kubwa la JWTZ aina ya Iveco likiwa limesheheni mbao ndani ya Pori la Akiba la Kigosi mkoani hapa.
Walikamatwa Ijumaa saa mbili usiku wakiwa na gari hilo pamoja na mwanamke aitwaye Sophia Shigemela ndani ya pori hilo eneo la Ulyankulu wilayani Urambo.
Mkurugenzi wa Mipango na Matumizi ya Rasilimali Misitu (TFS), Vallentine Msusa aliwaambia waandishi wa habari jana kuwa alipewa taarifa juu ya kukamatwa kwa watumishi hao wa Serikali wakiwa na maliasili hizo bila kuwa na kibali, kitendo ambacho ni cha aibu kwa Taifa. Msusa alisema gari lililokamatwa bado linashikiliwa katika kambi ya ndani ya pori hilo likiwa na mbao hizo.
Alisema siku za karibuni watu wengi wamekuwa wakitumia magari ya Serikali kusafirisha maliasili za misitu kwa vile hayakaguliwi kwenye vizuizi na kusababisha kupakwa matope watumishi wa wizara hiyo kuwa wahusika wa uvunaji holela wa maliasili.
Msusa alisema kitendo cha watendaji wa Serikali kutumia magari yao kusafirishia mazao ya maliasili, kimesaidia majangili kuingia ndani ya mapori na kuvuna mali zilizopo kwa kujiamini.
"Tulitarajia taasisi za umma zingesaidia ulinzi wa misitu na raslimali zilizomo, lakini kumbe sivyo," alisema Msusa.
Kwa mujibu wa Msusa, wanajeshi hao na watu wengine waliokamatwa na magari yakiwa na mbao hizo wanatarajiwa kufikishwa mahakamani kujibu tuhuma zinazowakabili.
Vitisho Katika hatua nyingine, Msusa alisema kumekuwa na matukio yasiyofurahisha kwani wiki mbili zilizopita, askari wa JWTZ wa kikosi cha Mirambo walimpiga mtumishi wa Idara ya Misitu huku wakimtishia kumuua.
Habari zilizopatikana kutoka ya kambi Kikosi cha Kuzuia Ujangili katika pori hilo, zilidai kuwa magari ya JWTZ yamekuwa yakibeba mbao ndani ya pori hilo mara mbili kwa wiki, wakidai kuwa wanakwenda kutumia katika ofisi zao. Inadaiwa kuwa askari hao wawili baada ya kukamatwa wakiwa na Sophia, walidai kuwa wamekodishwa.
Hata hivyo, kwa mujibu wa madai hayo, baada ya mahojiano, askari hao walidai kutoka Biharamulo na walikuwa wamesafirisha maiti lakini wakakosa mafuta ya kuwarudisha kwao, ndipo wakakubali kukodishwa ili wapate fedha za mafuta ya kurudia.
Watu wengine waliokamatwa siku hiyo wakiwa na gari namba T 761 BCV aina ya Fuso likiwa na mbao zaidi ya 350, ni Kiwele William na Sultan Hamda dereva wa Fuso, Richard Samwel, Msina John, Bashiba Lugaka na Gaspar Kugatwa.
SOURCE: HabariLeo