Askari amuua askari mwenzie Mtwara

Mjanja M1

JF-Expert Member
Oct 7, 2018
3,660
12,304
Askari wa Jeshi la Polisi Mkoani Mtwara Mkaguzi Msaidizi wa Polisi Eliuterius Hyera, aliyekuwa Mkuu wa Kituo Kidogo cha Polisi Chiungutwa wilayani Masasi, amefariki dunia baada ya kujeruhiwa kwa risasi na askari mwenzie.

Taarifa kutoka kwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mtwara Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Nicodemus Katembo leo Februari 03, 2024, imeeleza kuwa askari hao walikuwa kwenye jukumu la ukamataji wa mtuhumiwa anayedaiwa kuvunja ofisi (Haikutajwa) na kuiba.

“Mtuhumiwa huyo alianza kukimbia ili asikamatwe ndipo Askari aliyekuwa na bastola alipofyatua risasi kwa lengo la kufanikisha ukamataji na ikapelekea kumjeruhi Mkaguzi huyo.

Juhudi za kuokoa maisha yake zilifanyika kwa kupelekwa Hospitali ya Ndanda ambapo alifariki dunia akiendelea na matibabu.” Imeeleza taarifa ya ACP Katembo.

Taarifa hiyo imeeleza kuwa mwili wa marehemu umehifadhiwa hospitalini hapo kwa uchunguzi zaidi, huku mtuhumiwa akiendelea kushikiliwa kwa hatua zaidi za kisheria.

Source - CloudsTv
 
Askari wa Jeshi la Polisi Mkoani Mtwara Mkaguzi Msaidizi wa Polisi Eliuterius Hyera, aliyekuwa Mkuu wa Kituo Kidogo cha Polisi Chiungutwa wilayani Masasi, amefariki dunia baada ya kujeruhiwa kwa risasi na askari mwenzie.

Taarifa kutoka kwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mtwara Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Nicodemus Katembo leo Februari 03, 2024, imeeleza kuwa askari hao walikuwa kwenye jukumu la ukamataji wa mtuhumiwa anayedaiwa kuvunja ofisi (Haikutajwa) na kuiba.

“Mtuhumiwa huyo alianza kukimbia ili asikamatwe ndipo Askari aliyekuwa na bastola alipofyatua risasi kwa lengo la kufanikisha ukamataji na ikapelekea kumjeruhi Mkaguzi huyo.

Juhudi za kuokoa maisha yake zilifanyika kwa kupelekwa Hospitali ya Ndanda ambapo alifariki dunia akiendelea na matibabu.” Imeeleza taarifa ya ACP Katembo.

Taarifa hiyo imeeleza kuwa mwili wa marehemu umehifadhiwa hospitalini hapo kwa uchunguzi zaidi, huku mtuhumiwa akiendelea kushikiliwa kwa hatua zaidi za kisheria.

Source - CloudsTv
Dog 🐕 Kala Dog.
 
Askari wa Jeshi la Polisi Mkoani Mtwara Mkaguzi Msaidizi wa Polisi Eliuterius Hyera, aliyekuwa Mkuu wa Kituo Kidogo cha Polisi Chiungutwa wilayani Masasi, amefariki dunia baada ya kujeruhiwa kwa risasi na askari mwenzie.

Taarifa kutoka kwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mtwara Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Nicodemus Katembo leo Februari 03, 2024, imeeleza kuwa askari hao walikuwa kwenye jukumu la ukamataji wa mtuhumiwa anayedaiwa kuvunja ofisi (Haikutajwa) na kuiba.

“Mtuhumiwa huyo alianza kukimbia ili asikamatwe ndipo Askari aliyekuwa na bastola alipofyatua risasi kwa lengo la kufanikisha ukamataji na ikapelekea kumjeruhi Mkaguzi huyo.

Juhudi za kuokoa maisha yake zilifanyika kwa kupelekwa Hospitali ya Ndanda ambapo alifariki dunia akiendelea na matibabu.” Imeeleza taarifa ya ACP Katembo.

Taarifa hiyo imeeleza kuwa mwili wa marehemu umehifadhiwa hospitalini hapo kwa uchunguzi zaidi, huku mtuhumiwa akiendelea kushikiliwa kwa hatua zaidi za kisheria.

Source - CloudsTv
Maelezo ya kamanda hayajanyooka na hayajitoshelezi. Angekuwa raia ingeamriwa awekwe chini ya ulinzi ahojiwe zaidi.

Maelezo mepesi kwa kifo cha bi adamu,tena afisa wa ngazi ya juu wa jeshi.

Hapa maswali tupu, hakuna jibu.

Kamata watu wekeni ndani waeleze vizuri
 
Mtuhumiwa huyo alianza kukimbia ili asikamatwe ndipo Askari aliyekuwa na bastola alipofyatua risasi kwa lengo la kufanikisha ukamataji na ikapelekea kumjeruhi Mkaguzi huyo.

Taarifa hiyo imeeleza kuwa mwili wa marehemu umehifadhiwa hospitalini hapo kwa uchunguzi zaidi, huku mtuhumiwa akiendelea kushikiliwa kwa hatua zaidi za kisheria.
Mbona haijaelezwa ni namna gani mtuhumiwa alikamatwa mara baada ya askari polisi kujeruhiana? Au wamemfanya askari mwenye bastola kuwa mtuhumiwa pia??
 
Isije ikawa tu ni laana ndiyo imeanza kuwaandama. Maana na wenyewe hawajambo kwenye vifo kukuki vyenye utata kwa watuhumiwa.
 
Back
Top Bottom