Asiyefunzwa na mamaye...hufunzwa na ulimwengu

Msindima

JF-Expert Member
Mar 30, 2009
1,018
33
Mh! Sikio la kufa halisikii dawa ni baada ya Miss Tanzanian2006, Wema Abraham Sepetu kuendeleza sakata la vihoja visivyokuwa na kichwa wala miguu na kuweza kufunguliwa mashitaka mengine tena yatokana na wizi.

Kwani Mrembo huyo aliweza tena kurudishwa na kufunguliwa tena mashitaka mengine, na kuswekwa tena rumande kwenye kituo cha Polisi cha Kijitonyama kilichopo hapa jijiji.

Si pekeyake bali akiwa na mpenzi wake Jumbe, wamefunguliwa mashitaka ya wizi a televisheni, redio ikiwemo na microwave.

Wema pamoja na Jumbe wamefunguliwa jalada namba KJN/RB/1977/09 linalohusiana na wizi huo, na kubainisha kuwa mrembo huyo alibeba vitu hivyo kutoka kwao na kupotea navyo kwa mpenzi wake huyo ambako alijichimbia kwa siku kadhaa.

Mbali na kuibka na vioja vingine bado kesi yake ya kuvunja kioo cha gari la aliyekuwa mpenzi wake, mwigizaji maarufu, Steven Kanumba inaendelea katika Mahakama ya Kinondoni.

Kwani mama mzazi wa mrembo huyo akiwemo na dada yake walionekana ndani ya kituo cha Kijitonyama, kuhusiana na suala hilo.

Na imeelezwa walikuwa wanataka waelezwe vilipo vitu hivyo ili wawatoe nje kwa dhamana.

Siku chache za usoni hali ya Wema ilionekana kubadilika baada ya mama yake kumtafutia kazi, lakini siku chache zilizopita tabia yake ilibadilika tena na kuanza kurejea usiku nyumbani katika eneo la Sinza jirani na Lion Hotel ambako ni nyumbani kwa dada yake anakoishi baada ya kuibuka kwa tafrani mahakamani siku alipowekewa dhamana mwezi uliopita.

Jumbe amekuwa akituhumiwa kumfundisha mrembo huyo kutumia dawa za kulevya, na alishindwa hata kumwekea dhamana alipolazimika kulala mahabusu.

Imeelezwa alipotea kwa dada yake eneo la Sinza kwa zaidi ya siku mbili na walikuwa hawajui aliko na baadaye ilielezwa alirejea tena kwa Jumbe ambaye ndugu zake wanamtuhumu kuwa 'amemchezea’ mrembo huyo ambaye anaonekana kutosikia .
 
Naona jamaa is hitting the mmmh like he is supposed to, hakuna kulogwa wala nini. Wazazi wake kama vipi wampotezee. Kidume chenyewe kinashindwa kutoa dhamana ya nusu milioni tu, inaelekea huko skani wataanza kula dagaa deile siku si nyingi. Kila la kheri Wema.
 
Wema ana matatizo ya kisaikojia anahitaji msaada wa kitaalamu.
Inaonekana hata Mama Wema, hajalijua hili kwa sababu mama mtu mwenyewe aliingilia nyumba ya Isack Sepetu enzi hizo akiwa waziri. Mama alifuata uzito na pesa hivyo ndivyo anavyotaaka kumfundisha Wema utu ni pesa. Mama hataki kumsikia Jumbe kwa vile hana kitu.

Naungana na Wema katika kupenda pendo la dhati kwa kupatiwa anachokitaka toka kwa Jumbe. Siungu mkono vituko vyake bali naelewa vinahitaji uelewa na usaidizi wa counseling na sio hasira
Na ukali kama wa mama Wema.
Mtu aliyekaribu nao ni kwanza wamkubali Jumbe, namna ya kumsaidia Wema ni kuanza na kumsaidia Jumbe, amsaidie Wema.
 
Back
Top Bottom