kilimasera
JF-Expert Member
- Dec 2, 2009
- 3,068
- 268
ASILIMIA nne hadi sita ya Watanzania ndio wanaodaiwa kujua kunawa mikono kabla na baada ya kula huku kundi kubwa likionekana kutokujali kabisa afya zao, ilielezwa.Kauli hiyo ilitolewa juzi na Mkurugenzi wa Idara ya Kinga katika Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Dk Donan Mmbando wakati akikabidhi choo kwa mshindi wa shindano la fyatua choo na ushinde.
Dk Mmbando alisema idadi kubwa ya Watanzania yaani zaidi ya asilimia 94 hawana mazoea ya kunawa kabla ya kula na baada ya kula jambo ambalo ni hatari sana katika afya zao.
Alisema ingawa kwa Waafrika wengi hilo limekuwa ni tatizo, lakini kwa Watanzania linakuwa ni tatizo sugu ambalo linatakiwa kushughulikiwa kwa kila mtu kubadili tabia yake katika kuijali afya yake na familia yake.
Mkurugenzi huyo alisema kama kila mmoja atamua kwa dhati katika kuanzisha mapambano juu ya afya yake hakuna jambo ambalo linaweza kushindikana.
Katika zoezi hilo ambalo alimkabidhi choo chenye thamani ya zaidi ya Sh 22 milioni Fatuma Ally, Mmbando aliwataka Watanzania kujenga tabia ya kutumia vyoo na si kuvijenga na kuvitelekeza.
Alisema wengi wamekuwa wakijenga vyoo vyao, lakini badala ya kuvitumia kwa kazi inayokusudiwa wamekuwa hawavitumia na matokeo yake vinabaki kama urembo wa nyumba.
Mtaalamu huyo wa afya alilaani pia kitendo cha madereva wa magari makubwa wanaopenda kusimamisha magari yao maporini kwa mtindo wa kuchimba dawa na kusema kuwa wanahatarisha afya za wasafiri wao.
Kwa upande wake mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto (Unicef), Judina Mtenga aliahidi kumsaidia Fatuma tanki la maji lenye ujazo wa lita 3,000 ili choo hicho chenye matundu manane kianze kutumika hata kabla ya maji hayajafika katika eneo hilo.
Fatuma alijengewa choo hicho kwa ajili ya kukifanyia biashara kati ya makubaliano yake na Manispaa ya Dodoma katika eneo linakotarajiwa kujengwa Soko la Kisasa katika Kata ya Changombe na kwamba uongozi wa Manispaa kupitia kwa Naibu Meya Jumanne Ngede uliahidi kumpa ushirikiano wa hali na mali ili kuuweka mji huo katika hali ya usafi.
Dk Mmbando alisema idadi kubwa ya Watanzania yaani zaidi ya asilimia 94 hawana mazoea ya kunawa kabla ya kula na baada ya kula jambo ambalo ni hatari sana katika afya zao.
Alisema ingawa kwa Waafrika wengi hilo limekuwa ni tatizo, lakini kwa Watanzania linakuwa ni tatizo sugu ambalo linatakiwa kushughulikiwa kwa kila mtu kubadili tabia yake katika kuijali afya yake na familia yake.
Mkurugenzi huyo alisema kama kila mmoja atamua kwa dhati katika kuanzisha mapambano juu ya afya yake hakuna jambo ambalo linaweza kushindikana.
Katika zoezi hilo ambalo alimkabidhi choo chenye thamani ya zaidi ya Sh 22 milioni Fatuma Ally, Mmbando aliwataka Watanzania kujenga tabia ya kutumia vyoo na si kuvijenga na kuvitelekeza.
Alisema wengi wamekuwa wakijenga vyoo vyao, lakini badala ya kuvitumia kwa kazi inayokusudiwa wamekuwa hawavitumia na matokeo yake vinabaki kama urembo wa nyumba.
Mtaalamu huyo wa afya alilaani pia kitendo cha madereva wa magari makubwa wanaopenda kusimamisha magari yao maporini kwa mtindo wa kuchimba dawa na kusema kuwa wanahatarisha afya za wasafiri wao.
Kwa upande wake mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto (Unicef), Judina Mtenga aliahidi kumsaidia Fatuma tanki la maji lenye ujazo wa lita 3,000 ili choo hicho chenye matundu manane kianze kutumika hata kabla ya maji hayajafika katika eneo hilo.
Fatuma alijengewa choo hicho kwa ajili ya kukifanyia biashara kati ya makubaliano yake na Manispaa ya Dodoma katika eneo linakotarajiwa kujengwa Soko la Kisasa katika Kata ya Changombe na kwamba uongozi wa Manispaa kupitia kwa Naibu Meya Jumanne Ngede uliahidi kumpa ushirikiano wa hali na mali ili kuuweka mji huo katika hali ya usafi.