Ardhi na Maendeleo ya mgeni njoo mwenyeji akonde!

John Mnyika

JF-Expert Member
Jun 16, 2006
712
1,240
Mwezi Machi, nilipata wasaa wa kushiriki mkutano wa wananchi katika mtaa wa Kwembe, mkutano mambo kadhaa niliyatakari siku hiyo yaliyonifanya niandike makala ifuatayo ambayo naamini maudhui yake yanapaswa kujadiliwa:

"Wahenga walisema, mgeni njoo mwenyeji apone. Msemo huu, ni ishara ya baraka njema inayoletwa na wageni chini ya ukarimu wa kiafrika. Hata hivyo, yapo maeneo ambayo ujio wa wageni ama wa mambo mageni umezua hasara kwa upande wa wenyeji. Tunayaona hayo katika maeneo ya uwekezaji ambayo wenyeji wameondolewa kwa shuruti kupisha wageni bila kupata manufaa ya kutosha kutokana na ujio wa wageni hao. Hayo yamejitokeza katika sekta za uchimbaji madini, uwindaji na maeneo mengine yanayohusiana na rasilimali za taifa. Hapo ndio unapoweza kuzuka msemo mpya wa mgeni njoo mwenyeji akonde. Si dhamira ya makala yangu ya leo kuzungumzia hayo ya wageni katika maeneo ya rasilimali wengi wao wakiwa kutoka nje, leo nataka nizungumze kuhusu wageni wa ndani katika sekta ya ardhi. Inaendelea

Makala kamili inapatikana hapa: JJ: March 2009

JJ
 
Hakuna bilioni tatu zilipotea kifisadi kama ambavyo makala imeeleza. Fedha hizo wamelipwa fidia wananchi, na kuwakwamua kiuchumi chini ya falsafa ya maisha bora kwa kila Mtanzania. Waziri Chiligati naye anapowapa waandishi wa habari viwanja hivyo ni sehemu ya jitihada za serikali kuwajali wanahabari. Halafu saula hili sasa limepelekwa mahakamani hivyo kuendelea kulijadili ni kuingilia uhuru wa mahakama.

.........ndiyohiyo
 
Hakuna bilioni tatu zilipotea kifisadi kama ambavyo makala imeeleza. Fedha hizo wamelipwa fidia wananchi, na kuwakwamua kiuchumi chini ya falsafa ya maisha bora kwa kila Mtanzania. Waziri Chiligati naye anapowapa waandishi wa habari viwanja hivyo ni sehemu ya jitihada za serikali kuwajali wanahabari. Halafu saula hili sasa limepelekwa mahakamani hivyo kuendelea kulijadili ni kuingilia uhuru wa mahakama.

.........ndiyohiyo

Kwani mahakama imekataza kulijadili? Na wale wasiohusika na kesi nao hawatakiwi kujadili yanayofanyika mahakamani?
 
Yohana wa Mnyika,

Nashukuru umelileta hili nikakumbuka taarifa kuwa Kenya wamingia mkataba na Oman wa kuwapa Oman ardhi wajilimie Chakula kwa miaka 80 kwa malipo ya kujengewa Bandari yenye thamani ya Dola Bilioni 4!

Sasa najiuliza, je hiyo ardhi ni pori lisilo na watu sasa hivi? je kama kuna watu, watahamishwa na wapelekwe wapi? je kutakuwa na rutuba na maji ya kutosha kwa kujilimia na kulisha mifugo yao kama huko wanakondolewa ili mwekezaji ajilimie kwa kutujengea Bandari?

Leaders look for highest bidder to ‘auction’ State



Sunday, 5th April 2009



Billed as an effective instrument through which the cash-strapped Government can tap into funding from the private sector, the public-private partnership mechanism is raising concerns the country is being auctioned.
The business and legal fraternities expressed the fears when the State belatedly gazetted public-private partnerships (PPPs) regulations last week after it went on prime property selling spree that runs into billions of shillings in Nairobi, the Coast and northern Kenya , where the Government envisages to build a resort city.
Since late last year, the Government has been on shopping spree for investments in the transport, aviation, agriculture, oil and hotel industry. Kenya enlisted Qatari and Kuwaiti firms to develop the Lamu seaport and related infrastructure.
Kuwaiti contract
Transport PS Gerishon Ikiara made the announcement in 2007 when he confirmed the contract awarded to Al Bader International Development Company of Kuwait had been approved by the Cabinet.
The Government has also leased out 100,000 hectares of Tana River basin to the Qatar government for 80 years to grow food in exchange for the construction of the port at $4.8 billion (Sh350 billion).
Ndubi questioned the efficacy of the new regulations published by Finance Minister Uhuru Kenyatta on March 10 in the Kenya Gazette Supplement. They compel procuring agencies to benchmark the deals on value for money, transaction advisor, steering committee and a permanent secretariat.
The regulations also provide for an oversight body to vet all the partnerships. However, Ndubi pointed out the requirements were flouted "and there is now real fear the so-called foreign firms are Kenyan foreign registered companies."
The lawyer told The Standard on Sunday there is questionable eagerness in the Government to secretly sell, concession or lease public property.
"The partnerships are another avenue for corruption," he said.
Fears that the PPPs are a new front for corruption first came to public attention last year during the controversial disposal of the Grand Regency Hotel by Central Bank. The deal was one of those executed without regard to laid down procedures.
The Kenya Airports Authority (KAA) has signed Sh28 billion deal with the Qatar-based Afro-Asian Investment Corporation to build a five-star three-tower hotel on a 90-acre land at the Jomo Kenyatta International Airport. The hotel complex with a 750-bed capacity and a 200-inpatient capacity hospital will be completed in 2012.
The deals were sealed with Sheikh Hamad bin Khalifa Al Thani during President Kibaki’s visit to the oil-rich emirate last November.
The PPPs provide that such contracts be cleared by an oversight committee, whose members include permanent secretaries in the ministries of Finance and Planning and Vision 2030. The committee has not been constituted.
The recent deals smack of the controversial transfer of Government shareholding in hitherto quasi-state-owned telecommunication firms, Safaricom and Telkom Kenya, whose privatisation raised serious questions about transparency.
The Standard on Sunday has since Wednesday tried to reach Planning Minister Wycliffe Oparanya, under whose docket Vision 2030 falls, without success. Attempts to get Parliamentary Investment Committee Chairman Mithika Linturi to shade light on the foreign investment deals flopped after the Igembe South MP received The Standard on Sunday call only to disconnect when asked about the information his committee has on the investments. He did not answer subsequent calls from Wednesday afternoon to Friday.
Selling spree
Transparency International (Kenya) Director Job Ogonda concurred with Ndubi’s observations that the state is on selling spree. He said the mechanism picked momentum after the Government published an economic development prospectus designed to transform Kenya into a newly industrialised nation by 2030.
The development programme, estimated to cost Sh1.7 trillion, has unleashed a scramble for resources in the private sector. However, the execution of the economic blueprint is raising concern the Executive is auctioning national resources to foreigners.
The hunger for financial capital has escalated public fears of a looming rip-off after the Government executed five mega-shilling projects within a short period with little evidence, if any, of viability of the deals in the plum infrastructure, agriculture, transport, aviation and hotel industries.
The duration of the partnerships, some in the form of concessions, will be valid for as long 80 years, implying even children born after the country goes to polls in 2012 will never own these resources even if life expectancy rose to 75 years.
Aware of growing public concerns that the control of lucrative economic sectors was being vested in private hands, the Government grafted a build, own, operate and transfer provision in the PPPs regulations to cushion itself against potential legal questions. The new regulations, it appears, are being implemented retroactively to justify and legalise the actions.
Ogonda, a lawyer, said the multibillion-shilling deals have raised questions about governance and transparency issues. Ndubi concurred, but added the Government had found another avenue to sell off public property corruptly.
"There is a possibility that the so-called foreign partners are Kenyan-owned firms but incorporated in foreign countries. Ordinarily, national land cannot be alienated and given to foreigners without them being vetted," the lawyer said, citing the controversy around Mobitelea, which had a five per cent stake in Safaricom. Mobitelea is alleged to be a Kenyan-owned company incorporated abroad.
 
Kwani mahakama imekataza kulijadili? Na wale wasiohusika na kesi nao hawatakiwi kujadili yanayofanyika mahakamani?

Kweli, halafu inaonyesha hiyo makala ni ya Machi wakati kesi imefungiliwa April. Halafu humo kwenye makala imeelezwa ni kwa namna gani hizo bilioni 3 za walipa kodi zimetafunwa, na jinsi Chiligati anavyotumia kofia ya Uwaziri kugawa hivyo viwanja kwa wanahabari gazeti la CCM uhuru. Kwanini hajagawa kwa wa habari leo wa serekali kama ana lengo la kuwajali waandishi?

Asha
 
Kwani mahakama imekataza kulijadili? Na wale wasiohusika na kesi nao hawatakiwi kujadili yanayofanyika mahakamani?
Mahakama haina mamlaka ya kuzuia freedom of expression ambayo iko kwenye katiba yetu kufuatia kuridhia lile alizimio la haki za binaadamu.

Hata hivyo, mahakama inazuia kulijadili shauri lililoko mahakamani katika hali ambayo inaweza kuingilia uhuru wa mahakama katika kutenda haki 'contempt of the court'

Sisi tunafuata mfumo wa sheria wa Comon
Law tuliorithishwa na waingereza ambapo mtuhumiwa yoyote anahesabiwa 'not guilt until proven guilt by the court of competent jurisdiction'.

Kwa sheria hii, ni marufuku kupiga posed pictures/video au kuwakutanisha watuhumiwa wakiwa chini ya ulinzi wa polisi au mahakamani.

Ni mara ngapi tunaonyeshwa video na picha za watuhumiwa wakiwa mikononi mwa polisi?.
Ni mara ngapi wapiga picha na video wanapiga picha watuhumiwa ndani ya mahakama?. Vitendo vyote hivi ni ukiukwaji wa haki za binaadamu na kuingilia uhuru wa mahakama lakini mahakama imekaa kimya, wahusiki hawalalamiki kwa vile hawajui haki zao.

Tufike mahali, wanaichi waelimishwe haki zao ili kuziba mianya ya watu kutotendewa haki.

Nimemsoma JJMnyika, issue kubwa ni watu kujua haki zao
Na kuhakikisha serikali inawatendea haki.

Maeneo husika kama Kwembe, sio maeneo yanayomilikiwa na 'Customary Land Law' kwa mujibu wa Sheria ya Ardhi ya Vijiji No.5 ya 1999. Hao wananchi ni wavamizi wa maeneo hayo na sheria imeukubali uvamizi wa miaka mingi ndio maana wanatoa fidia na kukubali kuhama.

Kwenye ardhi halisi inayomilikiwa kimila, hata serikali haiwezi kuthubutu kuyatwaa maeneo hayo, mfano uchagani, umasaini, ama kwa Wahaya, wanaithamini ardhi kuliko thamani ya hela yoyote na kwao bora damu imwagike na sio ardhi iondoke.

Pointi muhimu sana Mnyika ameraise ni hii ya Watu kutambua haki zao, na hata ukishatambua haki zako, hauletewi kwenye kisahani cha chai, bali ni lazima uzidai haki hizo.
 
Back
Top Bottom