Herbalist Dr MziziMkavu
JF-Expert Member
- Feb 3, 2009
- 42,318
- 33,125
Friday, September 11, 2009 4:53 AM
Jamaa mmoja wa nchini Austria alipiga dua zote alizozijua wakati aliponasa kwenye lifti na baada ya kuokolewa alikimbilia moja kwa moja kanisani kumshukuru mungu na kuangukiwa na sanamu na kufariki. Gunther Link, muumini mkubwa wa kanisa katoliki alipiga dua zote alizokuwa akizijua kumuomba mungu amuokoe baada ya kunasa kwenye lifti kwenye jengo moja la ghorofa katika jiji la Vienna, Austria.
Link mwenye umri wa miaka 45, alikimbilia moja kwa moja kanisani baada ya kuokolewa ili amshukuru mungu kwa kumuokoa.
Akiwa kwenye kanisa hilo, Link aliangukiwa na sanamu la kihistoria la yesu lililotengenezwa kwa mawe lililokuwa na uzito wa kilo 390 na alifariki papo hapo.
Roman Hahslinger, msemaji wa polisi wa AVienna alisema: " Link alikuwa ni mtu wa dini sana na alihofia sana maisha yake baada ya kunasa ndani ya lift. aliomba dua sana kwa mungu amuokoe".
"Muda mfupi baada ya kuokolewa kutoka kwenye lift hiyo, alienda moja kwa moja kanisani kumshukuru mungu".
"Inaonekana kama aliiegemea na kuitingisha nguzo ambayo sanamu hilo lilikuwepo na ndipo lilipomdondokea. Alifariki papo hapo".
"Tumezigundua alama za vidole kwenye nguzo na tunalifanyia uchunguzi zaidi suala hili" alisema msemaji huyo wa polisi.
Mwili wa Link uligunduliwa siku iliyofuatia na waumini walioenda kanisani kusali huku ndugu zake wakiwa wametoa ripoti polisi kupotea kwa ndugu yao.
http://www.nifahamishe.com/NewsDetails.aspx?NewsId=3055882&&Cat=2