Msabaha lk
Member
- Apr 21, 2012
- 84
- 21
Leo asubuhi nilikuwa nasikiliza mwendelezo wa hotuba ya dr h Mwakyembe! yes kausomea udoctor! lkn nimeshindwa kumwelewa kabisa Kasimama mbele ya vyombo vya habari kututajia walinzi! Binafsi siamini kama wale wanahatia kwani hata kama ile kazi wasinge iruhusu kupenya basi huenda maisha yao yangekuwa matatani. Nilichotegemea kutoka kwa mtu mkubwa kama waziri mwakyembe ni kutuambia baada ya kuona muvi nzima kupitia makamera hayo ya JNIA amefanya uchunguzi gani na kubaini wanaosafirisha hiyo mizigo. kwa mtu na akili zake kumvimbisha kichwa MWAKYEMBE kuwa ni Mchapa kazi ni kuwadanganya watanzania ili wamuonapo mkuu wa kaya akigawa uwaziri kumfikiria huyu mtu. Sikubali utaratibu alooutumia MWAKYEMBE kwani hakutueleza ni jinsi gani amepambana na mizizi ya tatizo na siyo ujinga wa kuwapumbaza watanzania. kumfukuza mlinzi na wauza madawa ya kulevya wapi na wapi? hao ni dagaa tu mapapa yapo yanafikiria ni jinsi gani yawatumie hao vijana kupanu miradi yao. Miradi ya wakubwa tunajua ukilima bangi unatafutwa kwa udi ila wenye vidonge vya unga hadi wakamatwe out. nilichojifunza kwa taarifa ya Dr ni kuwa kitendo cha wauza unga kukamatwa sauz Africa kimetia doa TANZANIA hivyo waziri kaona kujiosha ni kuwatimulia mbali walinzi. huenda hata hawajahojiwa ili wasimwage siri za mtandao wa unga. Inauma sana