Anayechangia Bajeti Amepanda Economy Class, Anayepokea Michango Yuko Business Class!

maggid

JF-Expert Member
Dec 3, 2006
1,084
1,246


Ndugu zangu,

AFRIKA kuna mambo! Kuna picha niliyotundika jana bloguni; mjengwa.blogspot.com iliyozua mjadala mkubwa kuhusiana na matumizi ya Serikali na hususan matumizi ya viongozi waandamizi wa Serikali. Ni ni picha inayomwonyesha balozi wa Sweden nchini Tanzania, Lennart Hjalmaker alipokuwa safarini kuelekea Sweden akitokea Dar es Salaam.

Balozi huyo alionekana akiwa kwenye economy class. Nikaandika, kuwa katika nchi zetu hizi, katika ndege hiyo hiyo, yaweza kabisa kukawa na Waziri wa Serikali au hata Balozi wetu nje ya nchi ambaye amepanda Business Class yenye gharama kubwa huku anayechangia asilimia 40 ya bajeti yetu amepanda economy class. Naam. Nimeona kuwa huu ni mjadala wenye tija kwa nchi yetu na hususan katika kipindi hiki cha bajeti. Wengine mnasemaje?

Maggid,
Sweden,
Juni 11, 2011
http://mjengwa.blogspot.com
 


Ndugu zangu,

AFRIKA kuna mambo! Kuna picha niliyotundika jana bloguni; mjengwablog.com iliyozua mjadala mkubwa kuhusiana na matumizi ya Serikali na hususan matumizi ya viongozi waandamizi wa Serikali. Ni ni picha inayomwonyesha balozi wa Sweden nchini Tanzania, Lennart Hjalmaker alipokuwa safarini kuelekea Sweden akitokea Dar es Salaam.

Balozi huyo alionekana akiwa kwenye economy class. Nikaandika, kuwa katika nchi zetu hizi, katika ndege hiyo hiyo, yaweza kabisa kukawa na Waziri wa Serikali au hata Balozi wetu nje ya nchi ambaye amepanda Business Class yenye gharama kubwa huku anayechangia asilimia 40 ya bajeti yetu amepanda economy class. Naam. Nimeona kuwa huu ni mjadala wenye tija kwa nchi yetu na hususan katika kipindi hiki cha bajeti. Wengine mnasemaje?

Maggid,
Sweden,
Juni 11, 2011
http://mjengwa.blogspot.com

Si ibandike na hapa basi, au mpaka tuje kwenye blog yako?
 
Kwa Tanzania hata mkuu wa idara katika wizara/shirika la umma nk anasafiri business class kwenye ndege.
 
kuna marketing manager mmoja wa shirika la uma aliwahi kunambia kuwa yeye hajawahi kupanda economy class ktk maisha yake, ni bora ya hao walio first class kuna viongozi wetu wanakodi ndege nzima dar-dom, dar-mara, dar-bkb etc
 
Asante kwa kuja na mfano hai kabisa.

Toka alipochaguliwa kuwa waziri mkuu wa Uingereza, David Cameron, tumeona alivyokuwa na mikakati ya makusudi kabisa kubana au kupunguza matumizi yasiyokuwa ya lazima.
Hii ni nchi tajiri sana ukilinganisha na nchi yetu, ni wazi tunahitaji juhudi hizi kupunguza gharama.

Leo mawaziri na manaibu, makatibu wakuu, na viongozi wengine waandamizi, tunaona jinsi wanavyofunga misafara kuelekea Dodoma..Hapo kuna Overtime, gharama za hotel, mafuta ya magari yao na mambo mengine.

ni hatari kwa kweli kwa nchi yetu maskini. Mara kumi hata Bunge la Bajeti lifanyike Dar kupunguza gharama kwa sababu wamegoma kuhamia Dodoma. Unashangaa kwa nini nyumba za kuishi viongozi zejengwe Dar na wakati huo huo wana mkakati wa kuhamia makao makuu, it doesnt make sense at all.

hayo ni baadhi tu, ya vitu au mambo ambayo tungeweza kuyafanyia kazi...Ningekuwa mimi ndo Waziri Mkuu, viongozi wote wangepanda mabasi kuelekea Dodoma..full stop
 
Hili ni mojawapo ya gamba, viongozi kujiona wako tofauti na wananchi wa kawaida. Cha ajabu ni kwamba ukiwa bussiness or economy wote mnafika pamoja. Lakini itamchukua mda mrefu sana kiongozi wetu kuamini kwamba atafika mda sawa na watu walio economy. These people nafikiri wanatamani ata mbinguni wawe first class. Nafikiri cha kufanya ni kuwaomba awa wafadhili wawa-adabishe viongozi wetu, manake haiingii akilini mtu anayekupa msaada 40% yupo economy alaf unayesaidiwa unavinjari business class! Mie ningekuwa mmoja kati ya wafadhili immediate ningekata misaada. Kwa mantiki ya kawaida sie ndo tunatakiwa tuwasidie awa wasweden kwa sababu balozi wao hawezi kulipia tiketi ya ghali, sisi tunaweza na tumenyesha uwezo tunao. Zito kasema hasipewe posho, Mkulo anamjibu kuwa anatafuta umaarufu, na wakati uyo uyo Mkulo katuambia serikali katika bajeti hii imepunguza posho za wakubwa. Ilitakiwa ampe Zito ushirikiano na kuwaomba wabunge wengine wenye nia kama yake waungane kuzikataa posho. Hii nchi sometimes ukifikiria sana unaweza kujidunga sindano ya sumu ufe na ukubali yaishe, Hatubadiliki na wala hatuna dalili za kubadilika
 
Mjengwa, mpe michuzi na yeye aibandike...hawa waheshimiwa wanaiamini ile blogu yake, huenda weekend hii wakiwa Dar kwa maandalizi ya kurudi tena Dodoma kesho, waione..wasijisahau
 
Back
Top Bottom