commited
JF-Expert Member
- Feb 27, 2012
- 1,626
- 870
habarini za asubuhi ndugu zangu, bila shaka kwa uwezo wake maulana wote hatujambo.
Ni mejitokeza hapa kupata ushauri ili nami nikautoe sehemu ili kuhakikisah haki inapatikana,
kuna mdogo (binti miaka 20) wa jamaa yangu amebakwa hapo maeneo ya arusha majuzi alhamisi usiku (17/05 2012) mida ya sa mbili usiku, alitumwa sehemu akachukue maziwa, kwa bahati mbaya wakati anapita sehemu ambayo kiasi kuna giza, akatokea mtu (kijana wa kume) akamziba mdomo na akamtolea kisu kisha akambaka. Sasa kwa bahati mbaya huyu binti ambaye ni mdogo wa jamaa yangu anasema huyo kijana aliyemfanyia huo ukatili hamjui jina ila kwa sura anamtambua kuwa wanaishi naye hapo mtaani, ni mara kadhaa huyo mbakaji amewahi kumtongoza huyo binti lakini huyo binti (aliyebakwa) amekuwa akimkataa.
Ugumu wa hii ishu unakujaje, huyu binti baada ya kubakwa tangu hiyo alhamisi usiku alivyobakwa hakusema, zaidi ya kushinda ndani na huku akilia, mpaka jana jumamosi asubuhi wazazi walipomuhisi anatatizo, kumuhoji ndio akaeleza hayo niliyoeleza
maswali,
1. Wazazi hawana uwezo wa kiuchumi, sasa wanaanza kuhofia kuwa wakienda polisi then mahakamani, inaweza kuwa gharimu pesa nyingi ambazo wao hawana
2. Wanahisi hawatakuwa na nguvu ya kisheria kwa kuwa ule ushahidi halisi wa labda majimaji ya mbegu za kiume hayapo tena kwa sababu huyo mbakwaji tayari ameshaoga
3. Na kwa mujibu wa maelezo yaliyopo inahisiwa huyu binti ameingiliwa siku mbaya ambazo inawezekana atakuwa anaujauzito
sasa ndugu zangu naomba tusaidianae mawazo kwa sababu naamini humu kila mtu anamazo tofauti, lengo ni kusaidia kama huyu binti anaweza bado kwenda mbele ya vyombo vya sheria, na je kama bahati mbaya akapimwa akautwa tayari ana mimba au virusi vya ukimwi ni nini cha kufanya..
Karibuni kwa ushauri na maoni, tukio limetokea alhamisi usiku.
Ni mejitokeza hapa kupata ushauri ili nami nikautoe sehemu ili kuhakikisah haki inapatikana,
kuna mdogo (binti miaka 20) wa jamaa yangu amebakwa hapo maeneo ya arusha majuzi alhamisi usiku (17/05 2012) mida ya sa mbili usiku, alitumwa sehemu akachukue maziwa, kwa bahati mbaya wakati anapita sehemu ambayo kiasi kuna giza, akatokea mtu (kijana wa kume) akamziba mdomo na akamtolea kisu kisha akambaka. Sasa kwa bahati mbaya huyu binti ambaye ni mdogo wa jamaa yangu anasema huyo kijana aliyemfanyia huo ukatili hamjui jina ila kwa sura anamtambua kuwa wanaishi naye hapo mtaani, ni mara kadhaa huyo mbakaji amewahi kumtongoza huyo binti lakini huyo binti (aliyebakwa) amekuwa akimkataa.
Ugumu wa hii ishu unakujaje, huyu binti baada ya kubakwa tangu hiyo alhamisi usiku alivyobakwa hakusema, zaidi ya kushinda ndani na huku akilia, mpaka jana jumamosi asubuhi wazazi walipomuhisi anatatizo, kumuhoji ndio akaeleza hayo niliyoeleza
maswali,
1. Wazazi hawana uwezo wa kiuchumi, sasa wanaanza kuhofia kuwa wakienda polisi then mahakamani, inaweza kuwa gharimu pesa nyingi ambazo wao hawana
2. Wanahisi hawatakuwa na nguvu ya kisheria kwa kuwa ule ushahidi halisi wa labda majimaji ya mbegu za kiume hayapo tena kwa sababu huyo mbakwaji tayari ameshaoga
3. Na kwa mujibu wa maelezo yaliyopo inahisiwa huyu binti ameingiliwa siku mbaya ambazo inawezekana atakuwa anaujauzito
sasa ndugu zangu naomba tusaidianae mawazo kwa sababu naamini humu kila mtu anamazo tofauti, lengo ni kusaidia kama huyu binti anaweza bado kwenda mbele ya vyombo vya sheria, na je kama bahati mbaya akapimwa akautwa tayari ana mimba au virusi vya ukimwi ni nini cha kufanya..
Karibuni kwa ushauri na maoni, tukio limetokea alhamisi usiku.