Ama kweli watanzania tumelogwa

mayoscissors

JF-Expert Member
Nov 24, 2009
975
471
Watanzania wenzangu mgomo wa madaktari kama ukija kutokea kwa mara ya pili kwani mimi siamini,lazima tujilaumu wote kwani wewe na mimi tuna nafasi ya kutetea lile ambalo ni la maslahi ya watanzania na nchi yetu.
Ugonjwa hamna mtu anayeomba augue na hamna mtu anayeweza kujihakikishia hataweza kupata ajali hivyo mgomo unakuhusu na unanihusu kwani kwa namna moja au nyigine unaweza ukajikuta unapoteza maisha wakati leo watanzania tuna nafasi ya kuiambia serikali iwaweke pembeni Waziri wa afya na naibu wake ili mchakato wa meza ya makubaliano kati ya madaktari na serikali uendelee
Watanzania wenzangu tuwe na ujasiri wa kuisemea serilkali pale inapokosea,swala la mgomo likitokea tena kwa serilaki kulindana nitajilaumu sana na nitakulaumu kama serikali hatutaisemea kama Waziri wa afaya na naibu wake watakuwa ofisini watanzania tukipoteza maisha jumatano ijayo
MUNGU IBARIKI TANZANIA
 
Ndugu zangu madaktari chonde chonde safari hii kuweni wastahimilivu kidogo kuokoa maisha ya watanzania. JK ame prove kuwa ni rais asiye msikivu, sana sana utasikia jumatatu au jumanne ameenda zake Uingereza kwa best yake David Cameron na yote yatakayotokea hatakuwepo nchini.

SULUHISHO: Mtuamuru sisi waTanzania tuandamane kwenda kuwatoa kwa NGUVU OFISINI Mponda na Naibu wake ili mambo yaishe. Hakuna aliyetegemea baada ya mateso yale waliyopata watanzania serikali ingechelea kutekeleza madai yao na hata madaktari kuamua kugoma tena, hasa dai rahisi kabisa la waziri kujiuzuru.
 
Umeongea vizuri sana mkuu. Nadhani mwangwi wa sauti yako itakua imefika mpaka pale dirishani kwake Mkuu wetu, wa sasa kwa mujibu na matakwa ya sheria, pale Magogoni.

Kuna mabadiliko yako njiani kwa kuitikia hiyo sauti yako ya upole na unyenyekevu.
 
Ndugu zangu madaktari chonde chonde safari hii kuweni wastahimilivu kidogo kuokoa maisha ya watanzania. JK ame prove kuwa ni rais asiye msikivu, sana sana utasikia jumatatu au jumanne ameenda zake Uingereza kwa best yake David Cameron na yote yatakayotokea hatakuwepo nchini.

SULUHISHO: Mtuamuru sisi waTanzania tuandamane kwenda kuwatoa kwa NGUVU OFISINI Mponda na Naibu wake ili mambo yaishe. Hakuna aliyetegemea baada ya mateso yale waliyopata watanzania serikali ingechelea kutekeleza madai yao na hata madaktari kuamua kugoma tena, hasa dai rahisi kabisa la waziri kujiuzuru.

mkuu umetoa ushauri mzuri sana wenye mantiki. Maana madactari wanapogoma watu tunashangili wale tuliowazima bila kuchukua hatua yoyote huku wagonjwa tunaumia .
 
Yuko wapi Ananilea Nkya na Deus Kibamba? mnaotaka kuandamana andamaneni mimi nabaki nyumbani, lakini kwa upande wangu nawaomba madaktari wawe na uvumilivu maana si wao tu wenye madai serikalini. Watambue kuwa watumishi wa serikali wako wengi na wote wana umuhimu katika nafasi zao je nao wakigoma itakuwaje? inawezekana wao hawana ndugu wanaohitaji tiba au wataweza kuwatibu katika zahanati zao binafsi au wanazofanya kazi part time lakini naye mwalimu akigoma wajue kuwa watoto wao hawatafundishwa, Polisi wakigoma pia watavamiwa na hata hayo madai yao hawatanufaika nayo. Ni takribani watumishi wote nchini wana madai sawa na madaktari iweje wao ambao tena serikali imeshaahidi kuyashughulikia wanaendelea kutishia tu? wafanyeje wale ambao hata kukutana na Pinda hawajawahi?
 
Haiingii akilini kumtaka Mwalimu akaandamane ili Daktari atimiziwe madai yake wakati na yeye ana madai pia.
 
Yuko wapi Ananilea Nkya na Deus Kibamba? mnaotaka kuandamana andamaneni mimi nabaki nyumbani, lakini kwa upande wangu nawaomba madaktari wawe na uvumilivu maana si wao tu wenye madai serikalini. Watambue kuwa watumishi wa serikali wako wengi na wote wana umuhimu katika nafasi zao je nao wakigoma itakuwaje? inawezekana wao hawana ndugu wanaohitaji tiba au wataweza kuwatibu katika zahanati zao binafsi au wanazofanya kazi part time lakini naye mwalimu akigoma wajue kuwa watoto wao hawatafundishwa, Polisi wakigoma pia watavamiwa na hata hayo madai yao hawatanufaika nayo. Ni takribani watumishi wote nchini wana madai sawa na madaktari iweje wao ambao tena serikali imeshaahidi kuyashughulikia wanaendelea kutishia tu? wafanyeje wale ambao hata kukutana na Pinda hawajawahi?
jamani hii logic mnayoitumia mimi siielewi kabisa, eti mbona walimu nao wana madai hawagomi...... Ooh mbona mapolisi nao wana maslahi duni hawagomi............ So whaaat???kama wao wanaridhika au ni waoga haijustify kwamba madokta nao wawe waoga. Au unataka tuongeze na madai ya walimu,mapolisi,etc kwenye madai yetu? Msitulazimishe madokta na sisi tuwe waoga waoga. Aluta continua
 
Haiingii akilini kumtaka Mwalimu akaandamane ili Daktari atimiziwe madai yake wakati na yeye ana madai pia.
Wewe si mmoja wa mafisadi wa nchi hii, unadhani hatukujui? Wacha watu wadai haki zao. Sasa ni madaktari na siku nyingine watagoma wengine.

Endelea kulala na wala hatukuhitaji!
 
Yuko wapi Ananilea Nkya na Deus Kibamba? mnaotaka kuandamana andamaneni mimi nabaki nyumbani, lakini kwa upande wangu nawaomba madaktari wawe na uvumilivu maana si wao tu wenye madai serikalini. Watambue kuwa watumishi wa serikali wako wengi na wote wana umuhimu katika nafasi zao je nao wakigoma itakuwaje? inawezekana wao hawana ndugu wanaohitaji tiba au wataweza kuwatibu katika zahanati zao binafsi au wanazofanya kazi part time lakini naye mwalimu akigoma wajue kuwa watoto wao hawatafundishwa, Polisi wakigoma pia watavamiwa na hata hayo madai yao hawatanufaika nayo. Ni takribani watumishi wote nchini wana madai sawa na madaktari iweje wao ambao tena serikali imeshaahidi kuyashughulikia wanaendelea kutishia tu? wafanyeje wale ambao hata kukutana na Pinda hawajawahi?

Wacha kuongea utumbo wewe! Kwani kukutana na pinda ndo ku solve tatizo,issue ni kwamba matakwa yao yAtekelezwe,hatA kama huyo pinda Angebaki ofisini kwake au nyumbAni lakini idimrAdi etekeleze mAtakwa yote yA madaktari,hamna mtu anayehitaji kuonana nae,itasaidia nini?

UmepAtia kusemA karibu kila sector kunA matatizo,sAsa unAwAsihi madaktari wasigome kwasababu hao wengine hawAgomi,MAdAktari wamefunguka macho.HAtA wote wakigoma ni sAwa tuu,hii inAdhihirisha serikali imeshindwA mAjukumu yake.

Nawakilisha
 
kuna Mtanzania alisema 'nchi haiendeshwi kwa mitandao ya kijamii' ...time to prove otherwise? Time will tell.
 
ndugu K-killer yaani unamaanisha kama kuna nyani wamevamia shamba lako la mahindi usichukue hatua sababu eti mashamba ya jirani zako nayo yameliwa. Nadhani ni mtazamo wa kijuha.
 
Back
Top Bottom