Akina Dr. Mwaka na mwenzie Ndodi wameacha madhara makubwa sana kwenye jamii

ebaeban

JF-Expert Member
Jan 15, 2012
2,205
2,690
Mamlaka husika ilichelewa sana kuwadhibiti hawa jamaa wamasababisha madhara makubwa sana katika tasnia ya matibabu, kikubwa walichofanya ni ile kuwa wao ni waganga wa tiba mbadala lakini wakajikita zaidi katika tiba ya kihospitali na kuanza kujitangaza kwa television.

Waganga wa kihospitali (medical personnel) huwa hawajitangazi kihivyo bali wanajamii wenyewe huwapa umaarufu kwa huduma zao wanazozipata kutoka kwao pindi wanapofika sehemu zao za kazi.
Walichokuwa wanafanya akina Dr. Mwaka ni upotoshaji mkubwa ambao umesababisha madhara yafuatayo

Wametangaza sana ati kuna ugonjwa wa UTI na mtu anaweza kupata hiyo UTI kwa kuchangia choo yaani unaweza kupata UTI chooni, hii siyo kweli ni uwongo, uwongo, uwongo. Chooni unaweza kupata uambukizo aidha kupitia miguuni kama hujavaa viatu au mikononi vidudu ukavila kama hujanawa mikono ukitoka huko.

Sasa matokeo yake akina mama wakiwashwa kidogo sehemu zao za siri huja na kusema nimepata UTI tunachangia choo. Tabu iko kwenye matibabu antibiotic za kawaida kama Tetracycline, Ampicilline au Amoxycline hawazitaki tena eti hazitibu hiyo UTI. Wanataka dawa kama Cepharexine au Ceftriaxone au Azithromax ambazo ni very broad spectrum antibiotic for nothing.

Uambukizo katika njia ya mkojo (urinary tract) upo na husabibishwa na vimelea ambavyo ni very weak antibiotic zile nilizozitaja hapo juu ni zinafaa sana.
Madhara ni kwamba hizo antibiotic wanazozitaka na wanazoamini ndizo zinatibu hiyo UTI ya akina Dr. Mwaka ambazo zinatumika sana sasa hivi zikiisha zoeleka na vimelea na vikawa sugu basi jamii itapata tabu sana kupona hata uambukizo wowote unaosababishwa na bacteria hasa hasa magonjwa ya zinaa.
 
Mi naona umeilezea zaidi UTI kuliko kuelezea madhara waliyoacha kina Dk Mwaka
Yaani madhara ya kutumia madawa makubwa kwa sababu amazo hazipo ni za kufirika hiyo UTI ya akina mwaka siyo kweli wamepandikiza katika jamii kitu amacho siyo sahihi je! siyo madhara hayo
 
Hizo broad spectrum anti biitic zimeshaanza kutengeneza usugu tayari all for nothing, Dr.Kigwangwallah tunaomba utoe tamko kwamba ni marufuku mgonjwa kudai any broad spectrum antibiotic bila kibali cha daktari aliesajiliwa, na daktari asi-prescribe hiyo antibiotic unless it is necessary, kwa UTI dawa ndogo ndogo kama ciprofloxacin zinatibu UTI vizuri tu na ni cheap. Tukiachia huu usugu uendelee basi wote tuaathirika na kuteseka sana!
 
Mi naona umeilezea zaidi UTI kuliko kuelezea madhara waliyoacha kina Dk Mwaka
Nilitaka kusema hilo mkuu na ndokubwa lililonifanya nifungue huu uzi kujua hayo madhara makubwa ila nimekutana na UTI na ugumu wa kupona bacterial infections bada ya kutumia hizo dawa. Ila sio mbaya
 
Jamii ya Tanzania ilikosa viongozi wenye kusimamia dhamana walizopewa hili limekuwa tatizo kwetu,tunahijitaji wasimamizi,Afya zetu zinadhoofika kwa mengi tu.Tuna watabibu wasio na vigezo cha kusema tutafika tu
 
Mamlaka husika ilichelewa sana kuwadhibiti hawa jamaa wamasababisha madhara makubwa sana katika tasnia ya matibabu, kikubwa walichofanya ni ile kuwa wao ni waganga wa tiba mbadala lakini wakajikita zaidi katika tiba ya kihospitali na kuanza kujitangaza kwa television.

Waganga wa kihospitali (medical personnel) huwa hawajitangazi kihivyo bali wanajamii wenyewe huwapa umaarufu kwa huduma zao wanazozipata kutoka kwao pindi wanapofika sehemu zao za kazi.
Walichokuwa wanafanya akina Dr. Mwaka ni upotoshaji mkubwa ambao umesababisha madhara yafuatayo

Wametangaza sana ati kuna ugonjwa wa UTI na mtu anaweza kupata hiyo UTI kwa kuchangia choo yaani unaweza kupata UTI chooni, hii siyo kweli ni uwongo, uwongo, uwongo.
Chooni unaweza kupata uambukizo aidha kupitia miguuni kama hujavaa viatu au mikononi vidudu ukavila kama hujanawa mikono ukitoka huko.
Sasa matokeo yake akina mama wakiwashwa kidogo sehemu zao za siri huja na kusema nimepata UTI tunachangia choo. Tabu iko kwenye matibabu antibiotic za kawaida kama Tetracycline, Ampicilline au Amoxycline hawazitaki tena eti hazitibu hiyo UTI. Wanataka dawa kama Cepharexine au Ceftriaxone au Azithromax ambazo ni very broad spectrum antibiotic for nothing.

Uambukizo katika njia ya mkojo (urinary tract) upo na husabibishwa na vimelea ambavyo ni very weak antibiotic zile nilizozitaja hapo juu ni zinafaa sana.
Madhara ni kwamba hizo antibiotic wanazozitaka na wanazoamini ndizo zinatibu hiyo UTI ya akina Dr. Mwaka ambazo zinatumika sana sasa hivi zikiisha zoeleka na vimelea na vikawa sugu basi jamii itapata tabu sana kupona hata uambukizo wowote unaosababishwa na bacteria hasa hasa magonjwa ya zinaa.
Kuna sehemu hajakosea kwa wanawake wakichuchumaa au kwenye vyoo vya kukaa ambavyo havijasafichwa vizuri na ikatokea bacteria wakaingia kwenye urinary tract wanaweza kupata hapo hamna ubishi

Labda kwa dawa wanazopewa mbali na strong antb lakini pia madawa yao yanawezaleta effect kwenye figo,ini, na sehemu nyingine za mwili

Maana madadwa ya kitaalam yanaonesha side effect, contraindication for users lakini kwao eti wote wanatumia tu hata mtu ananyonyesha, trimister nk ni hatari kutumia dawa usiojua clearance yake, absorption yake then unampa mtu
 
Mtoa Mada umejikanyaga Kwanzaa Mimi mwenyewe nishawai kutumia Dawa ya meno ambayo alinitengenezea ndodi na sijawai umwa jino tena Ila tuwatanzania wengi ni wavivu wa kufikiria na kufatilia ikiwemo kutozingatia masharti
 
Back
Top Bottom