MWANAUME mmoja anayejulikana kwa jina la Tungaraza Harison [31] amejiua kwa kunywa sumu baada ya kufumaniwa akiwa na mke wa rafiki yake kipenzi.
Tungaraza alijiua kutokana na aibu aliyoipata kwa rafiki yake huyo ambaye alikuwa karibu naye sana katika mambo yao mengi ya kila siku.
Marehemu alifumaniwa na rafiki yake akiwa na shemeji yake nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam wakati rafiki yake huyo mwenye mke alipokuwa katika shughuli zake za kawaida.
Inasemekana marehemu alikuwa na uhusiano na shemeji yake huyo bila rafiki yake kutambua kinachoendelea.
Akisimulia mkasa huo,mke wa marehemu aliyejulikana kwa jina la Ester, nyumbani kwao Ukonga Madafu jijini Dar e salaam, alisema kuwa mume wake siku moja kabla ya kujinyonga siku ya Jumapili usiku wa saa mbili alirudi huku akiwa hana furaha hata kidogo.
Mke wake huyo alisema kuwa siku hiyo usiku shemeji yake alikuja nyumbani kwao na kumpa taarifa za mumewe kutembea na mkewe hali iliyopelekea marehemu kuomba msamaha mbele ya mkewe.
Shemeji yake huyo aliondoka nyumbani kwao bila kusema chochote kama amemsamehe au la.
Inasemekana kutokana na aibu aliyoipata kwa mke wake na kwa rafiki yake siku ya jumatatu asubuhi alisubiria mke wake alipokwenda kazini aliamua kujiua kwa kunywa sumu.
Ester alisema kuwa wakati anarudi kazini alimkuta mumewe akiwa kitandani amenyooka huku mapovu yakiwa yanamtoka na huku ujumbe wa nimejiua kutokana na aibu niliyoipata, mke wangu naomba unisamehe kwa kitendo nilichokifanya cha kukutia aibu niombee samahani kwa rafiki yangu kipenzi bye ukiwa pembeni.
Source: Nifahamishe.com
Tungaraza alijiua kutokana na aibu aliyoipata kwa rafiki yake huyo ambaye alikuwa karibu naye sana katika mambo yao mengi ya kila siku.
Marehemu alifumaniwa na rafiki yake akiwa na shemeji yake nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam wakati rafiki yake huyo mwenye mke alipokuwa katika shughuli zake za kawaida.
Inasemekana marehemu alikuwa na uhusiano na shemeji yake huyo bila rafiki yake kutambua kinachoendelea.
Akisimulia mkasa huo,mke wa marehemu aliyejulikana kwa jina la Ester, nyumbani kwao Ukonga Madafu jijini Dar e salaam, alisema kuwa mume wake siku moja kabla ya kujinyonga siku ya Jumapili usiku wa saa mbili alirudi huku akiwa hana furaha hata kidogo.
Mke wake huyo alisema kuwa siku hiyo usiku shemeji yake alikuja nyumbani kwao na kumpa taarifa za mumewe kutembea na mkewe hali iliyopelekea marehemu kuomba msamaha mbele ya mkewe.
Shemeji yake huyo aliondoka nyumbani kwao bila kusema chochote kama amemsamehe au la.
Inasemekana kutokana na aibu aliyoipata kwa mke wake na kwa rafiki yake siku ya jumatatu asubuhi alisubiria mke wake alipokwenda kazini aliamua kujiua kwa kunywa sumu.
Ester alisema kuwa wakati anarudi kazini alimkuta mumewe akiwa kitandani amenyooka huku mapovu yakiwa yanamtoka na huku ujumbe wa nimejiua kutokana na aibu niliyoipata, mke wangu naomba unisamehe kwa kitendo nilichokifanya cha kukutia aibu niombee samahani kwa rafiki yangu kipenzi bye ukiwa pembeni.
Source: Nifahamishe.com