Ajali ya Umeme: Ubungo darajani umeme walipuka

barafu

JF-Expert Member
Apr 28, 2013
6,726
32,818
ImageUploadedByJamiiForums1437931112.652747.jpg

ImageUploadedByJamiiForums1437931236.778607.jpg
ImageUploadedByJamiiForums1437931275.448424.jpg
ImageUploadedByJamiiForums1437931313.535303.jpg

Hali ya taharuki ilizuka ktk eneo la Ubungo darajani mkabala na ilipo mitambo ya Gas ya Songas baada ya waya wa umeme kudondoka ghafla na kusababisha moto mkubwa kuzuka na kuunguza bidhaa mbalimbali yakiwepo "masofa chakavu",vitanda na milango chakavu ambayo ulindikwa pembezoni mwa daraja la Ubungo.


Ikumbukwe kuwa eneo lote na Ubungo,kuanzia "Mataa" mpaka darajani,TANESCO imeweka mabango ya matangazo kuzuia biashara na mkusanyiko wa watu,lkn raia wameendelea kuuza mitumba,mbogamboga,nyanya na bidhaa mbalimbali licha ya tahadhari hilo iliyo kwa namna ya maandishi.


Leo hali ilikuwa tofauti,mara baada ya waya huo kudondoka na kuwakosakosa kina mama na vijana wanaofanya biashara ndogondogo eneo hilo,baada ya ajali hiyo,wananchi walifanikiwa kupiga simu kitengo cha Dharula cha TANESCO walifika na kuzima umeme na hivyo kutoa nafasi kwa wananchi kuuzima moto.
 
Kila nikipita pale huwa nafkiria iko siku litakuwa janga la taifa.

Hata mimi nawaza hivyo pia. Nikipita nawaza mara mbili mbili kuhusu umeme mkubwa uliojuu yetu. Na mwisho wa siku lawama watapewa Tanesco. Wakati na vibao vya tahadhari wameweka.
Kama hajafa wala kuumia mtu ni jambo la kheri hivyo vingine vinatafutwa tu.
 
Watu wengine wanadhani ikitokea ajali ya moto watalipwa fidia kama wale wa mafuriko.
 
Na kesho wataendelea na biashara kama kawa. Style ya mafuriko ya jangwani.
 
Tafadhalini acheni ku COMPROMISE maisha ya watu kwa sababu ya kura.walikwisha ondolewa na sasa wamerudi na wanaachwa kwa sababu ya Oct 25th...na ni wazi baada ya kura patakuwa peupeeeeee.
 
Kama sehemu imezuiwa kufanyia biashara na bado watu wapo wanafanya biashara siku yakitokea maafa lawama zitaelekezwa kwa serikali, huyu serikali sijui ni nani?
 
Kiujumla maisha ya mtanzania yapo hatarini bila kujali yupo mazingira gani.
 
  • Thanks
Reactions: G3T
Bado wale wa pale kimara mwisho sokoni uwanjani stendi ya basi za kwenda kimara bonyokwa,vinane,kwa kichwa nknilishangaa sana alhamisi hii,nilikuta kina mama kundi wamerelax chini ya ile nguzo ya kupitisha/kusafirisha umeme mkubwa na tangazo lipo hapo hapo huku mtu mmoja akiwa kaegemea hicho kibao cha tangazo nikapiga picha nikapita
 
Hiyo sehemu naijua sana na siyo mala ya kwanza kutokea tukio kama hilo.sema ugumu wa maisha ndiyo unaopelekea watu waendelee kufanya biashara hapo.
 
Hiyo sehemu naijua sana na siyo mala ya kwanza kutokea tukio kama hilo.sema ugumu wa maisha ndiyo unaopelekea watu waendelee kufanya biashara hapo.

Hivi ni kwanini umeme mkubwa kama huu ambao unapita maeneo hatarishi usingekuwa na nyaya zenye magamba ya plastic kwa ajili ya tahadhari? au technically umeme mkubwa lazima upitishwe wazi kama ilivyo hapo leo!!
 
Hivi ni kwanini umeme mkubwa kama huu ambao unapita maeneo hatarishi usingekuwa na nyaya zenye magamba ya plastic kwa ajili ya tahadhari? au technically umeme mkubwa lazima upitishwe wazi kama ilivyo hapo leo!!

Tunaishi kwenye mazingira hatarishi sanaa,haswa sie wenye kipato kidogo.
 
Back
Top Bottom