Pascal Mayalla
Platinum Member
- Sep 22, 2008
- 50,506
- 113,626
Wanabodi,
Makala ya Jumapili ya Tarehe 22./01/2023\
Leo naendelea na sehemu ya pili ya mada ya wiki iliyopita kuhusu haki kuu mbili za kisiasa zilizotolewa na katiba yetu ya JMT ya mwaka 1977, na jinsi haki hizo zilivyotolewa na kifungu kimoja, halafu serikali yetu ya wakati huo, ikaja kuzipora kwa kuzitungia sheria batili, na baada ya ubatili huo kubatilishwa na Mahakama Kuu ya Tanzania, serikali hiyo ikafanya kitu cha ajabu, kwa kuupeleka ubatili huo Bungeni, kwa hati ya dharura, na kuliomba Bunge kufanya mabadiliko ya katiba ambayo nayo ni batili, kisha ubatili huo ukachomekewa kiubatili ndani ya katiba yetu ili kuihalalisha batili hiyo!. Haya yote yalifanyika huku Tanzania ndio nchi ya kwanza kwa nchi za Afrika Mashariki kufundisha somo la sheria, hivyo tuna manguli wa sheria wabobezi na wabobevu, makala hii inauliza, haya madudu ya ajabu hivi, yaliwezekana vipi kufanyika na huku tuna wanasheria hao manguli wabobevu na wabobezi wakiangalia?!.
Kwa wasomaji wapya, anzia hapa Madudu haya ya ajabu ya kisheria yaliweza kufanyika vipi wakati tuna Wanasheria?
Kwa mujibu wa ibara ya 64.-(1) Mamlaka yote ya kutunga sheria juu ya mambo mengine yote yahusuyo Tanzania yatakuwa mikononi mwa Bunge la JMT. Ila ibara ya 64.- (5) inasema Katiba hii itakuwa na nguvu ya sheria katika Jamhuri nzima ya Muungano na endapo sheria nyingine yoyote itakiuka masharti yaliyomo katika Katiba hii, Katiba ndiyo itakuwa na nguvu, na sheria hiyo nyingine, kwa kiasi inachokiuka Katiba itakuwa batili.
Tafsiri ya ibara hii kwa mtu wa kawaida ni katiba ndio sheria mama, ikitokea sheria nyingine yoyote iliyotungwa, ikikinzana na katiba, sheria hiyo nyingine inakuwa ni batili automatically, kisheria wanaita null and void ab initio, yaani sheria hiyo batili inakuwa ni kama haipo na haijawahi kuwepo!.
Ibara ya 64 inazungumzia kitu kinachoitwa "the supremacy of the constitution" kumaanisha Katiba ndio sheria Mama, sheria yoyote nyingine itakayo kwenda kinyume cha katiba, sheria hiyo ni batili. Ubatisho huo umefanywa na katiba yenyewe na sio Mahakama Kuu!.
Kazi ya Mahakama ni kutafsiri sheria, baada tuu ya Mahakama Kuu Kuu kuthibitisha sheria fulani ni batili kwa kwenda kinyume cha katiba, sheria hiyo inakuwa imebatilika pale pale kwa mujibu wa Ibara ya 64!. Anayebatilisha sheria batili sio Mahakama Kuu, ni katiba yenyewe!. Kazi ya Mahakama Kuu ni kuthibitisha tuu ubatili na ukiisha thibitishwa, sheria hiyo batili inakuwa imebatika automatically!.
Sheria iliyobalika automatically maana yake ni haipo hivyo hakuna rufaa!. Baada ya kubatilishwa, kazi ya serikali na Bunge ni kurekebisha na kuifuta from the books, na sio kuikatia rufaa batili!.
Ibara ya 5 ya katiba imetoa haki kuu kwa kila raia wa Tanzania aliyetimiza umri wa miaka kumi na minane anayo haki ya kupiga kura katika uchaguzi unaofaywa Tanzania. Haki hii ya kuchagua, inakwenda sambamba na haki ya kuchaguliwa kwa mujibu wa ibara ya 21.-(1) kila raia wa Jamhuri ya Muungano anayo haki ya kushiriki katika shughuli za utawala wa nchi, ama moja kwa moja au kwa kupitia wawakilishi waliochaguliwa na wananchi kwa hiari yao.
Haki hizi mbili zilizotolewa na katiba, japo haki ya kuchagua bado ipo, lakini haki ya kuchaguliwa imeporwa kwa kuwekwa shurti batili kwenye ibara ya 39 na 67 kwa shurti la kudhaminiwa na chama cha siasa!. Wakati wote wa kuwekwa kwa ubatili huu ndani ya katiba yetu, Tanzania tulikuwa na wanasheria tena ma nguli wabobezi na wabobevu, kuanzia serikalini, bungeni na mahakamani!.
Kumefanyika mambo makubwa Sita
Wasalaam.
Paskali
Rejea mbalimbali za mwandishi huyu kuhusu haki katiba "Kwa Maslahi ya Taifa"
Makala ya Jumapili ya Tarehe 22./01/2023\
Leo naendelea na sehemu ya pili ya mada ya wiki iliyopita kuhusu haki kuu mbili za kisiasa zilizotolewa na katiba yetu ya JMT ya mwaka 1977, na jinsi haki hizo zilivyotolewa na kifungu kimoja, halafu serikali yetu ya wakati huo, ikaja kuzipora kwa kuzitungia sheria batili, na baada ya ubatili huo kubatilishwa na Mahakama Kuu ya Tanzania, serikali hiyo ikafanya kitu cha ajabu, kwa kuupeleka ubatili huo Bungeni, kwa hati ya dharura, na kuliomba Bunge kufanya mabadiliko ya katiba ambayo nayo ni batili, kisha ubatili huo ukachomekewa kiubatili ndani ya katiba yetu ili kuihalalisha batili hiyo!. Haya yote yalifanyika huku Tanzania ndio nchi ya kwanza kwa nchi za Afrika Mashariki kufundisha somo la sheria, hivyo tuna manguli wa sheria wabobezi na wabobevu, makala hii inauliza, haya madudu ya ajabu hivi, yaliwezekana vipi kufanyika na huku tuna wanasheria hao manguli wabobevu na wabobezi wakiangalia?!.
Kwa wasomaji wapya, anzia hapa Madudu haya ya ajabu ya kisheria yaliweza kufanyika vipi wakati tuna Wanasheria?
Kwa mujibu wa ibara ya 64.-(1) Mamlaka yote ya kutunga sheria juu ya mambo mengine yote yahusuyo Tanzania yatakuwa mikononi mwa Bunge la JMT. Ila ibara ya 64.- (5) inasema Katiba hii itakuwa na nguvu ya sheria katika Jamhuri nzima ya Muungano na endapo sheria nyingine yoyote itakiuka masharti yaliyomo katika Katiba hii, Katiba ndiyo itakuwa na nguvu, na sheria hiyo nyingine, kwa kiasi inachokiuka Katiba itakuwa batili.
Tafsiri ya ibara hii kwa mtu wa kawaida ni katiba ndio sheria mama, ikitokea sheria nyingine yoyote iliyotungwa, ikikinzana na katiba, sheria hiyo nyingine inakuwa ni batili automatically, kisheria wanaita null and void ab initio, yaani sheria hiyo batili inakuwa ni kama haipo na haijawahi kuwepo!.
Ibara ya 64 inazungumzia kitu kinachoitwa "the supremacy of the constitution" kumaanisha Katiba ndio sheria Mama, sheria yoyote nyingine itakayo kwenda kinyume cha katiba, sheria hiyo ni batili. Ubatisho huo umefanywa na katiba yenyewe na sio Mahakama Kuu!.
Kazi ya Mahakama ni kutafsiri sheria, baada tuu ya Mahakama Kuu Kuu kuthibitisha sheria fulani ni batili kwa kwenda kinyume cha katiba, sheria hiyo inakuwa imebatilika pale pale kwa mujibu wa Ibara ya 64!. Anayebatilisha sheria batili sio Mahakama Kuu, ni katiba yenyewe!. Kazi ya Mahakama Kuu ni kuthibitisha tuu ubatili na ukiisha thibitishwa, sheria hiyo batili inakuwa imebatika automatically!.
Sheria iliyobalika automatically maana yake ni haipo hivyo hakuna rufaa!. Baada ya kubatilishwa, kazi ya serikali na Bunge ni kurekebisha na kuifuta from the books, na sio kuikatia rufaa batili!.
Ibara ya 5 ya katiba imetoa haki kuu kwa kila raia wa Tanzania aliyetimiza umri wa miaka kumi na minane anayo haki ya kupiga kura katika uchaguzi unaofaywa Tanzania. Haki hii ya kuchagua, inakwenda sambamba na haki ya kuchaguliwa kwa mujibu wa ibara ya 21.-(1) kila raia wa Jamhuri ya Muungano anayo haki ya kushiriki katika shughuli za utawala wa nchi, ama moja kwa moja au kwa kupitia wawakilishi waliochaguliwa na wananchi kwa hiari yao.
Haki hizi mbili zilizotolewa na katiba, japo haki ya kuchagua bado ipo, lakini haki ya kuchaguliwa imeporwa kwa kuwekwa shurti batili kwenye ibara ya 39 na 67 kwa shurti la kudhaminiwa na chama cha siasa!. Wakati wote wa kuwekwa kwa ubatili huu ndani ya katiba yetu, Tanzania tulikuwa na wanasheria tena ma nguli wabobezi na wabobevu, kuanzia serikalini, bungeni na mahakamani!.
Kumefanyika mambo makubwa Sita
- Kwanza umetungwa muswada sheria batili inayokwenda kinyume cha Katiba. Sheria ya Uchaguzi Act. No. 1 ya mwaka 1985. Mchakato wa utungaji wa sheria unawahusisha wanasheria na unaanzia serikalini, ilikuweje kuweje, wanasheria wetu, wakatunga sheria batili inayokinzana na katiba!, hawa wanasheria walio draft sheria hiyo batili ni wanasheria wa aina gani?
- Muswada huo wa sheria batili ukatua Bungeni, nako kuna wanasheria manguli, wabobezi wabobevu. Bunge letu tukufu la JMT, likatunga sheria batili hiyo ya uchaguzi. Mchakato wa utungaji sheria wa Bunge pia unahusisha wanasheria kwa kila hatua chini ya mwanasheria mkuu wa serikali kuhakikisha kila sheria inayotungwa na Bunge letu lazima iendane na katiba!, sheria hii batili ya uchaguzi iliwezekanaje kutungwa ili hali Bunge letu limeshehenezwa na wanasheria manguli wabobezi na wabobevu?.
- Mchungaji Mtikila (Mungu amrehemu) mwaka 1993, alifungua kesi No. 5 ya 1993, kupinga kipengele kinachomtaka mgombea uchaguzi kudhaminiwa na chama cha siasa. Mahakama Kuu kupitia kwa Jaji Kahwa Lugakingira, (Mungu amuweke mahala pema peponi), ikatamka wazi na bayana kipengele hicho ni batili na kinakiuka katiba ya JMT ya mwaka 1977, hivyo kifutwe, na kutoa haki kwa kila Mtanzania ana haki ya kushiriki kugombea Uongozi.
- Mahakama Kuu inapotamka sheria fulani ni batili kwa kwenda kinyume cha katiba, kipengele hicho kilipaswa kufutwa pale pale kwa mujibu wa ibara ya 64.- (5) katiba itekelezwe pale pale kwa sheria hiyo kuwa batili kuanzia ilipotangazwa, na ni mara baada ya uamuzi huo wa mahakama kuu kuutangaza ubatili huo, ndipo sarakasi za mambo ya ajabu ya kisheria zilianza!. Mtu anapokutwa na hatia na kuhukumiwa kifungo jela, hupelekwa jela, kuanza kutumikia kifungo hata kama kama atakata rufaa. Hivyo uamuzi huu wa mahakama ulipaswa kuanza kutekelezwa pale pale!.
- Kama katiba ndio sheria mama, Mahakama Kuu chini ya Jaji Lukakingira, ikatamka sheria hiyo ni batili, kwasababu inakwenda kinyume cha katiba, mamlaka pekee nchini Tanzania, yenye mamlaka ya kutafsiri sheria na kueleza ubatili wa sheria yoyote ambayo inakwenda kinyume cha katiba, ni Mahakama Kuu ya Tanzania, baada ya hukumu ya Jaji Lugakingira, ni wanasheria wa aina gani walioishauri serikali kukata rufaa?.
- Hili ni tundu kwenye paa letu la mhimili wa Mahakama, baada ya mahakama kuutangaza ubatiliti huo, kitu kikisha kuwa batili, ni ni kama hakipo na hakijawahi kuwepo!, hatua ya kwanza ni kwanza hiyo sheria kubadilishwa kwa kuwa null and void ab initio, hivyo ilibidi ifutwe pale pale!.
Wasalaam.
Paskali
Rejea mbalimbali za mwandishi huyu kuhusu haki katiba "Kwa Maslahi ya Taifa"
- Sheria ya Uchaguzi Ni Bad Law! Kuendelea Kuitumia ni Ujinga? Kuwabebesha Masikini Gharama za Uchaguzi ni Dhambi!
- Shurti la kudhaminiwa na chama kugombea uchaguzi, ni shurti batili kwa mujibu wa Katiba, linatutia hasara, tulifute!.
- Mgombea Kudhaminiwa na Chama ni Ubatili Uliochomekwa Kiubatili na Bunge Letu Ndani ya Katiba Yetu!. Tuache Ubatili Huu Uendelee Ndani ya Katiba Yetu?
- Asante Rais kuruhusu mikutano, tunakuomba uruhusu haki nyingine ambayo imeporwa ya Watanzania wote kuchagua na kuchaguliwa
- Anayekuja pasi na hodi, huondoka pasi kuaga. Kuzuiwa bila kifungu, kuruhusu bila Kifungu. Ni hisani ya Rais Samia. Haki kuhisaniwa hadi lini?
- Watanzania ni maneno maneno na kulialia, Vitendo 0. Katiba ni maneno tu! Je, 2023 tuendeleze maneno matupu na kulialia au tubadilike tufanye kitu?
- Haki Huinua Taifa! Rais Samia kwa Kauli na Matendo ameonesha ni mtu wa Haki. Akitekeleza hili kama alivyosema, atabarikiwa, Tanzania itabarikiwa
- Asante Mungu kwa Rais Samia: Ni Msema Kweli na Mtenda Kweli, Ni Msema Haki na Mtenda Haki. Je, Ataruhusu Ubatili Huu Kuendelea Ndani ya Katiba Yetu?
- Asante Rais Samia kwa kuwasisitiza watendaji wa vyombo vya haki kuwa haki sio hisani, bali ni stahiki. Watende haki, tubadili Katiba kurudisha haki
- Samia Mpango wa Mungu kwa Tanzania: Kwa Hili, Atabarikiwa!, Taifa Litabarikiwa!. Asante Mungu kwa Samia, Mungu Mbariki Samia, Mungu Ibariki Tanzania
- Asante sana Rais Samia kwa kuliponya Taifa. Umeonesha kwa kauli na matendo; tunajenga nyumba moja, hakuna sababu ya kugombea fito!
- Madudu haya ya ajabu ya kisheria yaliweza kufanyika vipi wakati tuna Wanasheria?